LebronWade
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 1,615
- 1,508
1.hataki mijadala.. Mijadala ipi mbona TAASISI nyingi tu zinaendelea na vikao kuhusu masuala yao ya kiutendaji. Mijadala Gani unataka
2.kaiba CHETI, ukiambiwa ulete ushahid unasema Gwajima KASEMA kwanini rais a deal na mambo ya mitandaoni tena mepesi kama haya. Hivi kweli upo serious una amini kaiba CHETI.
3.kuvunjia watu nyumba Unaamini anafanya yeye kabla ya mamlaka husika kufanya uchunguzi na kugundua madhara yatakayokuja.. Embu assume we ni rais na una roho mbaya je kuvunja nyumba za watu unapata faida Gani. Rais ananufaika vipi hapo.. Jamani amkeni ndugu ZANGU serikali ina vyombo vingi wakati mwingine kutimiza majukumu Yake unamuona rais anamkosea mmiliki wa nyumba inayoweza kuingiza maji na kuua watu.
4.fedha zimetumika kufanya jambo Zuri la kuchangia madawati bado tu na Hilo huhitaji kuskia ndugu
5.hivi magufuli kuwaelekeza mahakama kwamba washughulikie kesi haraka nako amekosea? Ila ikumbukwe yeye ni mkuu wa nchi anasimama juu ya mihimili mingine Ila kizuri Anatoa maelekezo ambayo kikatiba yuko sawa
6.ni kosa rais kutoa mwelekeo wa serikali Yake Kanisani.. Na wakati kanisa linakuwa linajua kuwa kutakuwa na ugeni wa mkuu wa nchi. Kosa hapo silioni
7.kumpandisha mtu cheo Utaratib wa nini wakati katiba Inasema kabisa yeye ndio amiri jeshi mkuu.. Mamlaka hiyo yapo chini Yake..
8.hataki kusoma hotuba. Kavunja sheria Kivipi na hayo unaposema madudu HAUPO sawa. Rais ni amiri jeshi HUTAKI aongoze watu Sasa nini maana ya kuwa rais. Mwelekeo wa serikali Yake atautoaje Bila kuongeza maneno anayoyamini
Mimi nasema kwamba magufuli anafanya vizuri Sana Ukitulia na ukijua kuwa tuluchelewa kupiga hatua, hutampinga magufuli.. Pamoja na mapungufu aliyonayo madogo bado anatufaa Sana
Wewe bwana JOHN utakua m.bwa kasoro mkia....huu uzi ufutwe maana alieuleta ana majibu ya ki.maandazi sana....bashite wewe.