Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Subiri jumatatu tutasoma mengi.

Wahusika msifunge hii kitu tafadhalini. Huu ndio wakati wa ukweli na uwazi. Tuwekane sawa.

Mtoa mada heshima kwako!
Aisee ngoja nikuunge mkono,huu uzi usifungwe uwe ni wa kudumu,ila members tuutumie kwa uaminifu ili kuijengea heshima JF,kuirahisishia serikali na kuirahisishia jamii kufast track kero zetu kwenye platforms husika.
 
Ndugu wana JF.

Nchi imetafunwa mno hii na hawa mchwa. Sasa tuseme imetosha. Tumsaidie rais Mzalendo Dr JPM kuendelea kufyeka haya matango pori.

Weka taarifa yako hapa ili isaidie kutumbua. As far as Magufuli ni mfuatiliaji atanusa hapa tuuu.

Karibuni sana.
Mkuu wewe ni kichwa-THE GREAT THINKER!

Kwa style hii sasa wana JF wote wanageuka kuwa usalama wa taifa, kazi ya Usalama wa Taifa ni ya kila mzalendo mwenye mapenzi mema na nchi.

Natamani huu uzi uwe ni wa kudumu ili kumrahisishia JPM kuiweka nchi kwenye mstari mnyoofu wa nyuzi 180.
 
Barabara ya kuingia kituo cha mabasi cha SIMU 2000 ( mawasiliano) iwekwe lamiharaka ni kero kubwa.
2. Kitua chamabasi yaendyomikoani Ubungo kijengwe haraka.
Kipande chenyewe ni kidogo sana!halafu kila siku wanakusanya ushuru pale getini,hiyo pesa waibane waweke lami pale.
 
Kwa level ya JPM, hayo ni chunusi tu, hata Katibu Mkuu anamudu!
Ni kweli ndugu majipu ya kumkabidhi Magufuli kama ya Bandarini...

Meno ya Tembo twiga kupanda ndege.... Escrow hiyo nikwa uchache napia unapoweka Jipu lazima liwe na Taarifa za kutosha.

Mimi jipu langu ni CCM hili ndio limeharibu hii NCHI, likitumbuliwa hili basi Tanzania imepona
 
Jipu hili hapa:

Kuna meli huleta malighafi za viwanda vya Saruji nafikiri malighafi hiyo juitwa "crinca" material hayo huwa na uzito mkubwa, mwenye tenda ya kuyatoa badarini akisema afuate sheria kama wanavyotaka TANROADS haiwezi kupata faida kwani atalazimika kukodi magari mengi au magari aliyonayo yatalazimika kurudia mara nyingi.

Ili kuepuka hilo, mwenye tenda hutoa kama 20mln kwa msimamizi wa vijana Wa mzani hasa ule unaotembea na baada ya hapo wale wafanyakazi wanapatrol usiku na mchana huagizwa wasionekane katika barabara ambako mzigo huo utapita, baada ya mwenye tenda kuwa amemaliza mzigo wake bandarini humpigia mhusika sim basi mzani hurejea kazini kama kawaida. Hapo watanyanyasa watu mchanga, kokoto, matofali, vifusi, mawe nk.

Hilo ndo jipu linalotakiwa kutumbuliwa ili kuokoa Barbara zetu na kuongeza mapato
 
Jipu: HESLB ni jipu kubwa sana, kuanzia mwezi wa nne tegemeeni migomo mingi sana vyuoni. Wametoa waraka kwamba hela zikishakuja chuo zitakaa chuo siku saba na usipo sign zinarudi board.

Tatizo hapa ni kuwalazimisha wanafunzi kulipa ada kabla ya ku sign hilo boom kitu ambacho kitakuwa kigumu kwa sababu wanafunzi wengi hutegemea hizo hela kulipa ada.....

Magufuli chukua tahadhari mapema.
 
Jipu lipo barabara ya Makumbusho kituoni. Ni mbovu sana na mvua ikinyesha magari na vyombo vyote vya usafiri vinatuama sana na kuharibikia hapo, pia gari inabidi ziwashushie abiria njiani ili wakwepe hiyo barabara....

Hili ni jipu kwa injinia wa wilaya ya kindoni anatakiwa awajibike hii barabara iweze kupitika kwani magari mengi yanashindwa kufika kituoni


Ugalila, barabara za makumbusho kuingia kituo cha mabasi ipo chini ya halmashauri ya kinondoni na tayari bajeti yake ipo mezani kusubiri utekelezaji.

Na huu ndio utakuwa mtihani wa kwanza kwa UKAWA kwakuwa halmashauri ipo chini yao hvyo ubora na viwango vya barabara itakayojengwa ndio itaonesha umakini walionao ktk usimamizi wa miradi.
 
