Total yatoa fursa vituo vya COCO na CODO kuzigeuza DODO! Kuwa umiliki kituo cha mafuta cha total

Total yatoa fursa vituo vya COCO na CODO kuzigeuza DODO! Kuwa umiliki kituo cha mafuta cha total

Ila mkuu naona ni fursa sema wengi wetu tutakuwa hatuna elimu ya kutosha kwenye uendeshaji wa hizi biashara
 
Pascal acha upotoshaji. Naona kama kawaida yako umeamua kuja kufanya damage control baada ya kuona uzi wa mtu aliyeukiza kunani Total baada ya Tangazo Lao kuuza depot zao na Mali zao.

Labda nikuulize tu Pascal kama biashara na uwekezaji wa Total hapa Tanzania unaenda vizuri na kuwalipa kwa nini wanauza Mali zao depot zao????

Pili umeelezea mradi wa Bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanzania kama moja ya miradi yao wanaotaka kujikita nayo. Sasa nikuulize Je imekuwaje huo mradi Kukwama hadi saivi??? Maana hadi saivi hatuoni huo mradi ukiendelea????

Hoja yako ingekuwa na nguvu Kama tungeona mradi wa bomba la mafuta la Tanga ukiwa unafanya kazi sasa kama kote hatuoni lolote je unawezaje kuja na hoja mfu namna hii????

Alafu kwenye hili kumbuka pia kuna vituo vingi vya mafuta hapa Tanzania sasaivi vinaendeshwa kwa ukata na wafanyakazi wao hawalipwi mshahara kwa wakati. Je kwenye Hilo unaelezeaje juu ya sekta ya biashara ya mafuta Tanzania??? Je ipo stable????
 
Mkuu Retired, mimi nipo sana tuu, ila kwa sasa kufuatia mimi kuwa ni kada, hoja zangu nimezielekeza zaidi kwa maslahi ya taifa.
P
Hakuna cha maslahi ya taifa, sema unatafuta kula yako, tena kula ya ulaini! Maana sasa kula yako inatokana na hard earned money, siyo kama kwenye siasa ambapo ni kama kokota! Unadhani do you make any impact for the benefit of masses kwa kuandika humu?
 
Wanabodi,

Japo hili ni Jukwaa la Siasa, na hii ni story ya fursa za Kiuchumi, issues zozote za utilities, umeme, maji na mafuta, ni siasa, hivyo ikitokea sintofahamu yoyote kwenye issues za mafuta ya fuel, nchi inatikisika!.

Kumetokea Tangazo fulani la Total kwenye gazeti, kuna jamaa ka panic, anataka kuwapanikisha Watanzania!.
What happened? Total yafungasha virago vyake Tanzania(?)

Kabla sijakisema nilicho dhamiria, naomba kwanza nitoe elimu kidogo kuhusu biashara ya mafuta na gesi Tanzanian.

Biashara ya mafuta na gesi Tanzanian imegawanyika katika makundi mawili,
1. Upstream- Watafutaji mafuta na gesi, wachimbaji mafuta na gesi, hawa wanadhinitiwa na PURA.
2. Downstream- hawa ni wasambazaji wa mafuta na gesi, yaani makampuni ya mafuta. Hawa wanadhibitiwa na EWURA.

Kwenye usambazaji wa mafuta, nako kuna makundi mawili,

Waagizaji wa mafuta ya jumla, bulk procurement na wasambazaji wa mafuta ambao wanachukua kutoka kwa bulk na kuuza kwenye vituo vya mafuta.

Ni makampuni machache ambayo wanafanya biashara ya mafuta kuanzia upstream, downstream na retail supply, kwa Tanzania kampuni ya kwanza ilikuwa Shell, ya Waingereza, pili Agip ya Wataliano na tatu ilikuwa Total ya Wafaransa.

Shell iliuzwa sasa ndio Puma, Agip ikauzwa na kuwa Gapco, hivyo kwa sasa, baada ya Total kuinunua Gapco, Tanzania, kampuni kubwa ya mafuta, kwa upande wa mtandao wa vituo vya mafuta, ni Total.

Kwa msio jua, Total ndio kampuni inayoongoza kwa uwekezaji Tanzania, yaani investment, mradi wa bomba la gesi la Hoima Uganda hadi Chongoleani ndio the biggest investment in the history of TIC, hata Dangote atasubiri!.

Tukija kwenye biashara ya reja reja ya mafuta, Total ndio inayoongoza kwa wingi wa vituo vingi.

Sasa naomba kuendesha shule fupi ya maneno matatu haya, COCO, CODO na DODO kuhusu vituo vya mafuta vya Total.

Kuna aina tatu ya vituo vya mafuta vya Total.
COCO ni Company Owned, Company Operated, hivi ni vituo vinavyomilikiwa na kampuni ya Total, 100% kwa 100% na kampuni ya Total inaviendesha, vikiwemo vituo vyake vyenyewe na vituo vyote vilivyokuwa Gapco.

CODO ni Company Owned, Dealer Operated, ni vituo ambayo Total inavimiliki lakini vinaendeshwa na watu wengine, dealers.

DODO ni Dealer Owned, Dealer Operated, hii ni mtu au kampuni binafsi inamiliki kituo na kukiendesha, ila Total wanakupa mkataba wa franchise, kwa kukijenga kwa viwango vya Total na kuuza bidhaa za Total.

