Dan Zwangendaba
JF-Expert Member
- Apr 25, 2014
- 5,814
- 8,118
Huyu Kumbusho ni vema angeweka ushahidi kuwa bandari inakodishwa kwa miaka 100 otherwise, akamatwe kwa kuleta tafrani. Kwa namna mazingira ya biashara, uchumi na uwekezaji yanavyokwenda kwa Sasa, sidhani hata kama tungekuwa na JUHA ambaye angeingia mkataba wa miaka 100 kwa jambo hilo. Kumbusho atoe ushahidi otherwise akamatwe kwa upotoshaji.
Hatimaye wazee wa buku 7 mmekamilisha script...Kuna upotoshwaji mkubwa sana unafanywa juu ya mkataba unaotaka kusainiwa kati ya serikali na kampuni ya DP World na wanasiasa wa upinzani na watu wasio na taarifa sahihi kuhusu jambo hili.
Watu wetu wamezoea kutokusoma mambo na kuokota mambo mitandaoni na kutafanya kuwa ndiyo rasmi. Nimesoma makubaliano haya kurasa zote 33 sijaona mahali palipotajwa miaka 100 imekubaliwa kukodishwa DP World bandari.
Sijajua wanaosema bandari imekodishwa miaka 100 wanatoa wapi hizi taarifa! Ni tabia ile ile ya kuzusha mambo na kupayuka bila kuwa na ushahidi. Tabia hii inaleta taharuki sana kwa watanzania bila sababu za msingi.
Wote ni mashahidi wa jinsi TICTS na akina Karamagi wamefanya kazi bandarini kwa miaka 26 na hakuna uwekezaji wamefanya mpaka wamepelekea bandari ya Dar Es Salaam pamoja na umuhimu wake kuzidiwa na bandari mpaka ya Mombasa kwa sababu huduma mbovu na TICTS hawakuwa wanawekeza kwenyw kununua vifaa kwa miaka yote 26 ya mkataba wao. Hatuwezi kuwa na bandari haina vifaa na meli zinasubiri siku 14-21 kupakua mizigo wakati jambo hilo kilitakiwa kufanywa kwa masaa 12-24 tu na hicho ndicho kiwango cha kimataifa cha ufanisi wa bandari kupakua mizigo.
Nani aliwahi kuhoji miaka 26 ya TICTS kuwa watoa huduma hapo bandarini? Nani aliwahi kuwaza na kujua TICTS wamekaa hapo bandarini kwa miaka 26? Marais wangapi wamepita na hawakuwa na uthubutu wa kuwaondoa TICTS pamoja na utapeli wao?
Awamu hii iliamua kuifanya bandari kuwa lango kuu wa uchumi na wakaamua kutafuta muwekezaji mwenye uzoefu na mwenye hela ya kufanya kazi na DP World wakawa chaguo.
Serikali imeenda mbali zaidi kufanya mambo wazi na kupeleka bungeni kujadili jambo hili, nataka watu wanaopinga DP World waje hapa watuambie lini TICTS na mikataba yao ilijadiliwa bungeni kwa uwazi huu?
Haikuwa hivyo kwa kuwa TICTS walikuwa wanagawa rushwa haswa na Karamagi ndiye alikuwa kinara na viongozi wengi wakiopita walikuwa wanufaika.
Serikali hii imekuwa jasiri kuliko zote na kuwang'oa TICTS kwa sababu walikuwa wanadharau mkataba wao na hakuna kitu cha maana wamefanya na bado walikuwa wanapewa kikataba kihovyo hovyo tu na kwa kugawa rushwa.
Upotoshaji unaofanywa kuhusu DP World ni jambo la hovyo na aibu sana. DP World wanakwenda kuifanya bandari ya Dar Es Salaam kuwa ya kisasa na yenye ufanisi sana kutokana na aina ya uwekezaji na fedha wanakwenda kuweka na kufanya mabadiliko kwenye hii bandari.
Issue sio TICTS. Issue ni ufisadi na urasimi wa CCM na KIKWETE & Co. DP World yenyewe ni ya wazawa ila registered UAE kwa wajomba. Kwahiyo kuwapa DPW haitasaidia kitu zaidi ya kuleta unyanysaji na uzalilishaji, ufisadi pamoja na udini katika nchi hii.Kuna upotoshwaji mkubwa sana unafanywa juu ya mkataba unaotaka kusainiwa kati ya serikali na kampuni ya DP World na wanasiasa wa upinzani na watu wasio na taarifa sahihi kuhusu jambo hili.
Watu wetu wamezoea kutokusoma mambo na kuokota mambo mitandaoni na kutafanya kuwa ndiyo rasmi. Nimesoma makubaliano haya kurasa zote 33 sijaona mahali palipotajwa miaka 100 imekubaliwa kukodishwa DP World bandari.