Tunaomba usalama barabarani waangalie usalama wa abiria katika njia "isiyo rasmi" ya Mbezi-Kinyerezi.

Kwanza nauli ya shilingi elfu moja kwa njia hii( ambayo kwa kukadiria haizidi kilometa kumi) ni kubwa sana,pili njia hii imeja magari mabovu(ukiacha Noah) ambayo hayana sifa ya kubeba abiria kwani mengine hata brake ni shida-lakini abiria mnalazimika kupanda kwa kuwa hakuna gari inaruhusiwa kuondoka kabla ya gari yenye zamu ya kupakia kujaa, tatu madereva wengi katika njia hii hawana leseni zinazowaruhusu kuendesha magari ya abiria.

Ni vyema njia hii ikapitishwa rasmi na mamlaka husika ili iweze kuwa na daladala zilizosajiliwa kubeba abiria kwani itasaidia kudhibiti nauli hizi holela, kudhibiti magari mabovu ambayo ni hatari kwa usalama wa raia na kuwadhibiti madereva wababaishaji wasio na sifa ya kuendesha magari ya abiria lakini pia hata mapato ya kodi kwa serikali.

NAWASILISHA JIPU KWA WATUMBUAJI.
 
Lijipu st.Joseph university in tanzania mbezi na tcu kuna harufu ya rushwa walikuja wakaguzi kutoka tcu wahindi walihangaika siku mbili au tatu kuficha maovu yao

Kukarabati mazingira ya maabara kuficha kompyuta zilizo chini ya kiwango

Kuandaa wanafunzi wa kujibu maswali ikiwa watauliza wakazi

Utaratibu mibovu

Lakini walipofika hawakukagua maabara wala mazingira ya chuo ila walijifungia ofiisini ikawa vikao tu

Na kula na kunywa huku wahindi wakiwasimamia show baada ya hapo wakaondoka lakini hali ni mbaya

Wizara husika inahitajika kufuatilia wasiende huku wametoa taarifa

Washtukize
Haha haaaaa......kumbe mkuu ulikuwepo siku hiyo, wahindi wanajua sana kuchezea akili za watanzania. Subiri siku wakija watu wa Uhamiaji......
 
Jipu lipo barabara ya Makumbusho kituoni. Ni mbovu sana na mvua ikinyesha magari na vyombo vyote vya usafiri vinatuama sana na kuharibikia hapo, pia gari inabidi ziwashushie abiria njiani ili wakwepe hiyo barabara....

Hili ni jipu kwa injinia wa wilaya ya kindoni anatakiwa awajibike hii barabara iweze kupitika kwani magari mengi yanashindwa kufika kituoni
Aisee hawa jamaaa kila siku wanaenda kazini asubuhi na kurudi jioni. Na mwisho wa mwezi pesa inaingia.... Hapa hata Magufuli naye ni jipu..... Nchi hii imelogwa.... Triumph kasema ukweli..
 
Kaka, barabara za kuingilia Makumbusho kaka.. Hasa kuanzia huku mwananyamala .. Kuna handaki pale karibu na shule ya Makumbusho ..

Ikulu ipo dsm.... Hili handaki lipo dsm.. Rais yupo dsm, mkuu wa wilaya yupo .. Mluu wa mkoa yupo .. Mkandarasi wa wilaya na mkoa yupo daaaah...

Kaka wafikishie taarifa
 
Kaka bara bara za kuingilia Makumbusho kaka.. Hasa kuanzia huku mwananyamala .. Kuna handaki pale karibu na shule ya Makumbusho .. Ikulu ipo dsm.... Hili handaki lipo dsm.. Rais yupo dsm, mkuu wa wilaya yupo .. Mluu wa mkoa yupo .. Mkandarasi wa wilaya na mkoa yupo daaaah... Kaka wafikishie taarifa
Mtakatifu unaongelea mwanyamala mbali hivyo ...hapa posta kwenye Petrol Station kama unaenda Haidery Plaza ni kichefuchefu
 
Mtakatifu unaongelea mwanyamala mbali hivyo ...hapa posta kwenye Petrol Station kama unaenda Haidery Plaza ni kichefuchefu
Kaka hapo nadhani pia na seawage system zimezidiwa uwezo... Ila Kuna mdau kaniambia kuwa pesa ya hizii bara bara imeshasainiwa manispaa na Bavicha kwa vile ndio waliopewa udiwani ndio watasimamia ujenzi wa hivi bara bata ... Ila kusema kweli mimi hawa bavicha/ukawa siwaamini bado japo mimi ni Ukawa damu toka kitambo .. Ila siku zote jiwe naliita jiwe ..
 
Mimi ni mteja wa siku nyingi wa Dstv Tanzania.

