Wanabodi,
Ushindi mnene, mnono, mtamu wa raha ni ule ushindi unaotokana na kupatikana kwa ushindani halali wa haki unaopatikana na kuendeshwa kidemokrasia kwenye uwanja ulio sawa, a level playing ground na sio ushindi wa uwanja tenge!, wala sio ushindi wa mezani!. Ushindi wa dhulma, unabeba a bad karma repercussions, hivyo ukifika muda wa karma pay back time, mtashangaa tuu watu wanapukutika, bila kujua sababu kumbe ni karma inakula vichwa!.
Hivyo natoa wito kwa serikali ya CCM, chini ya Jemedari wake, JPM, kiukweli labisa, hata kabla ya uchaguzi, CCM tayari imeishashinda kwa ushindi wa kishindo sio tuu huu Uchanguzi wa Serikali za Mitaa, bali hadi Uchanguzi Mkuu ujao wa mwakani 2020 kutokana na sababu za ki political social dynamics ya Magufulification nilizoeleza lakini ili CCM iweze kuufurahia huo ushindi kwa furaha ya kweli na hivyo kusheherekea ushindi huo, lazima CCM ishinde kwenye ushindani wa kweli, ushindani wa haki na ushindani wa usawa na sio kupata ushindi kwa kufanya figisu ili washindani wako wasuse, watie mpira kwapani na wewe upewe ushindi wa mezani!. Ushindi wa hivi sio ushindi mtamu, wala hauleti raha ya kudumu kwasababu karma itaingilia kati kuja kuikatisha hii raha kwa kula vichwa!.
Naomba nimalizie kwa ile kauli ya thread hii
"Ushindi Mtamu ni ushindi unaopatikana kwa ushindani wa haki kwenye uchaguzi huru na wa haki, unaaendeshwa na Tume huru na shirikishi ya uchaguzi na unaofanyika kwenye uwanja sawa wa ushindani wa kisiasa, sio huu uwanja tenge tulionao, na kupata ushindi wa mezani!.
Mheshimiwa Rais, wetu, Dr. John Pombe Magufuli, aka.JPM, kasi yako ya maendeleo ya Tanzania unaoifanya, ina ku guarantee utailetea CCM ushindi safi wa kishindo cha halali katika uchaguzi wowote, tunakuomba sana!, sana!, sana!, "Please! Please! Please!, ruhusu tuu ushindani wa haki, wazi na usawa kwa vyama vyote, kushiriki uchaguzi kwa uhuru na haki sasa kwa wote!, utabarikiwa zaidi na zaidi, na Tanzania tutabarikiwa!, ukiruhusu hizi figisu zinazoendelea, hazina hatima njema kwako, kwa chama chako wala kwa nchi yetu, kwasababu kuna lijamaa fulani linaitwa karma'hilo linataka haki bin haki!, usipotenda haki, lenyewe linaingiliaga kati na halijuagi cha nani wala cha nini!, lenyewe ni haki haki tuu bin haki usipotenda haki!, karma itaingilia kati, na kwa vile no one knows what karma will do, it's better kutenda haki kuiepuka adhabu ya karma !.
Nawatakia Jumapili Njema
Paskali