Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Samahani wakuu tunapokuwa tunaweka kero zetu tujaribu kuzifafanua yaani namaani tuwetunabainisha sehemu (wilaya& mikoa) ya kero inakotokea
 
Kero ya malaya kutishia kunijazia nzi kama sitawapa hela wanayotaka (sisemi ni wapi). Srkl iwatambue kuwasajili na watoe risiti ili walipe kodi. Vinginevyo bk2 zinawatosha anayebisha makofi#×&%÷+@ kwani nzi kawaida yao hawakosekani
 

Tungefuata ushauri wako leo hii tungekaa upande wa Nani?
Leo hii KOREA KASKAZINI wako katika mazungumzo;
 
Ni matumaini yangu kuwa, wengi tu wazima wa afya njema kabisa katika siku hii ya leo ya DOMINIKA ya matawi ya 2018.
Lengo la ujumbe huu ni kutoa maoni binafsi juu ya ujumbe/waraka wa Maaskofu wetu.
Kwa maoni yangu mimi kuhusu nyaraka zinazotolewa na maaskofu wetu ni kwamba, haukuwa muda mwafaka sana kwa viongozi wetu wa Dini kuanza kuandika nyaraka zao hizo.
Kama kuna mtu ataniambia kwamba maaskofu wapo sahihi kuleta nyaraka zao hizi kwa sasa, lazima kwanza tukubaliane kuwa, wenzetu hawa kwa sasa ama wanatumika KISIASA au wana AGENDA iliyo nyuma ya pazia. Kwa nini? Kwa sababu: -
(1)Huko nyuma tumepita katika kipindi ambacho UFISADI, DHULUMA, UZEMBE makazini ulikuwa umekithiri kwa kiwango kikubwa sana, lakini hatukusikia hata Askofu mmoja akilalamikia hali hiyo. Iweje leo?
(2)Kwenye kashfa ya UFISADI wa ESCROW baadhi ya Maaskofu wetu walikuwemo na walipata mgao wa fedha za KIFISADI za ESCROW. Kwa nini hatukusikia hayo MABARAZA ya Maaskofu wakiandika nyaraka kulaani na kuwakemea maaskofu wenzao kwa kitendo hicho?
(3)Maaskofu wamekuwa wakikosa kabisa muda wa kuyaona mazuri mengi yaliyofanywa na serikali ya awamu hii ya tano, kinyume chake wamekuwa wakiyaona mapungufu tu. Kama kweli hawa ni maaskofu, ni aibu kubwa mno?

MAONI YANGU KWA MAASKOFU.
(1)Kabla ya kuandika nyaraka zao wajaribu kutafakari pia athari za nyaraka hizo kwa jamii na Taifa kwa ujumla.
(2)Wanapotaka kumhukumu mtu au serikali ni vema wakatumia kigezo cha MEMA yaliyofanywa na MABAYA yaliyofanywa na kuona yapi yamezidi.
(3)Siku nyingine ni vema kufanya kwanza MAZUNGUMZO ya faragha na serikali kabla ya kukimbilia kwenye nyaraka ambazo kwa Asilimia kubwa ZINAWAFITINISHA wananchi na serikali yao. Hiyo ni DHAMBI ya kufitinisha.
 