Sijajua wanaosema bandari imekodishwa miaka 100 wanatoa wapi hizi taarifa! Ni tabia ile ile ya kuzusha mambo na kupayuka bila kuwa na ushahidi. Tabia hii inaleta taharuki sana kwa watanzania bila sababu za msingi.
Wote ni mashahidi wa jinsi TICTS na akina Karamagi wamefanya kazi bandarini kwa miaka 26 na hakuna uwekezaji wamefanya mpaka wamepelekea bandari ya Dar Es Salaam pamoja na umuhimu wake kuzidiwa na bandari mpaka ya Mombasa kwa sababu huduma mbovu na TICTS hawakuwa wanawekeza kwenyw kununua vifaa kwa miaka yote 26 ya mkataba wao. Hatuwezi kuwa na bandari haina vifaa na meli zinasubiri siku 14-21 kupakua mizigo wakati jambo hilo kilitakiwa kufanywa kwa masaa 12-24 tu na hicho ndicho kiwango cha kimataifa cha ufanisi wa bandari kupakua mizigo.
Nani aliwahi kuhoji miaka 26 ya TICTS kuwa watoa huduma hapo bandarini? Nani aliwahi kuwaza na kujua TICTS wamekaa hapo bandarini kwa miaka 26? Marais wangapi wamepita na hawakuwa na uthubutu wa kuwaondoa TICTS pamoja na utapeli wao?
Awamu hii iliamua kuifanya bandari kuwa lango kuu wa uchumi na wakaamua kutafuta muwekezaji mwenye uzoefu na mwenye hela ya kufanya kazi na DP World wakawa chaguo.
Serikali imeenda mbali zaidi kufanya mambo wazi na kupeleka bungeni kujadili jambo hili, nataka watu wanaopinga DP World waje hapa watuambie lini TICTS na mikataba yao ilijadiliwa bungeni kwa uwazi huu?
Haikuwa hivyo kwa kuwa TICTS walikuwa wanagawa rushwa haswa na Karamagi ndiye alikuwa kinara na viongozi wengi wakiopita walikuwa wanufaika.
Serikali hii imekuwa jasiri kuliko zote na kuwang'oa TICTS kwa sababu walikuwa wanadharau mkataba wao na hakuna kitu cha maana wamefanya na bado walikuwa wanapewa kikataba kihovyo hovyo tu na kwa kugawa rushwa.
Upotoshaji unaofanywa kuhusu DP World ni jambo la hovyo na aibu sana. DP World wanakwenda kuifanya bandari ya Dar Es Salaam kuwa ya kisasa na yenye ufanisi sana kutokana na aina ya uwekezaji na fedha wanakwenda kuweka na kufanya mabadiliko kwenye hii bandari.
Tz ninayoifahamu inawezekana tena haraka sana.Nikataka kushangaa How uipe kampuni sehemu ya kimakakati kama bandari miaka mia moja
100%Issue sio TICTS. Issue ni ufisadi na urasimi wa CCM na KIKWETE & Co. DP World yenyewe ni ya wazawa ila registered UAE kwa wajomba. Kwahiyo kuwapa DPW haitasaidia kitu zaidi ya kuleta unyanysaji na uzalilishaji, ufisadi pamoja na udini katika nchi hii.
Hiyo nchi ya Dubai iko dunia ipi?Tarehe 5 Juni 2023, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitoa Taarifa kwa Umma kuhusu mwaliko wa Wadau wote kutoa maoni kuhusu Azimio la Bunge la mapendekezo ya Kuridhia Makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania a Serikali ya Dubai kuhusu ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii kwa ajili ya Uendelezaji na Uboreshaji wa Utendaji Kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania la Mwaka 2023.
Kufuatia Taarifa hiyo kwa Umma iliyotolewa kupitia tovuti ya Bunge, kumekuwa na upotoshaji katika mitandao ya kijamii kwamba "Serikali imepanga kuipa kampuni ya DP World ya Falme ya Dubai kandarasi ya undeshaji wa shughuli za Bandari ya Dar es Salaam kwa muda wa miaka mia moja (100)".
Kufuatia kusambaa kwa taarifa hizo, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inapenda kuwajulisha Wateja, Wadau wa Kitaifa a Kimataifa na Umma kwa jumla kwamba, taarifa hizo sio sahihi, ni upotoshaji unaofanywa kwa makusudi na watu wenye nia ovu ya kukwamisha mipango thabiti ya Nchi katika kuongeza ufanisi wa Sekta ya Bandari Nchini kwa maslahi mapana ya Taifa.
Taarifa sahihi ni kuwa, Azimio la Bunge linahusu Mkataba ambao Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaingia na Serikali ya Dubai wenye ukomo wa miezi kumi na mbili (12) kwa ajili ya kutoa nafasi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujadiliana na Serikali ya Dubai kuhusu maeneo ambayo Serikali hizo mbili zinaweza kushirikiana katika boreshaji na endelezaji wa Sekta ya Bandari Nchini Tanzania.
