Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Point si nani aende mahakamani, point ni, Kikwete ana cha kujibu au ana kinga kamaulivyosema?

Kama ana cha kujibu, Magufuli kumuachia kunaonyesha Magufuli hayuko serious katikahi vita, anaifanya kisiasa kwa kuchagua nani wa kumshtaki na nani wa kumuacha.

Anashtaki dagaa, wakati mapapa anayaacha.

Lissu kashapigwa risasi ukitaka aende kumshtaki Kikwete sasa hivi utakuwa unamuonea tu.
Maybe yes maybe no, kama Magufuli wanafanya hii vita ya kisiasa. Lakini navyojuwa mimi PCCB wako busy kukoji wahusika ambao wengine wameshaaza kutimka.
 
Maybe yes maybe no, kama Magufuli wanafanya hii vita ya kisiasa. Lakini navyojuwa mimi PCCB wako busy kukoji wahusika ambao wengine wameshaaza kutimka.
PCCB haiwezi kumgusa Kikwete, kwa sababu anayemteua na kutengua bosi wa PCCB, Magufuli, kashasema hawa wastaafu wasiguswe.

Hapo ndipo utakapoona hii vita ni ya kisiasa na vyombo vya dola vishawekewa mipaka.
 
PCCB haiwezi kumgusa Kikwete, kwa sababu anayemteua na kutengua bosi wa PCCB, Magufuli, kashasema hawa wastaafu wasiguswe.

Hapo ndipo utakapoona hii vita ni ya kisiasa na vyombo vya dola vishawekewa mipaka.
Ndio muda wa wanasheria kudai mahakama ifafanue kama kikwete ana lakujibu au la. Hiyo ndio kazi ya mahakama, kama kuna kitu kinatatiza tena ni kitu cha kisheria, mahakama iko na itatoa ufafanuzi. Tatizo mtu kama Lissu akifuatilia kitu hiki na yeye anawekwe katika kundi la watu wanaochuklia hili swala kisiasa maana amevaa anakofia ya kisiasa. Ilipaswa wanasheria ambao hawajihusishi na siasa ndio fuatilie hili swala.
 
Ndio muda wa wanasheria kudai mahakama ifafanue kama kikwete ana lakujibu au la. Hiyo ndio kazi ya mahakama, kama kuna kitu kinatatiza tena ni kitu cha kisheria, mahakama iko na itatoa ufafanuzi. Tatizo mtu kama Lissu akifuatilia kitu hiki na yeye anawekwe katika kundi la watu wanaochuklia hili swala kisiasa maana amevaa anakofia ya kisiasa. Ilipaswa wanasheria ambao hawajihusishi na siasa ndio fuatilie hili swala.
Hakuna cha kufafanua kwamba Kikwete ana cha kujibu.

1. Kasaini mikataba yenye utata.
2. Kasaini wakati hana kinga ya urais.
3. Ana cha kujibu kuhusu mikataba hiyo

Kitu ambacho mahakama inatakiwa kuamua ni kama ana hatia ama la.

Sasa kwa nini Kiwete kaachwa katikahao wanaoandamwa?
 
Hakuna cha kufafanua kwamba Kikwete ana cha kujibu.

1. Kasaini mikataba yenye utata.
2. Kasaini wakati hana kinga ya urais.
3. Ana cha kujibu kuhusu mikataba hiyo

Kitu ambacho mahakama inatakiwa kuamua ni kama ana hatia ama la.

Sasa kwa nini Kkwete kaachwa katikahao wanaoandamwa?
Naona umemkomalia huyo jamaa, lakini kwa hulka hizi ndio watu hawata weza kumpata maana kama mnaona Magufuli ana upendeleo basi kuna njia ya mahakama, na kama mahakama inaoneka haitowi haki, then upinzani inabidi uongeze bidii kukamata dola ili waakamate wote. Japo wakiwakamata itawaleta kwenye mahakama hizi hizi ambazo watu hawana imani nazo.
 
