Tozo za miamala ni njia ya kufidia pesa zinazokujenga miradi kama Burigi National Park na Ikulu Dodoma?

Tozo za miamala ni njia ya kufidia pesa zinazokujenga miradi kama Burigi National Park na Ikulu Dodoma?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ingekuwa sawa kama ongezeko la tozo za miamala na mafuta kwa wanyonge lingelenga kwenda kununua meli kubwa za uvuvi ili tuvue kisasa kwenye kina kirefu, kununua matrekta kwa wakulima ili walime mashamba makubwa, kuchimba madini ya kimkakati kama chuma au kusambaza nishati ya gesi nchini ili watu wasikate miti.

Unapojenga zahanati kila kijiji utahitaji pia kupeleka watumishi, vifaa tiba, madawa na kujenga nyumba za watumishi huko vijijini. Tatizo leo sio kuwa na zahanati kila kijiji, bali ni kuziboresha hizi zilizopo ili zitoe huduma zilizokusudiwa (quality badala ya quantity).

Pesa za kujenga vituo vya afya na shule zilikuwepo ila vipaumbele vya viongozi ilizielekeza kwenye miradi ambayo haigusi wananchi moja kwa moja kama vile kujenga Ikulu kubwa ya kufa mtu, kujenga ukuta melelani, kujenga national park kule Burigi, safari za viongozi ndani na nje ya nchi, kujenga majengo ya wizara na ofisi mpya wakati majengo hayo yapo. Kuhamia Dodoma ni sawa na ni jambo jema, lakini kutumia fedha nyingi kuhamia dodoma wakati watu hawana maji, shule, barabara, umeme, majosho, mbolea, na zahanati zenye watumishi, vifaa tiba na dawa ni kejeli kubwa kwa wananchi ambao wanatakiwa kuongezewa tozo za miamala na mafuta eti kujijengea vitu hivyo.

Binafsi sioni uhusiano uliopo kati ya kuhamia dodoma na upatikanaji wa maji, zahanati, madarasa, umeme, nyumba za watumishi, vifaa tiba na watumishi kwa wananchi wote nchini na hasa vijijini.

Mheshimiwa Mwigulu anataka kutuaminisha kuwa pesa ya kodi, tozo na mauzo ya mazao na madini kama korosho, kahawa, pamba, dhahabu, bandari na uchukuzi, mikopo, misaada na huduma mbalimbali tunazotoa kama nchi sio za kujengea madarasa na zahanati hadi tukamue watu kwenye miamala, mafuta na umeme.

Tusidanganyane jamani, tukutane 2025
 
Ingekuwa sawa kama ongezeko la tozo za miamala na mafuta kwa wanyonge lingelenga kwenda kununua meli kubwa za uvuvi ili tuvue kisasa kwenye kina kirefu, kununua matrekta kwa wakulima ili walime mashamba makubwa, kuchimba madini ya kimkakati kama chuma au kusambaza nishati ya gesi nchini ili watu wasikate miti.

Unapojenga zahanati kila kijiji utahitaji pia kupeleka watumishi, vifaa tiba, madawa na kujenga nyumba za watumishi huko vijijini. Tatizo leo sio kuwa na zahanati kila kijiji, bali ni kuziboresha hizi zilizopo ili zitoe huduma zilizokusudiwa (quality badala ya quantity).

Pesa za kujenga vituo vya afya na shule zilikuwepo ila vipaumbele vya viongozi ilizielekeza kwenye miradi ambayo haigusi wananchi moja kwa moja kama vile kujenga Ikulu kubwa ya kufa mtu, kujenga ukuta melelani, kujenga national park kule Burigi, safari za viongozi ndani na nje ya nchi, kujenga majengo ya wizara na ofisi mpya wakati majengo hayo yapo. Kuhamia Dodoma ni sawa na ni jambo jema, lakini kutumia fedha nyingi kuhamia dodoma wakati watu hawana maji, shule, barabara, umeme, majosho, mbolea, na zahanati zenye watumishi, vifaa tiba na dawa ni kejeli kubwa kwa wananchi ambao wanatakiwa kuongezewa tozo za miamala na mafuta eti kujijengea vitu hivyo.

Binafsi sioni uhusiano uliopo kati ya kuhamia dodoma na upatikanaji wa maji, zahanati, madarasa, umeme, nyumba za watumishi, vifaa tiba na watumishi kwa wananchi wote nchini na hasa vijijini.

Tusidanganyane jamani, tukutane 2025
wala sio hivyo. Zinatumika kuziba malipo ya wasimamizi wa uchaguzi. Walifanya kazi kubwa.
 
Ingekuwa sawa kama ongezeko la tozo za miamala na mafuta kwa wanyonge lingelenga kwenda kununua meli kubwa za uvuvi ili tuvue kisasa kwenye kina kirefu, kununua matrekta kwa wakulima ili walime mashamba makubwa, kuchimba madini ya kimkakati kama chuma au kusambaza nishati ya gesi nchini ili watu wasikate miti.