SALAMU ZA PASAKA 2018 KWA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
Kwa wakristo wote, Heri ya siku kuu ya pasaka.
Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais, Waziri mkuu, Mawaziri na viongozi wote wa ngazi mbalimbali katika Serikali ya awamu hii ya tano, nawapongeza sana kwa kazi njema na ngumu mnazozifanya kila siku kwa ajili ya Watanzania.
Nitumie fursa hii kuwapongezeni kipekee kwa mambo machache yafuatayo:
(1)Kuongeza uwajobikaji wenye tija katika utumishi wa umma.
(2)Kuongeza bajeti ya madawa ya binadamu zaidi ya mara7 ya bajeti ya madawa iliyopita.
(3)Kuzuia wizi wa rasilimali zetu ikiwemo madini, wanyamapori nk.
Hayo ni mfano tu, lakini yapo mengi mazuri yaliyo na yanayoendelea kufanywa na serikali hii.
Ndugu zangu viongizi, yanapofanyika mambo makubwa kama haya, lazima tutegemee kuibuka makundi kinzani ya kila sura na kila aina kutoka ndani na nje ya nchi . Kwani, kufanya haya ni kuwaumiza baadhi ya waliokuwa wanufaika wa rasilimali zetu hapo mwanzo.
Najua wengi watapiga kelele za kila aina na watafanya njama za kila aina lengo likiwa ni kufifisha jitihada hizi.
Rai yangu kwenu viongozi ni mshikamano wa kweli baina yenu ikiwa ni pamoja na sisi raia. KAMWE, KAMWE, KAMWE tusikubali hata kidogo kuyumbishwa au kurudishwa nyuma na mtu yeyote awaye yote.
TUSIGEUKE NYUMA, TUSIJE KUWA MAWE.

Mabadiliko ni Mapambano.
Ahsante, pasaka njema.
 
Kuna barabara ilikuwa inakera ya Mbagala Kuu Shuleni kuelekea Mbagala Zakiem kupitia Chemichemi sasa naona wanaikarabati. Safi sana serikali. Ila Sasa Sumatra na Traffic wapite huko maana magari ya ruti hiyo mengi hakidhi vigezo na bado nauli wanatu'chaji' mia tano badala ya mia nne.
 
Umeme!! Umeme!! Umeme!! Suala la umeme bado ni MSIBA MKUBWA WA KITAIFA.Kukatikakatika hovyo na wakati mwingine kuukosa kwa siku kadhaa si jambo la kushangaza.Uwekezaji mkubwa,makini na endelevu ufanyike kuondoa kero.Nimesema makini kwa kwa sababu WAHUNI walitumia na wanaweza kutumia kadhia hii kutuletea 'Escrow' nyingine kwa kisingizio cha dharura.
 
Big up Kinundu, ila na ajira huku Geita K ni kerooo
 
waziri wa ardhi ni Fisadi, achunguzwe vizuri kuhusiana ukaribu wake na GBP, hela ilikua inapelekwa kwenye mifuko kwa huyu mzee.
 
Kero yangu kubwa sana ni kwa afsa polisi wa tz hasa wale wanaoshirikiana na watu wa mitaana ili wawaibie haki ya msingi wananchi watiifu, wazalendo na wachapakazi.

Vitendo vya rushwa vimekithiri kwenye huu muhimiri watu wanaobainika na makosa na wengine wasio na makosa wamekuwa wakitengenezewa mazingira ya kutoa rushwa na pengine kuombwa rushwa na maafsa polisi hakika wengi wa afsa polisi ni wala rushwa.
 
Utasikia basi limeua wanne,
Piki piki imeua sita,
Au waliokufa muhimbili wamefika 100 kwa mwaka jana,
Meli ya Nungwi imeua 60,

Na hao ni wateja wa M-PESA, Tigo pesa na Airtel money,

Hela zao zinaendaga wapi?

Kuna utaratibu upi wa kuwapatia survivorship au next of kin wao?
 
Jipu:kero yangu ni kamata kamata ya viongozi wa upinzani,hii haileti maana kabisa naishauri serikali na pamoja na vyombo husika hii kamata kamata haiwezi kutafutwa njia nyingine ya kushughulika na viongozi hawa wa upinzani mpaka wawekwe ndani? huo ni unyasasaji kwani hawa ni wawakilishi wa wananchi ambao wana kazi walitumwa na wananchi,wanapowaweka ndani ina maana wanashindwa kutekeleza majukumu waliokabidhiwa na wananchi,ushauri wangu watafute njia mbadala ya kuweza kukaa meza moja na iwe ya amani kujadili nini kifanyike ili kuepusha usumbufu kwa viongozi hawa.
 
Wew sio mzalendo unapinga maagizo toka juu
 
Kelo yangu ni upotevu wa 1.5 t raisi mbna utoi tamko lolote lile
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…