Tofauti ya kuoa au kuolewa na sogea tukae

Tofauti ya kuoa au kuolewa na sogea tukae

luchelele mzunguko

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2021
Posts
1,206
Reaction score
1,641
Wakuu mimi ninavyofahamu ni kwamba ndoa ni makubaliano ya mwanaume na mwanamke ya kuwa mume na mke.

Lakini makubaliano haya yawe yamedhibitishwa eidha na watumishi wa Mungu au viongozi wa kimila kwa mujibu wa ndoa za kimila au na Hakimu kwa mujibu wa ndoa za kiserikali zote hizi wakiwepo mashahidi wa pande zote mbili za wale wanao funga ndoa wakiwekeana viapo na mambo mengine kulingana na muktadha husika hukiitimishwa kwa kuvishana pete na kutunukiwa vyeti vya ndoa yaani hati miliki na udhibitisho wa kwamba makubaliano yao yapo sawa kisheria.

Sasa tujadili kwa kueleweshana maana siku hizi vijana wanachukuana tu na kuanza kuishi pamoja almaharufu kama sogea tukae na kuanza kuitana mume na mke, hii si sawa kisheria na ndio imekithiri kwa sasa wasichokijua wanawake ni kwamba siku wamegombana na kuamua kutengana hata kama mwanamke alichangia mwanaume kutengeneza mji atashindwa kupata mgawanyo wa mali kwakuwa hana cheti cha ndoa kinachothibitisha kwamba huyu ni mume wake.

Karibuni tulijadili hili jambo kwa manufaa ya wengi
 
Watu wenyewe wa sogea tukae wengi wanaishi geto watagawana nin?..ukiwapa cheti ni matumizi mabaya ya karatasi na sahihi...
Lakini kikubwa furaha na aman katka ndoa..heher
Sasa ikitokea mmoja kashikwa ugoni au matatizo mengine yatayo sababisha kupelekana mahakamani.

Lazima mahakama kwanza hiombe uthibitisho kwamba je kweli wawili awa ni mume na mke.Sasa hili ndio la kuulizana itakuaje!
 
Sasa ikitokea mmoja kashikwa ugoni au matatizo mengine yatayo sababisha kupelekana mahakamani.

Lazima mahakama kwanza hiombe uhibitisho kwamba je kweli wawili awa ni mume na mke.Sasa hili ndio la kuulizana

Sasa ikitokea mmoja kashikwa ugoni au matatizo mengine yatayo sababisha kupelekana mahakamani.

Lazima mahakama kwanza hiombe uhibitisho kwamba je kweli wawili awa ni mume na mke.Sasa hili ndio la kuulizana itakuaje!
Haya mambo ya ndoa magumu sana, hayana formula..utakachofanya no sahihi kikubwa uwe happy tu...mambo ya kugawana muulize kylin wa mengi
 
Back
Top Bottom