Ushirikiano wa Nchi mbili za Dubai a Tanzania una lengo la kongeza ufanisi wa huduma za Bandari Nchini, kukuza ajira za Watanzania na kufungua fursa za kiuchumi na kijamii kupitia uwekezaji kwenye baadhi ya maeneo ya Bandari ya Dares Salaam, maeneo huru ya kiuchumi na viwanda (Special Economic and Industrial Zones) kwa kujenga viwanda pamoja na uwekezaji katika mnyororo mzima wa usafirishaji kutoka Bandari za Tanzania kwenda chi za jirani ambazo zinatumia Bandari zetu.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inawaomba Wateja, Wadau na Umma kutambua kwamba, jitihada zote na hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita katika kuvutia wekezaji Nchini hususan kwenye maeneo ya Banadari, zinalenga kumaliza changamoto za muda mrefu ikiwemo ucheleweshwaji wa meli, mizigo na kukosekana kwa ufanisi katika Bandari zetu.
View attachment 2648437View attachment 2648438
Pia soma: Tanzania inatarajiwa kuingia mkataba na kampuni ya DP World ya Dubai kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam
Na wapo wengi sana!Kwa watu wenye mawazo kama yako ccm ita ongoza milele
Wapewe na Takukuru ili kuwafuatilia wanaofuja pesa za Serikali kwa mujibu wa Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali.Kama DP world Ni kampuni nzuri Basi ipewe bunge iliendeshe maana huko ndio Kuna ubadhirifu wa kupindukia.
Kisha wapewe mkoa wa Geita ambàko mauaji yamezidi.
wapewe wizara ya nishati na wizara ya ardhi. HIZI ZIMESHINDIKANA.
Why bandari?
Mbona wanauza Tanzania bara tu ? Zanzibar hakuna cha kuuza?Tarehe 5 Juni 2023, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitoa Taarifa kwa Umma kuhusu mwaliko wa Wadau wote kutoa maoni kuhusu Azimio la Bunge la mapendekezo ya Kuridhia Makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania a Serikali ya Dubai kuhusu ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii kwa ajili ya Uendelezaji na Uboreshaji wa Utendaji Kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania la Mwaka 2023.
Kufuatia Taarifa hiyo kwa Umma iliyotolewa kupitia tovuti ya Bunge, kumekuwa na upotoshaji katika mitandao ya kijamii kwamba "Serikali imepanga kuipa kampuni ya DP World ya Falme ya Dubai kandarasi ya undeshaji wa shughuli za Bandari ya Dar es Salaam kwa muda wa miaka mia moja (100)".
Kufuatia kusambaa kwa taarifa hizo, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inapenda kuwajulisha Wateja, Wadau wa Kitaifa a Kimataifa na Umma kwa jumla kwamba, taarifa hizo sio sahihi, ni upotoshaji unaofanywa kwa makusudi na watu wenye nia ovu ya kukwamisha mipango thabiti ya Nchi katika kuongeza ufanisi wa Sekta ya Bandari Nchini kwa maslahi mapana ya Taifa.
Taarifa sahihi ni kuwa, Azimio la Bunge linahusu Mkataba ambao Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaingia na Serikali ya Dubai wenye ukomo wa miezi kumi na mbili (12) kwa ajili ya kutoa nafasi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujadiliana na Serikali ya Dubai kuhusu maeneo ambayo Serikali hizo mbili zinaweza kushirikiana katika boreshaji na endelezaji wa Sekta ya Bandari Nchini Tanzania.
Ushirikiano wa Nchi mbili za Dubai a Tanzania una lengo la kongeza ufanisi wa huduma za Bandari Nchini, kukuza ajira za Watanzania na kufungua fursa za kiuchumi na kijamii kupitia uwekezaji kwenye baadhi ya maeneo ya Bandari ya Dares Salaam, maeneo huru ya kiuchumi na viwanda (Special Economic and Industrial Zones) kwa kujenga viwanda pamoja na uwekezaji katika mnyororo mzima wa usafirishaji kutoka Bandari za Tanzania kwenda chi za jirani ambazo zinatumia Bandari zetu.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inawaomba Wateja, Wadau na Umma kutambua kwamba, jitihada zote na hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita katika kuvutia wekezaji Nchini hususan kwenye maeneo ya Banadari, zinalenga kumaliza changamoto za muda mrefu ikiwemo ucheleweshwaji wa meli, mizigo na kukosekana kwa ufanisi katika Bandari zetu.
View attachment 2648437View attachment 2648438
Pia soma: Tanzania inatarajiwa kuingia mkataba na kampuni ya DP World ya Dubai kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam
Chama cha mboga wanaweza kuuza hata ikulu.Nikataka kushangaa How uipe kampuni sehemu ya kimakakati kama bandari miaka mia moja