Sasa Total Tanzania imemwaga fursa kibao kwa Watanzania kumiliki vituo kwa huo mtindo wa DODO ambapo Total inauza vituo vyake vyote vya COCO na CODO kuwa DODO!.

Changamkia Fursa.

Naomba kuchukua fursa hii kuwaonyesha uzinduzi wa kituo cha mafuta cha Dodo uliofanyika jana pale Goba Mshigeni.


Kwa faida ya wasiojua mambo ya Total karibuni mitaa hii
Kampuni ya Total Yainunua Gapco na Kuwa The Biggest Oil Company in Tanzania, Kenya & Uganda.

Maendeleo ya Kweli Yataletwa na Watanzania: Kampuni ya Mafuta ya Total Yazindua Kituo cha Kwanza cha Watanzania, Total Tegeta Service Station

Jee Kuna Ukweli Kuwa in Tanzania, Mafuta ya Vituo vya Total, " They are The Best?. If Yes, How Wakati Tunanunua Bulk?.

Leo ni Valentine: Jaza mafuta kituo cha Total, upate Zawadi ya punguzo la bei ya mafuta.

From Hyatt Regency, The Kilimanjaro: the 2nd Tanzania Oil & Gas Congress. Wazungu Wengi Kuliko Wenyeji!

Total Tanzania yazindua shindano la 'startupper of the year by total'

Total Tanzania Yafanya Makubwa, Kuigeuza Tanzania Kama Ulaya!, Yaanzia Temeke.

Vita dhidi maambukizi ya corona Tanzania, kampuni ya Total Tanzania mfano wa kuigwa!. Ukifika lazima unawe, upimwe na mashine ndipo uruhusiwe kuingia!

Paskali



Thanks Pascal,, Nmekuelewa vyema!!
 
Idea ya kuuza hizo kampuni ndogo ndogo ni nzuri kwa sababu itasaidia kuongeza mzunguko wa pesa kwa jamii, sijui kama bei ya hizo kampuni itakuwa nzuri kwa watanzania ili wengi waweze kujitokeza kuzinunua.

Lakini pia serikali kujiingiza kwenye biashara ya mafuta nayo inaweza kupunguza idadi ya wataojitokeza kununua hizo kampuni kwa kuhofia ushindani na serikali kwenye biashara ya mafuta.

Serikali ikishakuwa mshindani lazima pawe na kushindwa tu! Ngumu kuweza kushindana na serikali!

Case study " FastJet Vs Air Tanzania"
 
safi sana mliokuwa mnajifanya marketing hr procurement mafundi pump katafuteni kazi zingine, mie nikinunua kituo nauza mimi na mke wangu hakuna cha marketing officer
 
Maamuzi Total nyuma ya pazia ni mazingira magumu ya biashara tz, usumbufu mifumo ya kodi, serikali imeanza kujenga na kuendesha vituo vyake rejea vituo Dodoma,Dar.... Tozo nyingi toka maamlaka tofauti, Ewura, Nemc, jiji,manispaa na halmashauri. Lissu kwa siku chache kaweza kusemea taifa kuliko wabunge mamia wa ccm wapiga makofi.
 
Swali langu ni je? Itabaki nembo ya TOTAL vile vile? Na je oil zao zitaendelea kupatikana kwa bei ile ile au ndo zitapotea kama zilivyopoteaga oil za BP
No, brand ya Total itaendelea, BP, waliuza jumla, kama Total iliponunua GAPCO, hii wanachofanya ni vituo wa COCO na CODO, kuwa DODO.
P
 
Si kweli pasco labda uendelee na shule.
Lile tangazo ni la kuuza na si ubia, pia linasema anauza had depot hapo unasemaje ni CoCo au DoDo wakati wanauza?

Nilitegemea useme inauzwa kama shell ili watz tuchangamkie fursa kumbe wewe unaleta propaganda apply to good name, oooh poor u!!!!
 
Mbona advertisement yao inasema tofauti kabisa. Total wanauza mali zao zote kuanzia depots mpaka service stations. Je wanafanya hvyo kwa Nchi zote walizo na uwekezaji au ni Tanzania tu?

I know about Franchising, ila hili la Total sio franchising. Let's wait and see. Ila navyoona Total anafunga downstream business yake kwa Tanzania
 
Sioni fursa yoyote hapo zaidi ya anguko lakibiashara kwa hao watakaokuja kumiliki hivyo vituo.Kumbuka mabeberu sio wajinga kivile.Hizo nyingine ulizotuletea ni terminology tu ila ujatuambia sababu hasa zawao kufikia maamuzi hayo ili kuondoa sintofahamu iliyojitokeza.Ila ngoja tusubiri muda utatupa majibu sahihi.
 
No, brand ya Total itaendelea, BP, waliuza jumla, kama Total iliponunua GAPCO, hii wanachofanya ni vituo wa COCO na CODO, kuwa DODO.
P
Total is selling her properties, from plots, depots to Service stations. CODO ni leasing your properties to another person/company kwa muda, so hili kwa Total halipo, and you know that Paschal.

By selling her properties that means she owns non, so COCO haitahusika hapa.

DODO kidogo inaweza kuhusika ila nayo ni mpaka tupate agreements behind the selling process. Yawezekana ikawa total ownership kiasi kwamba mpaka brand name Dealer aliyenunua akaamua kubadilisha akaweka lake
 
Back
Top Bottom