Tofauti Kati ya Watawala na Viongozi: Je, Tanzania Yetu Ina Viongozi au Watawala?"

Tofauti Kati ya Watawala na Viongozi: Je, Tanzania Yetu Ina Viongozi au Watawala?"

Je, Tanzania Yetu Ina Viongozi au Watawala?"

  • A. Ina Viongozi

    Votes: 1 7.1%
  • B. Ina Watawala

    Votes: 12 85.7%
  • C. Sifahamu

    Votes: 1 7.1%

  • Total voters
    14
  • Poll closed .
Sifahamu chochote, ila ambacho nina uhakika nacho ni hiki. Kiongozi yoyote wa ummah, ni zao la jamii anayotoka. Hivyo tabia za kiongozi huakisi mno tabia na aina ya jamii inayotawaliwa....

Tusiwatenge viongozi kama ni binadamu wa aina nyingine tofauti na sisi. Hujiulizi kwanini, watu wanaoonekana ni wazalendo na wachukia ufisadi, hubadilika mno pindi wamepata madaraka.

Mwanafalsafa wa kijerumani Max Weber anasema ukiona kiongozi anaishi kama mtawala "mfalme" na anategemea sana nguvu zake na hulka "charisma" kuliko sheria, kanuni na taratibu basi fahamu fika kwamba jamii anayoiongoza iko nyuma mno kimaendeleo.

Tembea sehemu muhimu za nchi hii kama, taasisi za kielimu, masoko ya ummah, maofisi ya ummah, hospitali za ummah na taasisi za kifedha, halafu angalia aina ya watu waliopo huko ndiyo utafahamu kwanini Tanzania ipo hapa ilipo. Kuna hatari kubwa mno.

Watanzania tusitafute mchawi kabisa, ilhali sisi wenyewe ni watu wa hovyo. Jamii ambayo imejiaminisha kwamba fedha, mali na starehe ndiyo malengo makuu ya binadamu hapa duniani, usitegemee itakuza viongozi wazuri.

Vijana leo hii wanaingia kwenye siasa au wanafanya kazi ili wapate ukwasi wa kupondea raha. Waende sehemu wanywe pombe, wapate wanawake, wawe maarufu au wapate vyeo.

Hedonistic Societies are inherently destructive. Ancient Rome is a prime example.....
Kwa hiyo tabia ya watawala wetu ni zao jamii yoote.
 
Kwa hiyo tabia ya watawala wetu ni zao jamii yoote.
Wewe na mimi, hatuko tofauti sana na watu kama Raisi Kikwete, Magufuli, Mkapa na Nyerere. Unaweza kukataa sasa hivi kwasababu tu hauko madarakani, ila huo ndiyo ukweli.

Mantiki rahisi ni hii, kama Kikwete, Magufuli, Mkapa na Nyerere wangekuwa na tabia za tofauti na jamii wanayoitawala basi wasingeweza kukusanya na kutegengeneza magenge makubwa ya mashabiki ambao walikuwa radhi hata kuua ili kuwafurahisha wenyewe.

Raia hujiona wenyewe ndani ya kiongozi, ndiyo maana atampenda huyu na kumchukia yule. Hata kwenye dini iko hivo, wafuasi wa dini fulani hufuata na kuakisi tabia za miungu wa dini zao. Mahusiano baina ya raia na mtawala hayana utofauti sana na yale baina ya mungu na mwanadamu. Hivi ndivyo dunia ilivyo..
 
Back
Top Bottom