Unapojenga zahanati kila kijiji utahitaji pia kupeleka watumishi, vifaa tiba, madawa na kujenga nyumba za watumishi huko vijijini. Tatizo leo sio kuwa na zahanati kila kijiji, bali ni kuziboresha hizi zilizopo ili zitoe huduma zilizokusudiwa (quality badala ya quantity).

Pesa za kujenga vituo vya afya na shule zilikuwepo ila vipaumbele vya viongozi ilizielekeza kwenye miradi ambayo haigusi wananchi moja kwa moja kama vile kujenga Ikulu kubwa ya kufa mtu, kujenga ukuta melelani, kujenga national park kule Burigi, safari za viongozi ndani na nje ya nchi, kujenga majengo ya wizara na ofisi mpya wakati majengo hayo yapo. Kuhamia Dodoma ni sawa na ni jambo jema, lakini kutumia fedha nyingi kuhamia dodoma wakati watu hawana maji, shule, barabara, umeme, majosho, mbolea, na zahanati zenye watumishi, vifaa tiba na dawa ni kejeli kubwa kwa wananchi ambao wanatakiwa kuongezewa tozo za miamala na mafuta eti kujijengea vitu hivyo.

Binafsi sioni uhusiano uliopo kati ya kuhamia dodoma na upatikanaji wa maji, zahanati, madarasa, umeme, nyumba za watumishi, vifaa tiba na watumishi kwa wananchi wote nchini na hasa vijijini.

Mheshimiwa Mwigulu anataka kutuaminisha kuwa pesa ya kodi, tozo na mauzo ya mazao na madini kama korosho, kahawa, pamba, dhahabu, bandari na uchukuzi, mikopo, misaada na huduma mbalimbali tunazotoa kama nchi sio za kujengea madarasa na zahanati hadi tukamue watu kwenye miamala, mafuta na umeme.

Tusidanganyane jamani, tukutane 2025
1.Meli za uvuvi bajeti yake ipo na zitaanza kuingia mwisho wa mwaka huu
2. Ukimpa mkulima trekta unamsaidia ila hayo mazoa atasafirsha kwa wakati wakati njia na barabara ni mbovu? Tunaongeza thamani ya mazao na maligjafi zisafirishwe kwa urahisi

Watu wengi hukimbia vijijini kwa sababu huduma sio nzuri ukiwaboreshea huduma watakaa huko na kufanya kazi huko mfano kilimo, kwa hiyo ana uhakika wa huduma za afya na mazao yake kufika sokoni kwa wakati

Waziri wa tamisemi ameeleza kwenyenpesa ya tozo kuna asilimia ya kununua vifaa tiba hospitalini

Kumbuka tulikua tunakopa kutekeleza miradi na bajeti zilikua hazikamiliki asilimia 100 kwa sababu fedha haipatikani ya kutosha
 
1.Meli za uvuvi bajeti yake ipo na zitaanza kuingia mwisho wa mwaka huu
2. Ukimpa mkulima trekta unamsaidia ila hayo mazoa atasafirsha kwa wakati wakati njia na barabara ni mbovu? Tunaongeza thamani ya mazao na maligjafi zisafirishwe kwa urahisi

Watu wengi hukimbia vijijini kwa sababu huduma sio nzuri ukiwaboreshea huduma watakaa huko na kufanya kazi huko mfano kilimo, kwa hiyo ana uhakika wa huduma za afya na mazao yake kufika sokoni kwa wakati

Waziri wa tamisemi ameeleza kwenyenpesa ya tozo kuna asilimia ya kununua vifaa tiba hospitalini

Kumbuka tulikua tunakopa kutekeleza miradi na bajeti zilikua hazikamiliki asilimia 100 kwa sababu fedha haipatikani ya kutosha
Tusidanganyane, vipaumbele vyetu ndio chanzo kikubwa cha matatizo yetu. Hizo tozo zenu ni sehemu tu ya kufidia uozo kwenye vipaumbele vyetu.

Tangu uhuru tuliamua vipaumbele vyetu viwe kuikomboa Afrika, kujenga ujamaa, siasa na muungano. Hata kuhamia Dodoma ni kete tu ya kisiasa isiyofungamana na ujenzi wa barabara vijijini, upatikanaji wa maji, umeme na dawa kwenye hospitali zetu.

Mipango yetu ni kuhakikisha kuwa CCM inabaki madarakani milele. Hela kiasi chochote itatumika kufanya chochote ili CCM isitoke madarakani.

Pesa ya kujenga barabara na kupatia watu wote elimu, afya, maji na vifaatiba ipo kwenye madini, bahari, mito na maziwa; misitu, utalii, na kilimo kama tungekuwa na chama na viongozi serious.
 
Back
Top Bottom