Naona umemkomalia huyo jamaa, lakini kwa hulka hizi ndio watu hawata weza kumpata maana kama mnaona Magufuli ana upendeleo basi kuna njia ya mahakama, na kama mahakama inaoneka haitowi haki, then upinzani inabidi uongeze bidii kukamata dola ili waakamate wote. Japo wakiwakamata itawaleta kwenye mahakama hizi hizi ambazo watu hawana imani nazo.
Mimi objective yangu hapa si kumkamata Kikwete.

Objective yangu ni kuonyesha kwamba Magufuli hayuko serious na hii vita ya mafisadi, anaitumia kisiasa.
 
Mimi objective yangu hapa si kumkamata Kikwete.

Objective yangu ni kuonyesha kwamba Magufuli hayuko serious na hii vita ya mafisadi, anaitumia kisiasa.

Cha kujifunza ni kuwa wanasiasa watabaki kuwa wanasiasa. Kokote kule duniani hautakuja kuona mwanasiasa anacha kundi lake na kupenda kundi la jirani. Hii inaenda hata kwa wanasiasa wa upinzani hapa Tanzania, Mungu atuweke hai na wao siku wachukuwa dola uone kama hawata lindana.
 
Binafsi napenda kutumia fursa hii adhimu kuendelea kumshukuru na kumpongeza mheshimiwa Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Serikali yake yote kwa kazi njema wanazozifanya kwa ajili ya watanzania.
Zaidi sana natoa pongezi zangu kwao kutokana na UZALENDO usio na mashaka walio nao na unaoonekana kwa wazi kabisa.
Hapa katikati kumekuwa na shutma nyingi sana dhidi ya hawa viongozi wetu. Lakini kwa mtazamo wangu nimeona shutuma hizo hazina ukweli ndani yake.
Mimi naomba tumwache Rais afanye kazi yake ya kuwaletea watanzania maendeleo.
Kwa hakika, kazi hii ya kutetea rasilimali za nchi inayofanywa sasa kama ingefanywa kikamilifu tangu awamu zote zilizopita nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo.
Sina maana kwamba awamu zilizopita hazikufanya kitu, la hasha, kila awamu imefanya mengi tu mazuri.
Nihitimishe kwa kuwaomba watanzania tumuunge mkono Mh. Rais wetu, kwani hizi rasilimali anazopigania si kwa ajili yake na familia yake bali ni kwa ajili ya watanzania wote. Amina.

Wanauzalendo gani zaidi ya matumbo Yao raisi mroho anajirimbikizia mali
 
Kwangu sikujua kuwa kuna watanzania wabinafsi wasiopenda wengine wasionakipato wapate kidogo tunachopata kama nchi. Watu wachoyo wapenda rushwa na wabinafsi. wanaopinga juhudi za raisi kusaidia tabaka la walalahoi.

Mungu saidia rais wetu Magufuli.

Mbona mwenyewe Mla rushwa na rushwa anaiihusudu
 
Binafsi napenda kutumia fursa hii adhimu kuendelea kumshukuru na kumpongeza mheshimiwa Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Serikali yake yote kwa kazi njema wanazozifanya kwa ajili ya watanzania.
Zaidi sana natoa pongezi zangu kwao kutokana na UZALENDO usio na mashaka walio nao na unaoonekana kwa wazi kabisa.
Hapa katikati kumekuwa na shutma nyingi sana dhidi ya hawa viongozi wetu. Lakini kwa mtazamo wangu nimeona shutuma hizo hazina ukweli ndani yake.
Mimi naomba tumwache Rais afanye kazi yake ya kuwaletea watanzania maendeleo.
Kwa hakika, kazi hii ya kutetea rasilimali za nchi inayofanywa sasa kama ingefanywa kikamilifu tangu awamu zote zilizopita nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo.
Sina maana kwamba awamu zilizopita hazikufanya kitu, la hasha, kila awamu imefanya mengi tu mazuri.
Nihitimishe kwa kuwaomba watanzania tumuunge mkono Mh. Rais wetu, kwani hizi rasilimali anazopigania si kwa ajili yake na familia yake bali ni kwa ajili ya watanzania wote. Amina.
Swali...? Wakati wa awmu zilizopita ulikuwa hujazaliwa...?kama ulikuwepo bas ww utakuwa ni mnafiki mkubwa kwa sababu muda wote ulichimbia likichwa lako mchangani halaf leo hii unajifanya kushauri.....!
 
