Tottenham Hotspurs Thread

umenielewa sasa?
 
Nadhani umeanza kuangalia game za spurs hii hatua ya 16 bora Ila hujajua ubora wa spurs we subiri mkuu hadi final tupo Ila hatuvumi.
natazama UCL tangu 1994.Nawatazama spurs miaka nenda rudi.Nawatazama Juve tangu 96 wakimpiga Ajax mikwaju ya penati.
Niliwaambieni saikolojia ya wataliano.Mlipomtoa kamasi uwanjani kwake ndio mlipojichimbia kaburi,kaja wembley kufa kupona,ndio walivyo wataliano,hesabu zao ni over two legs.panapohitajika mzuka wao hupandisha hapo hapo,hata mngeshangilia na honi za treni,haiwasumbui wataliano wakiwa wamelazimika kutafuta matokeo moto wao mkubwa kama ulivyoona,leo Totenham asiyefungika Wembley,kafungwa hapo hapo.
 
Sasa Ndiyo Mjue Kuwa Munapocheza Mechi Kubwa Kama Hizi muwe Munamchukua John Moss Akakae Referee!
Halafu muwe munafanyia Mazoezi Zile Diving Zenu.
Na Harry Kane aongeze Mazoezi Zaidi ya Kuotea...
Halafu Mushauriane Mufungua Pale London Kwenye Oxford University mufungue SCHOOL OF DIVING ili kina Harry Kane, Eric Lamela na Delle Ali Wakaongeze Doctor Of Philosophy in Diving.

Kwa Taarifa Yenu Maisha Kombe lenu Litakuwa ni Top Four, lakini Champion League Katu hamtovuuka Hata Robo Fainali.
 
Subiri mkuu mpira uwanjani na sioni mnapoenda kuwabahatisha hawa watoto Wa Portugal goal 5 usidhani ndio mmemaliza. Fc porto Si wale Wa kipindi lile hadi mkawafumua kiasi kile.

Katika robo ya UCL nyingi ndio mtaongoza kwa kutoka kwa aibu subiri mda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…