Nakubaliana na maelezo yako lakini kama wewe ni mfuatiliaji wa mijadala ya Diamond ungegundua kwamba wengi wao raha yao ni kuona Diamaond anapotea... na hili wanalisema wazi wazi... huyo Somji niliyemtaja ni mfano tu coz' nisingeweza kumtaja kila mtu! Sidhani kama hao uliowataja watu walikuwa wanawaombea mabaya bali walikuwa tu against na tabia zao!!NasDaz kauli ya Somji Juma hatuwezi kuitumia kama conclusion ya mada iliyopo mezani. Kwa sababu yeye ni mmoja kati ya wengi wanaopaza sauti zao hapa jamvini.
Mashabiki wanapo zomea ni njia mojawapo ya kuonyesha kuna kitu fulani ambacho hakipo sawa. Au kimekuwa ni kinyume na matarajio yao.
Ndiyo maana wasanii wakomavu huwa wanatoa press release ktk matukio kama haya. Especially kuomba msamaha mashabiki wao. Kwa kuwa wanajua watakuwa wameumia nafsi zao. Na wakati mwingine tukio linaloongelewa halihusiani kabisa na fani ya msanii.
Nitakupa mifano kama mitatu. R Kelly alipofikishwa mahakamani kwa kosa la kujihusisha kimapenzi na Aaliyha. Mashabiki wake walichukia sana kwa sababu Aaliyha alikuwa bado hajatimiza umri wa miaka 18!! Hili halihusiani kabisa na muziki. Ni maisha yake private. Lakini watu walisusa kununua kazi zake na hata albamu zake alizotoa baada ya tukio lile hazikupata support kubwa. Kifupi zili flop!!!
Tiger Woods aliopokamatwa ugoni na mkewe. Kitu cha kwanza aliomba msamaha mashabiki wake kwa kuwakosea. Hujiulizi hili lina uhusiano gani na golf? Kilichofuata pale ni nini? Tiger Woods alishuka toka No.1 mpaka sijui No.7 na imemchukua miaka kadhaa kurudi tena ktk top positions.
John Terry (Captain wa Chelsea na England Football Team) alipokumbwa na kashfa ya kutembea na mke wa mchezaji mwenzake. Mashabiki sio tu walimzomea kila alipoingia uwanjani bali walipaza sauti ya kuwa hafai kuongoza kikosi cha England kwa sababu ya maadili. Na kweli alivuliwa ukepteni akapewa Rio Ferdinand!!!
Michael Jackson alipokumbwa na kashfa ya kunajisi mtoto mdogo. Ndo ulikuwa mwanzo wa anguko lake la kimuziki. Ule msongo aliopata ulimpelekea kujiingiza ktk matumizi ya madawa hadi kifo chake. Management yake ilikanusha lakini pia iliwaomba msamaha mashabiki kwa kuwaumiza mioyo yao!!!
Nimetoa mifano hiyo michache kwa nini?? Ninataka kukuonyesha kuwa watu wakishakukupenda sana. Inabidi uangalie muenendo wa wa maisha yako. Ndiyo maisha ni yako lakini yana athari kubwa kwa wapenzi wako. Especially matamshi yako. Ukiwa Star wewe ni watu. So chochote utakachofanya kinyume na matarajio yao, ujiandae...
Ndo maana halisi ya kioo cha jamii. Watu wanakuangalia wewe kama mfano. Sasa kama wewe ni mjivuni/malaya,mlevi n.k sidhani wewe uta fit hiyo role ya kioo cha jamii.
Kuna mifano mingi hapa nyumbani nikupe mmojawapo. Unamkumbuka yule dada wa African Stars mnenguaji mahiri ambaye watu walimpenda sana? Alipoanza vituko vya madawa ya kulevya na picha za utupu sijui. Watu walimchukia na wala hawakuwa na huruma naye. Angeweza kusema ni chuki kwa mafanikio aliyoyapata ktk fani.Kwa nini?!! Kwa sababu ukishapendwa na watu wanategemea wewe utajiheshimu au you behave in a certain way. Kwani kuna watoto wao wanakuangalia wewe kama kioo...
Nadhani umenielewa na wengine wote wenye mtazamo kama wako. Tusikimbilie majibu mepesi kama wivu,husda,chuki nk.
Uliza sababu za msingi zinazowafanya wamuombee mtu mabaya... lakini hakuna atakayekupa jibu... afadhali umetaja uovu wa akina Tiger Wood na MIchael Jackson! Uliza hao wanaotamani kuona Diamond ameshuka, kijana amefanya nini hasa so serioua... hakuna mwenye jibu! Wapo watakaokuambia ameikashifu Mbeya... ukiwaomba source inayoaminika iliyomnukuu Diamond akiiponda Mbeya, hakuna atakayekupa! Sasa wenye akili zao wanajiuliza... Diamond ambae anapiga show hadi wilayani na miji midogo kama TUnduma, hivi kweli inaingia akili azikashifu hotel za Mbeya?? Wengine wanadai oh, jamaa ni malaya sana... nani kasalimika? Huyo KIba mwenyewe wanayemlinganisha nae amezaa na wanawake watatu tofauti na wote amewapiga chini... kwahiyo Diamond akichapa akina Wolper inakuwa nongwa, lakini wengine wakizalisha huku na kule ni sawa tu!! Hata hao wanaosema Diamond ana dharau ukiwaliza dharau ipi wamefanyiwa wao kama wao, hakuna mwenye jibu! Kuna mtu humu amedai kwamba wakati Diamond anauza mitumba Magomeni alikuwa mshikaji wa jamaa mmoja ambae member wa humu JF ni mtu wake wa karibu! Lakini member huyu anadai hivi sasa Diamond hamkumbuki kabisa huyo jamaa.... aaaaaargh! Hili nalo limfanye mwingine kuwa na nongwa??
Kutokana na watu kutokuwa na hoja za msingi ndio maana wengine tunashawishika kuamini kwamba wengi wao wanasukumwa na chuki na wivu kwavile mtu asiye na husuda hawezi kuombea kuona mtu mwingine anaanguka tena kwa sababu ambazo wala hazikuhusu moja kwa moja!