Kuna majipu bado yapo mengi mfano:

Utafiti mdogo niliofanya, umeonesha kuna shule za msingi zinaendesha tuisheni, mfano.

Shule ya msingi Tumaini na Kimanga zote shule hizi zimeunganishwa pamoja. Walimu wao wamekuwa wakiendesha tuisheni, pembeni kidogo ya shule hizo.

Walimu hao huendesha tuisheni, katika majengo ya shule ya sekondari ya wazazi iliyoko maeneo ya sokoni huko huko tabata kimanga

Chanzo mimi mwenyewe nimefanya utafiti.
Hili sio jipu Bali wanawasaidia watoto,hats ss tumesoma tuition ndio maana tumefika hapa. Bila masomo ya muda WA Ziada Ni kaz bureee
 
Wadau
Mnatambua kuwa Serikali ya awamu ya 5 imetangaza kuingia katika vita vya kiuchumi. Vita hii ni ngumu sana inayohitaji watu kujitolea kwa hali na mali bila kujali maslahi binafsi.

Matokeo ya vita hii ni kuwawezesha Watanzania walio wengi kufaidika na rasilimali zao vizuri badala ya rasilimali hizo kuendelea kuwanufaisha wachache.

Naamini wapo watu wachache watakaojaribu kuhujumu jitihada za Serikali yetu.Watu hao ni lazima tuwabaini mapema na kutoka taarifa kwa mamlaka husika.

Sasa ni vema kwa hapa JF tukaanzisha utaratibu maalumu wa kuwadhibiti kwa kuwa na orodha maalumu ya watu hao yaani black book.

Pia napendekeza awepo mtu maalumu tena mwenye uzalendo usio na shaka akabidhiwe na atunze orodha hiyo. Black book hiyo iwe na taarifa zote muhimu.

Tushirikiane na Serikali yetu kuwadhibiti na kuwabaini watu hao ili tuweze kupata maendeleo.
Tupeane mawazo
 
Huo utakuwa ni UNAFIKI.

Ni unafiki kwasababu hata huyo anayejifanya anapinga ufisadi na kupambana na Wahujumu uchumi hata yeye alishakuwa fisadi wa kuuza nyumba za serikali na kuhonga hovyo hovyo lakini leo anahukumu kana kwamba yeye ni malaika.

Mbaya zaidi anawahukumu wale wanyonge tu na kuwaacha wale Mapapa wa Ufisadi na kusema waachwe wapumzike.

Hiyo Double standard ndio UNAFIKI wenyewe.

 
Wasalaam wakuu,

Naomba kuwasilisha kero yangu kwenu huku nikiwa nina imani kabisa itawafikia watu sahihi na kuifanyia kazi.

Natambua wazi juhudi zinazofanywa na mheshimiwa raisi katika kupambana na kutatua kero mbali mbali zinazotuhusu sisi wananchi lakini ni wazi kabisa watendaji wake wanamuangusha na hawafanyi vile ambavyo ye anahitaji iwe. WATEDAJI HASWA VYOMBO VYA USALAMA ENEO HILI NILILOPO HAWANA UZALENDO WAMEWEKA MASLAI YAO MBELE NA NI WAPENDA RUSHWA.

Nipo mkoa wa mara katika eneo la nyamongo ndani kabisa ya mgodi unaomilikiwa na kampuni ya ACACIA, sehemu ambayo kuna wazungu wanafanya kazi bila hata ya kuwa na vibali, ni wazi kabisa kuna rushwa kubwa inaendelea kati vyombo vyetu vya usalama haswa uhamiaji/Polisi na uongozi wa huu mgodi kwa sababu mara kwa mara watu wa uhamiaji wamekuwa wakiingia mgodini wakifanya ukaguzi kwa wageni hawa lakini wanaishia kupewa rushwa na kuondoka zao na si mara moja, imefikia hatua wazungu hawa eti wanamiliki vitambulisho vya utaifa! kuna wakati tulienda ofisi za usalama wa taifa wilaya pamoja na nyaraka zinazothibitisha wazungu hao kufanya kazi bila vibali lakini matokeo yake mpaka sasa imepita miezi mitatu na hakuna kilichofanyaika na wageni hawa wanaendelea kutapa tena wakiikejeli serikali ya mheshimiwa raisi kwa jinsi inavyowabana ACACIA. hii na aibu sana kwa nchi na inakatisha tamaa.

