Naona umekuja hapa kama kipofu, hujuia hata nini kilisemwa TLS na nini ambacho Mama amefanya leo.
kuweka kumbukumbu sawa hapa JF, TLS walisema kuapishwa kwa Mama Samia Suluhu kuwa rais maana yake ni kuvunjwa kwa baraza la mawaziri la zamani. Na kuundwa kwa baraza jipya kunaanza kwa kuteua waziri mkuu mpya ambaye kisheria anapitishwa bungeni kwanza kabla ya kuapishwa, na ndio mawaziri wengine wafuate kuteuliwa na wote wataapa kwa rais mpya!
Sasa leo mama Samia katangaza baraza lake la mawaziri (kabla ya kuteua kwanza waziri mkuu wake na kwenda bungeni kupitishwa)! Alichokifanya mama Samia ni kama anajichanganya, hajui afanye nini na kipi asifanye. Anadandia ukweli na kuuchanganya na uongo.