TRA fuatilieni hii kampuni ya wachina inayoitwa Hiview International Co Ltd, wanakwepa kodi sana

Awakomalie watarajesha tu,tena aambatane na maofisa wa TRA na TAKUKURU atawashika tu
Akikomaa inakula kwake,

Hazijui figisu za mjini uyu.

Akileta ujuaji,
Mzigo unataifishwa afu watu wa tra wanajifanya wamempiga faini feki muuzaji.

Kisha wanamwambia jamaa akungute matako yake haende maana kwa mujibu wa sheria Mali ya magendo hairudishwi kwa mhusika.

Afu baadae,
Jamaa wa maduka wanaenda kuwapoza tra kitu kidogo afu mzigo unawarudia wao wenyewe.

Mjini shule bwashee[emoji12]
 
unashangaa nini mbona hata TRA penyewe ukiingia ofisini unakutana na madalali wanaoweza kukuchezeshea ili kodi ipungue? labda kama ndio umeanza biashara hivi karibuni ndio utashangaa kusikia unaweza kukutana na dalali ndani ya ofisi flani
Atakua mgeni wa biashara uyu
 
Soma maelezo yangu vizuri.hakuna sehemu nimelia bei
Mkuu,
Kubali ukatae wee Ni mgeni kwenye biashara.

Kama na wenzio walokuelekeza ilo chimbo wangekua wanakamatwa na kupigwa izo faini kila siku,
bila shaka na wao wangeshafilisika na kamwe usingelijua pia ilo chimbo.

Wafanyabiashara wa JUMLA always huwa tunalindana.

HAKUNA Mfanyabiashara was JUMLA anaclaim exact efd receipt,

Miundo mbinu iko wazi na inaeleweka mjini kote.

Unakwama wapi mkuu?
 
hajawahi kuwepo kabisa na ukileta mambo ya professionalism kwenye biashara za Tanzania utapotea mapema sana kwenye scene, do what you do to survive, siri ya biashara za bongo unapaswa kumjua mtu anayemjua mtu, information is akey
Mtoa mada aliliparamia chimbo la watu kichwa kichwa.

Hakua na information Sahii ya Nini hatar ya alichokua anakifata.

Wengi Sana tumekumbwa na madhila ya hivi,
Na hatujawai Kuna apa Kuanzisha Uzi.

Na nimfahamishe mtu mtoa mada,
Kitendo alichokifanya kuweka details zake Kwenye Huu Uzi, ili kuwasagia kunguni wenzie.

Lawama zote zitaenda kwa waliokuelekeza pale.

Na always Kwenye biashara ukishajulikana hunaga kifua afu unatabia za snitch snitch,

kinachofata huwa Ni kukufungia tu vioo Kabisa na ikiwezekana kukupoteza Kabisa Kwenye ramani usiwaletee washkaji wengine jau.

Kama Kuna mtu wako wa karibu mnafanya biashara na ameuona huh Uzi wako,
Bila shaka utaona ambavyo mabadiliko jinsi gan hajafurahushwa na hiki ulichokifanya humu.
 
Muuzaji kakujibu juu juu tu kwa maana anaaasume wee Ni mwenyeji wa hizi biashara na unajua utaratibu husika.

Niliwai mpeleka rafk angu mmoja kampuni flai Kwenye godown Moja kupakia mzigo.

Baada ya kuandika oda,
jamaa mchana kweupe kumbe tayar keshaanda fuso ije ipakie.

Afu asivyo na aibu,
baada ya kulipa akaomba risiti, Akapewa ya maandishi.
Ghafla kaanza kulalamikia eti anataka apewe ya efd.

Mhasibu akaingia ndani na kurudi na kitita Cha pesa zake zote (14.2million) na kumkabidhi na kumwambia "PESA ZAKO HIZI HAPA KANUNUE KWINGINE".

