Mwabukusi akigombea uraisi dhidi ya Samia, na akaungwa mkono na vyama vyote vya upinzani, atapita kirahisi sana kuwa raisi. Hatapita ikiwa atagombea uraisi kupitia chama kimoja cha upinzani. Kampeni yake anaweza kuifanya kama uchaguzi wa kupiga kura kama referandum kuhusu bandari zetu, misitu yetu, ardhi yetu, madini yetu, mbuga zetu na Tanganyika yetu, ili kule visiwani wabaki na Zanzibar yao tuwe na muungano uliosawazika. Hapo Samia na CCM hawatafua dafu!
Hebu fikiria, unapiga kampeni unasema wale wote wanaoona bandari zetu, mbuga zetu, madini yetu, misitu yetu havipaswi kupewa waarabu wa nje wanipigie kura tuzuie hili! Wale wote wanaoona kwamba Tanganyika tunapaswa kuwa na serikali yetu ili tuamue mambo ya Tanganyika sisi wenyewe na Wazanzibar waamue mambo yao wenyewe wanipigie kura ili nibadilishe hili, make Tanganyika great again!!!!!!!i!
View attachment 3143641