Huyu Kumbusho ni vema angeweka ushahidi kuwa bandari inakodishwa kwa miaka 100 otherwise, akamatwe kwa kuleta tafrani. Kwa namna mazingira ya biashara, uchumi na uwekezaji yanavyokwenda kwa Sasa, sidhani hata kama tungekuwa na JUHA ambaye angeingia mkataba wa miaka 100 kwa jambo hilo. Kumbusho atoe ushahidi otherwise akamatwe kwa upotoshaji.
 
Kuna upotoshwaji mkubwa sana unafanywa juu ya mkataba unaotaka kusainiwa kati ya serikali na kampuni ya DP World na wanasiasa wa upinzani na watu wasio na taarifa sahihi kuhusu jambo hili.

Watu wetu wamezoea kutokusoma mambo na kuokota mambo mitandaoni na kutafanya kuwa ndiyo rasmi. Nimesoma makubaliano haya kurasa zote 33 sijaona mahali palipotajwa miaka 100 imekubaliwa kukodishwa DP World bandari.

Sijajua wanaosema bandari imekodishwa miaka 100 wanatoa wapi hizi taarifa! Ni tabia ile ile ya kuzusha mambo na kupayuka bila kuwa na ushahidi. Tabia hii inaleta taharuki sana kwa watanzania bila sababu za msingi.

Wote ni mashahidi wa jinsi TICTS na akina Karamagi wamefanya kazi bandarini kwa miaka 26 na hakuna uwekezaji wamefanya mpaka wamepelekea bandari ya Dar Es Salaam pamoja na umuhimu wake kuzidiwa na bandari mpaka ya Mombasa kwa sababu huduma mbovu na TICTS hawakuwa wanawekeza kwenyw kununua vifaa kwa miaka yote 26 ya mkataba wao. Hatuwezi kuwa na bandari haina vifaa na meli zinasubiri siku 14-21 kupakua mizigo wakati jambo hilo kilitakiwa kufanywa kwa masaa 12-24 tu na hicho ndicho kiwango cha kimataifa cha ufanisi wa bandari kupakua mizigo.

Nani aliwahi kuhoji miaka 26 ya TICTS kuwa watoa huduma hapo bandarini? Nani aliwahi kuwaza na kujua TICTS wamekaa hapo bandarini kwa miaka 26? Marais wangapi wamepita na hawakuwa na uthubutu wa kuwaondoa TICTS pamoja na utapeli wao?

Awamu hii iliamua kuifanya bandari kuwa lango kuu wa uchumi na wakaamua kutafuta muwekezaji mwenye uzoefu na mwenye hela ya kufanya kazi na DP World wakawa chaguo.

Serikali imeenda mbali zaidi kufanya mambo wazi na kupeleka bungeni kujadili jambo hili, nataka watu wanaopinga DP World waje hapa watuambie lini TICTS na mikataba yao ilijadiliwa bungeni kwa uwazi huu?

Haikuwa hivyo kwa kuwa TICTS walikuwa wanagawa rushwa haswa na Karamagi ndiye alikuwa kinara na viongozi wengi wakiopita walikuwa wanufaika.

Serikali hii imekuwa jasiri kuliko zote na kuwang'oa TICTS kwa sababu walikuwa wanadharau mkataba wao na hakuna kitu cha maana wamefanya na bado walikuwa wanapewa kikataba kihovyo hovyo tu na kwa kugawa rushwa.

Upotoshaji unaofanywa kuhusu DP World ni jambo la hovyo na aibu sana. DP World wanakwenda kuifanya bandari ya Dar Es Salaam kuwa ya kisasa na yenye ufanisi sana kutokana na aina ya uwekezaji na fedha wanakwenda kuweka na kufanya mabadiliko kwenye hii bandari.
 
Hatimaye wazee wa buku 7 mmekamilisha script...
Mbona mmetumia muda ivo?
 
Issue sio TICTS. Issue ni ufisadi na urasimi wa CCM na KIKWETE & Co. DP World yenyewe ni ya wazawa ila registered UAE kwa wajomba. Kwahiyo kuwapa DPW haitasaidia kitu zaidi ya kuleta unyanysaji na uzalilishaji, ufisadi pamoja na udini katika nchi hii.
 
Tunakoelekea kama huenda tukawa nchi iliyofikisika zaidi dunian kiuchumi na kifikra. Tutakuwa tunawaza Nini maana urithi na rasilimali zetu zoote tumewauzia wagen.
 
100%
 
Hiyo nchi ya Dubai iko dunia ipi?
 
Mkiuza hii nchi mapema namna hii, mnategemea hiyo awamu ya Saba mtakuta Cha kuuza Tena?
Tumesikia Kuna bilionea la kibeberu la kimarekani limeshamegewa kipande Cha ardhi yetu bila ridhaa yetu.
Mnataka kuuza bandari hata vitukuu vitushangae.
Znz wameshauza bandari Yao Sasa hivi wanasema Kuna ardhi Yao bagamoyo.
 
 
Hili bunge hatutalisamehe, kazi kuhongwa mitunguni ya gesi, wanafilisi nchi pumbavu kabisa. Hapo kuna royal famili nyingine inataka kuzaliwa hamna haya nyie katika dimbwi la umaskini huu tulionao.
 
Ukiona Kiongozi anashiriki sana kwenu vimatukio vidogo vidogo ( vyenye attention ya watu wengi)ujue Kuna kitu anakificha! Kuna mlevi mmoja Kijijini kwetu , alikuwa anaiba mtama Kwa wazazi kwenda kubadilishana na pombe! Sasa Ili kuondoa attention ya watu alikuwa akifika tu kwenye pombe anaanza kuimba! Watu watu waliishia kushangilia nyimbo zake , bila kubaini kuwa kwenyenkoti lake kubwa alifunika kakiroba ka mtama!
Kununua magoli!
Chakula Cha jioni!
Fei Toto!
Mara paap Oktoba 2025🤔
 
Hivi sisi ngozi nyeusi kwa miaka yote hii tuliotoa wasomi Maprofesa tena wengine wana PHD 6, tumeshindwa kabisa kuendesha bandari hadi tuombe kusaidiwa na Waarabu ?

Mbona sijawahi kuona Mwarabu au Myunani akija Tanzania kutuomba tukamwendeshee Bandari zake huko kwao.

Futeni basi hivyo vyuo vikuu vyenu mnavyodai vinatoa Degree, ili mbaki nyumbani wageni waje waendeshe nchi yetu.

Mbona hamuikodishi CCM iendweshwe na Wazayuni ?

Kweli Ngozi nyeusi hatujithamini, miaka 62 ya Uhuru hata kuendesha Bandari tumeshindwa.
Nchi ina vyuo Kikuu zadi ya 100, Maprofesa Lipumba zaidi ya Laki Moja, kuendesha bandari mnashindwa.

Huenda kabisa sisi Ngozi nyeusi tulitoka kwa Manyani.
 
Kama DP world Ni kampuni nzuri Basi ipewe bunge iliendeshe maana huko ndio Kuna ubadhirifu wa kupindukia.
Kisha wapewe mkoa wa Geita ambàko mauaji yamezidi.
wapewe wizara ya nishati na wizara ya ardhi. HIZI ZIMESHINDIKANA.
Why bandari?
Wapewe na Takukuru ili kuwafuatilia wanaofuja pesa za Serikali kwa mujibu wa Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali.

Why wapewe kunakomwagika pesa kirahisi tu ?
 
Mbona wanauza Tanzania bara tu ? Zanzibar hakuna cha kuuza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…