Tofauti na mfanano wa kikazi na kimamlaka kati ya CIA na FBI

Tofauti na mfanano wa kikazi na kimamlaka kati ya CIA na FBI

CIA ni majasusi wanaokusanya na kuchambua habari za mataifa na raia wa nchi nyingine ili kusaidia mikakati na sera za Marekani.

FBI ni wapelelezi wanaohusika zaidi na mambo ya ndani ya Marekani na wananchi wake, pia wana nguvuvu kisheria kuweza kukamata au kuchukulua mtu hatua tofauti na CIA.
 
Kwanini nchi yetu haiundi vyombo vya kitaalamu kama hivi?

Unakuta mtu kama msukuma eti ndio usalama wa Taifa!??

Nchi inajengwa na wananchi. Tuijenge nchi kwa uzalendo.
 
Kwa uelewa wangu mdogo CIA wanadeal na masuala ya intellijensia nje ya marekani kwa mfano kama kuna threat yoyote ambayo iko targeted to US , CIA ndo wanaenda kusolve. FBI wanadeal na masuala ya intellijensia na ulinzi ndani ya US , hawavuki nje ya boarders za US
 
CIA ni shirika la kipelelezi la marekan linalofanya upelelezi nje ya mipaka ya US. Maafisa wa CIA wamejaa dunian kote hata hapa Tanzania wapo mfano mimi hapa.

FBI hili ni shirika la kipelelezi linalo operate ndani ya mipaka ya US. Maafisa wake wamejaa marekani nzima,mfano mange kimambi
 
CIA ni shirika la kipelelezi la marekan linalofanya upelelezi nje ya mipaka ya US. Maafisa wa CIA wamejaa dunian kote hata hapa Tanzania wapo mfano mimi hapa.

FBI hili ni shirika la kipelelezi linalo operate ndani ya mipaka ya US. Maafisa wake wamejaa marekani nzima,mfano mange kimambi
Haaaaaa wewe lazima utakua ndugu musiba
 
FBI inaanza na herufi ya F na CIA inaanza na herufi ya C. Kwenye CIA herufi inayofuata ni I wakati FBI inafuata B. Halafu FBI inamaliza na I wakati CIA inamaliza na A.

Hiyo ndiyo tofauti MKuu.
Ahahaha
 
CIA ni shirika la kipelelezi la marekan linalofanya upelelezi nje ya mipaka ya US. Maafisa wa CIA wamejaa dunian kote hata hapa Tanzania wapo mfano mimi hapa.

FBI hili ni shirika la kipelelezi linalo operate ndani ya mipaka ya US. Maafisa wake wamejaa marekani nzima,mfano mange kimambi
Haahaha umetisha mkuu
 
FBI ni polisi aliyespecialize kwenye upelelezi , CIA ni usalama wa taifa
FBI sio polisi ni kitengo kingine kinachojitegemea. Japokuwa mtu akiwa nq background ya kuwa polisi inakuwa rahis kuvhukuliwa.
 
Usalama wa taifa wanaitwa wapo *Secret service*
Secret service si usalama wa taifa. Wale ni kitengo cha ulinzi wa rais. President protection.
Hawahusiki na kazi wanazofanya kina CIA na FBI
 
NSA ndo usalama was taifa
NSA si usalama wa taifa. Ni shirika la kupepeleza mawasiliano... na hawa jamaa wanafuatilia email, mawasiliano ya simu, na mawasiliano yoyote yale.

Wakifanikiwa kugundua taarifa za mawasiliano ya adui ..taarifa hupelekwa CIA au FBI kwa ajili ya ukamataji wa adui.. au jumdhibiti adui.
 
Marekani kuna mashirika ya
a) Kiupelelezi ambayo ni

1. C.I.A -upelelezi wa kimataifa/ukachero,na halipo chini ya wizara yoyote,linajitegemea.
2. N.S.A-upelelezi wa mitandaoni,linalinda njia kuu za mawasilaiano ya electronik ya nchi,kuiba data za nje kwa mitandao,lipo chini ya wizara ya ulinzi,na kwasasa ndiyo kubwa kwa idadi ya wafanyakazi na bajeti.
3. D.I.A-Upelelezi wa kijeshi,juu ya uwezo wa kijashi wa nchi nyingine,wapo chini ya wizara ya ulinzi

b) Uchunguzi/kipolisi

1. F.B.I-Hawa ni polisi wa ngazi ya kitaifa(federal polisi),wanahusika na uhalifu unaohusisha zaidi ya jimbo mji mmoja/matuiko ya kijimbo,lipo chini ya wizara ya sheria...

Huonekana katika balozi mbalimbali,kwakuwa ubalozi wa nchi A ndani ya nchi B kwasheria za kimataifa ni sawa na eneo la nchi A

Yaani, ubalozi wa marekani ndani ya Tanzania,ni sawa na eneo lilipo ndani ya mpaka wa marekani.
Note: Marekani kuna polisi wa ngazi ya mji e.g NYPD, LAPD etc na polisi wa kijimbo/taifa i.e F.B.I

2. U.S MARSHALS -hawa uhusika na ulinzi wa majaji,kusafirisha wafungwa,kutafuta wafungwa waliopotea,na wale walio katika parole
3. D.E.A-hawa uhusika na masuala ya madawa ya kulevya,ndani na nje ya nchi.
4. SECRET SERVICE-hawa uhusika ulinzi na usalama wa viongozi wa ngazi ya juu katika serili, viongozi wastaafu,wagombea uraisi na familia ya viongozi hao,lakini pia hawa uhusika usimamizizi wa noti za marekani, kuepusha fedha fedha feki. wapo wenye uniform na wale waio na uniform

Kimsingi U.S.A kuna mashirika ya kiusalama yasiopungua 16, na hayo ni baadhi.
 
CIA Hawaruhusiwi kisheria kufanya kazi ndani ya USA , FBI wanafanya kazi ndani ya USA tu au katika special occasion pale wanapoitwa ku provide utaalamu
Kaka haukosawa, kumbuka tukio la la US EMBASSY BOMBING IN E.AFRICA, waliokuja ni FBI.
FBI wanadeal na UCHUNGUZI wa masuala ya KIHALIFU, ndani na nje ya US.

CIA wao ni MAJASUSI wanadeal na masuala ya kiuchumi,wanachunguza mipango yote katika nchi zote za nje ya marekani kuona waibe nini US iendelee,nani ni kikwazo wamuue au wamuangushe,muna mpango gani na silaha gani kiulinzi NK.
 
Umeshindwa kuelewa CIA wanafsnya kazi ya kupata na kuchunguza taarifa international , kisheria haruhusiwi kufanya kazi ndani ya marekani , FBI wanafanya kazi ndani ya marekani na njee pale tu watakapoitwa na taifa usika kusaidia katika uchunguzi au operation, CIA wakipata taarifa ambayo inahusu mtu kufanya uharifu wanawaambia taarifa hizo FBI , CIA ni mashushu tena wengi hawajulikani.
[emoji3][emoji3][emoji3]kakaaaa,mzee baba siyo hivyo.
 
Back
Top Bottom