Niko zangu nje naongea na simu,
Jamaa anakuja analalamika eti hawana customer care nzuri wamenirudishia pesa.

Nkarudi ndai kujua tatizo Nini,

Wauzaji wanalalamika nimewaletea mtu wa ovyo afu mshamba Sana.

Ila baadae walimpa TU mzgo kupitia jina langu.
Kwa utaratibu ule ule ulozoeleka kwa wadau.

Kwaiyo watu Aina ya mtoa mada,
Mjini ni wengi
 
A
Asante Sana mzalendo wa kweli.Hawa TRA siku hizi wanafanya utani na makusanyo
 
Hii nchi ni tajiri Sana, naangalia michango ya nguli wa biashara wanavyokwepa kulipa Kodi wakishirikiana na TRA, alafu TRA hao hao ofisini wanajilipa mi-allowance ya kufa mtu....dah!

Rais aliomba maelezo ya kwanini polisi wengi wanagombamia wapangwe trafiki, sijuhi kama alijibiwa!
 
Nchi ngumu Sana Hii mkuu, kila mtu anapambania ugali wake
 
Ntakutafuta mkuu..nataka kuyajua vyema machimbo ya mjini.
 
pole jombaa.
ila ningekuwa ni mim hela wanatoa mzee tena ya ukweli. unakubalije kupigwa kirahc hivyo aisee! hao hao TRA ndio wakuwakamatisha. mi nakumbuka miaka hyo ninajenga kuna mhind aliniletea za kuleta nikampa General mmoja wa Jwz laki 3 akajifanya mzigo ni wake mi nilitumwa tu. kilichotokea yule mhind hatakaa anisahau aisee.
 
Mkuu muwe mnaweka na risiti,sio kila mtu anataka janja janja yenu.
 
Duh,changamoto
 
Mkuu muwe mnaweka na risiti,sio kila mtu anataka janja janja yenu.
Wazalendo,
Huwa mnasehemu yenu ya kuchukulia mzigo kwa Bei kubwa afu mnapewa na risiti halali ya efd.

Sisi Wahujumu uchumi huwa tuna sehemu yetu rasmi ya kuchukulia mizigo kwa Bei rahisi zaidi afu kwa makubaliano ya hiari ya bila ya kupewa risiti but at your own risk.

Chaguo Ni lako, usuke au unyoe
 
Nahisi TRA wangekua serious, hata haya matozo ya kijinga yasingekuwepo kwa sasa.
Mama uku kwa wafanyabiashara keshaona maruweruwe tayar
Anacheza TU mziki wanaoutaka wafanyabiashara.

Ndo maana kakomaa na miamala maana uko kila kitu Kiko wazi
 
Ntakutafuta mkuu..nataka kuyajua vyema machimbo ya mjini.
Haina shida mkuu,
Hizi biashara usipozielewa miundo yake huwezi toboa apa mjini.

Utajikuta mshindani wako anauza Bei ya reja reja ndogo kuliko Bei yako wewe uliyonunulia mzigo wa jumla.
Mfano: umenunua CTN kwa 10,000 ili uuze 12,000 rejareja.
Afu Kuna jitu liko opposite na wewe linauza rejareja 8,000, na wale wanaonunuaga mzigo mkubwa linawashushia mpaka elfu 6 kila katoni[emoji1787]

Wateja wote wanakuhama unaanza kumsingizia wachawi.

Kumbe machimbo huyajui, umezoea TU kwenda kununua maduka ya wachuuzi yanayoonekana usoni.

Wakati magwiji tunaendaga kupakia moja kwa moja godown au Kwenye makontena ya maboss uko majumbani mwao mizigo isiyokua na risiti, haijalipiwa ushuru wa bandari, Wala haijatozwa gharama za tbs na taka taka nyinginezo.

Tukifika sokoni,
Tunakukimbiza mchaka mchaka unarudi mwenyewe kijijini kwenu kulima mbaazi bila shuruti[emoji12]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…