Kuna OCD pia wa eneo hili (OCD NYAMWAGA) pia anatia aibu sana kwa serikali na kwa jeshi la polisi, kila siku iendayo kwa Mungu huingia mgodini na kuzunguka zunguka kwenye maofisi ya hao wazungu kwa muda usiopungua masaa saba mpaka tisa na wakati mwingine amekuwa akishirikishwa inapotokea migomo kutishia wafanyakazi, swali je hiyo ndio kazi yake kama OCD!? ni kitu gani humleta kila siku humo mgodini!!? .... polisi hawana sauti kabisa eneo hili, nashangaa eti polisi wanasachiwa na walinzi wa mgodi kwenye mageti!!! inawezekana vipi polisi mwenye dhamana na mafunzo anasachiwa na raia ambae hana dhamana!

Yapo mengi sana lakini hili nimeona liwe la kwanza maana linashusha heshima yetu kama nchi na linaondoa thamani yetu watanzania.

Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu isue nyingine ni kero ya maji maeneo ya mbezi luis wanazingua tu
 
mchezo ulioanzishwa na baadhi ya wakuu wa wilaya wa kutumia wanafunzi kuwapigia kura walimu wenye tabia ya kufanya mapenzi na wanafunzi ukome maana wanafunzi wanaweza kumpigia kura mwalimu anayewajibika na kuwachapa viboko huku mwalimu mzembe akionekana msafi.

Lakini pia mwalimu mwenzie au mtu mwingine mtaani mwenye chuki naye anaweza kuahamasisha upigaji wa kura hizo. Tatizo jingine wale walimu wanaopigiwa kura nyingi wanaambiwa wahamie shule nyingine, swali ni je hiyo shule anakohamia ndo wanahitaji walimu wenye tabia mbaya?

Kama ni kuwabaini walimu wenye tabia chafu serikali inavyo vyombo vingi kwa nini isitumike njia nyingine isiyoacha shaka ili kuwabaini walimu wenye tabia mbovu badala ya kutumia njia yenye ukakasi? Wanasiasa acheni tabia hizo za kutafuta kiki huku mukiacha jamii kwenye mitafaruku isiyokuwa na tija.
 
Mheshimiwa Waziri wa Elimu, naomba kupata ukweli juu ya mambo yafuatayo:-
(1)Je, VYETI vya kumaliza Elimu ya msingi bado vinatolewa kwa wahitimu au vilifutwa?
(2)kama vilifutwa, kwa nini bado vinahitajika hasa watoto wetu wanapotaka kujiunga na kozi mbalimbali?
(3)Kama havijafutwa, kwa nini havitolewi kwa takribani miaka 6 mfululizo mpaka sasa?
 
Nitumie fursa hii kuipongeza nchi yangu Tanzania kwa kitendo cha kishujaa cha kuipinga USA kuhusu Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.
Kitendo kilichonikasirisha mimi zaidi ni pale USA wanapotufanya sisi watoto wadogo kwa sababu tu ya vimisaada vyake.
NI HERI KULA PUMBA KAMA WANYAMA PAMOJA NA UHURU KAMILI KULIKO KULA CHAKULA KIZURI BILA UHURU KAMILI.

Mimi ningekuwa na mamlaka ya juu katika nchi hii, ningeanzisha urafiki wa chanda na pete na KOREA KASKAZINI ambayo ndiyo kiboko ya US.
Ningesema "Karibu NORTH KOREA, kwa heri USA"
 
Sijui nisemeeee?au nimwache huyu hizi hela za Magufuli anazokula pasipo uoga.
 
Back
Top Bottom