Gharama za kampuni hii kwa Tanzania binafsi naona ni kuwaibia watanzania kwa sababu tu ya monopoly ya kampuni hii kurusha ligi ya soka ya uingereza (England ) kwa ukanda wote wa Afrika chini ya jangwa la sahara.

Malipo ya mwezi ya vifurushi yaani packages ni kubwa mno nchini kwetu ukilinganisha na mataifa mengine ilipo hii kampuni.

Tunaomba wizara inayohusika na kampuni hii ya Dstv/ Multichoice Tanzania ifuatilie kwa karibu kuona kama gharama za vifurushi tunavyotozwa ni halali hasa kifurushi cha Capact Plus na Premium.
 
NAOMBA NIKUMBUSHE HILII MAANA AMH ALIKUWA WAZIRI KIPINDI HIKO

KUNA TAA ZA GARAMA KUBWA SANA SIJUI MNAZIONA NA ZINGINE MNAZIZADHARAU SABABU ZINGINE ZIEMEGONGWAA TAA ZINAINGINIA ZIKO PEMBENI YA BARA BARA HIZI ZA STRABAG KIMARA MPAKA KARIAKOO

NDUGU YETU MH DK HIVI HIZI TAA ZA NINI LEO MTU ANAOGOPA KUTEMBEA TOKA BARUTI MPAKA BUCHA AMA KIBO

MNAONAJE MKAFWATILIA NA KAMAWAMEWEKA TAA CHINI YA KIWANGO WAHUSIKA WATUMBULIWE BANA TUSHASHOKA SISI...TAA MIAKA MINGAPI AMZIWASHI WANAOGOPA BILLL YA UMEME AMA
 
Jipu langu mimi ni magari ya kuzolea taka kuharibika na kutengenezwa kwenye hizi barabara ambazo zimeligarimu taifa fedha nyingi za walipa kodi kwa kumwaga oil na diesel hovyo.

Hivi mamlaka husika kwa nini haziwakamati au kukamata wanaofanyia matengezo barabarani wakati hairuhusiwi?

Jamani, sheria ni traffic kukamata makosa ya madreva tu na sio pamoja na hayo yanayotengenezewa barabarani yaharibikapo?
 
Jipu la Miradi ya NGOs ni kubwa.

Wana miradi inayowaingizia pesa nyingi huku wakijifanya kutoa misaada ila kiukweli ni kukwepa kulipa kodi za serikali.

Mifano halisi na majumba ambayo watakuwa wameingiza vifaa bila kulipia kodi kwa kigezo cha kusaidia jamii ila kiukweli nyumba hizo wanazifanyia biashara na kutoza kodi kubwa sana, MASHIRIKA KAMA YA AFRICA MUSLIM AGENCY ni ya kufatiliwa sana
 
Jipu kubwa lipo TAZARA.

Kuna wakurugenzi 7 toka uongozi wa Waziri Nundu mpaka sasa wapo. Nundu aliwasimamisha kazi kupisha uchunguzi akaja Mwakyembe kuwarudisha kwa madai ya taratibu zilikiukwa, sasa wameongezeka na kufikia 19.

Mwanzo alikuwepo Ndg Ally Iddy - Head of Commercial, Mr Ayeshi-HHR, Ndg Kasumbai-Marketing Manager, Mrs Masilisi - Finance Manager, Ndg Kamugisha - Ag RGM, Ndg Mabala - Corperate Secretary, Ndg Longino - Head of Passenger, hawa pamoja na hujuma za wizi wa fedha bandalini pia wameshiriki kuuza karakana ya TAZARA likiwa na jengo lenye Standby generator yenye uwezo wa kusambaza umeme karibu wilaya yote ya Temeke. Teknolojia ya mchina!

Mbaya zaidi Serikali iliwaingiza wafanyakazi wa TAZARA keenye payroll ya azina, yaani serikali iliamua kulipa mishahara tangu mwaka jana july kipindi ambacho wafanyakazi wanadai mshahara wa January mpaka June, serikali iliagiza mamlaka ilipe mshahara wa January to June mwaka jana na yenyewe ianze kulipa toka july mpaka June mwaka huu.

Pesa imeliwa japo treni zinatembea za mizigo na abiria nadhani nyinyi baadhi ni mashahidi, hamsikii tena migomo TAZARA lkn toka mwaka jana hakuna hata senti iliyolipwa kwa wafanyakazi hela yote imeliwa na tumeimba sana na hela hii inavyoliwa kweupee.

Tuna uchungu na hela ya serikali, inalipa mishahara ila hii inayozalishwa inaliwa,, jipu lije litumbuliwe
 
Duh! Hii kweli special thread. Kuna jipu la kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa. Waliouziwa wote, walipe kadiri ya thamani ya mali na location.
 
Back
Top Bottom