TRA waunde kitengo cha upangishaji wa nyumba, kila mwenye nyumba aripoti TRA anapotaka kupangisha na iwe kwa mujibu wa sheria

Wanapewaga nauli elf20 or 30k ujue..!

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Mataga akili zimeanza kurejea taratibu, ingekuwa hili tamko limetolewa enzi za mwendazeke ungesema zidumu fikra sahihi za msaidizi wa mwenyekiti wa chama.
 
Mtumishi wa umma mwenye mshahara wa shilingi 300,000 kwa mwezi, analipa kodi, halafu dalali anaepangisha na kulipwa kodi ya mwezi(shilingi 300,000, 400,000 na kuendelea) halipi chochote na tunaona sawa tu.

Tanzania nchi ya ajabu sana!
 
Sasa kama hela unajua ni ngumu, kati ya dalali na mpangaji, nani anastahili kutetewa?
Tatizo Ni kwamba mfumo mzima was biashara ya upangishaji hapa bongo hauko rasmi.

Hauko rasmi kwasababu Hii biashara Haina Bei elekezi.

Kila kitu Ni maelewano,

Sasa serikali itakusaidiaje ikiwa Ni wee mpangaji, dalali na mwenye nyumba mlielewana wenyewe na wewe ukakubali kwa hiari yako?

Hapo,
Suala litabaki mwenye shida kuliko mwenzie ndie atoboke mfukoni.

Na kibongo bongo,
Kwenye suala la mpangishaji na mpangishwaji.

Mpangishwaji always ndo mwenye shida, kwaiyo Lazima atoboke yeye atake asitake mfumo ndo umekaa hivyo.
 
Tafuta Hera Ujenge then Jipereke TRA , Kama unaona Kujenga Nyumba ni Kitu rahisi kihivyo.
Mtoa mada anaongea akidhani kujenga nyumba Ni rahisi Kama kuvaa boxa.

Vuuup tayar ishakaa matakoni[emoji2]
 
Nenda kwingine kwani lazima iwe hapo? Ulijuaje kuwa hiyo nyumba inapangoshwa taarifa ulipata wapi?

Nyumba zingine waweza ona kibao kimeandikwa nyumba hii inapangishwa wasiliana na mwenye nyumba kwa namba hii lakini hicho kibao kimewekwa na dalali sio mwenye nyumba.

Mwenye nyumba hukabidhi kazi dalali kuwa amletee watu hata Kama ulisikia watu wakiongea dalali ndie husambaza hizo taarifa sehemu mbalimbali kwa jamaa marafiki vijiweni sehemu za mikusanyiko no
Ndipo wewe wazidaka hizo taarifa kuwa kuna mahali nyumba yapangishwa .Analipwa kihalali hata Kama hukukutana naye
 
Asikuelewa Basi akapimwe
 
𝗧𝗥𝗔 𝘁𝗲𝗻𝗮 𝗸𝘄𝗲𝗻𝘆𝗲 𝗻𝘆𝘂𝗺𝗯𝗮 𝘇𝗲𝘁𝘂 𝗯𝗶𝗻𝗮𝗳𝘀𝗶? 𝗪𝗮𝗱𝗲𝗮𝗹 𝗻𝗮 𝘇𝗶𝗹𝗲 𝘇𝗮 𝘀𝗵𝗶𝗿𝗶𝗸𝗮 𝗹𝗮 𝗻𝘆𝘂𝗺𝗯𝗮 𝗸𝘄𝗮𝗻𝘇𝗮
 
Wazo lako zuri ila hebu fikiria haya.

1.TRA hawako kila mahali, usiwaze mjini mjini tuu.

2.Dalali ni middleman kama agent wengine sema hajarasmishwa.

3.Hayo magari hayaendi bure, hiyo pesa unayomlipa dalali inaweza kuwa ndio hiyo hiyo au zaidi ukichanganua

4.Uswahilini chumba cha 15,000 cha giza unaiingiza TRA.

Yaboreshwe maisha ya wananchi kwanza then menginw yatakuja
 
Mtumishi wa umma mwenye mshahara wa shilingi 300,000 kwa mwezi, analipa kodi, halafu dalali anaepangisha na kulipwa kodi ya mwezi(shilingi 300,000, 400,000 na kuendelea) halipi chochote na tunaona sawa tu.

Tanzania nchi ya ajabu sana!
Ni jambo la kawaida kabisaa kwa madalali wa mikocheni, masaki, upanga, kumkuta anapata dollar mpaka 2,000 kiulaini kabisaa kama kodi ya mwezi mmoja toka kwa mpangaji na wala halipi kodi popote.
 
Nishakwambia,
Hii biashara ni ya maelewano huwezi kulalamikia popote ukaskilizwa.

Kama hujaridhika unaachana na uyo dalali unaenda kwingine.

Wewe ndo mwenye shida ya nyumba, dalali Wala mwenye nyumba wao hawana shida na wewe.

Usipotaka utakuja, usipotaka atakuja mwenzio.

Na wenye nyumba wengi,
Bila kuelewana na dalali wako hakupangishi nyumba.

Huo ndo mfumo uliopo,
Hapo Ni win-win situation.

Wee Jenga nyumba afu uanze kuipangisha bila dalali uone shughuli yake.
 
Unaongelea habari ya vijijini wakati humu mijini tu kulikojaa majumba ya kupangisha wameshindwa kukusanya hiyo kodi licha ya kuwa na sheria inayowaruhusu kukusanya kodi?
 
Ni jambo la kawaida kabisaa kwa madalali wa mikocheni, masaki, upanga, kumkuta anapata dollar mpaka 2,000 kiulaini kabisaa kama kodi ya mwezi mmoja toka kwa mpangaji na wala halipi kodi popote.
Na serikali ipo na inaona sawa tu.
 
Kwani mpangaji anaokota hiyo hela?
Nishakwambia,
Kupangisha Nyumba kwa bongo hii Ni huduma na sio biashara.

Kwaiyo,
Hailipi Kama unavodhani.

Pale wewe ni Kama KENGE,
Yaani umepewa TU pango ujisitiri Kwa muda usinyeshewe([emoji2] joke)

Pango Ni sehemu TU ya kujisitiri kwa muda ukiwa porini ukipambana utoboe.

Ndo maana pesa unayomlipa mwenye nyumba yako,
Kiserikali inatambulika kama PESA YA PANGO. Na Wala haiitwi Kodi ya nyumba.
 
Hata kuuziwa vocha na makampuni ya simu ni huduma.
 
Mifumo ikiwekwa vizuri hata nyumba iliyopo nyayoni mwa Tanzania ikipangishwa, kodi TRA watalipwa tu nielewe nimesema mifumo ikiwekwa vizuri. Aisee kuna nchi wana msemo wao kuwa ukikanyaga ardhi ya nchi yao kuna vitu viwili hakika huwezi kwepa hata ufanyeje ni suala la muda tu vitu hivi vitakupata kwanza ni kifo pili ni kulipa kodi. Hivi kwa mfano wabunge watunge sheria kuwa mpangaji akikwepa kupeleka kodi ya zuio toka kwenye kodi aliyomlipa mwenye nyumba atapata kifungo cha miaka kadhaa jela au let say atalipa faini ambayo ni sawa na kodi ya hiyo nyumba aliyopanga ya miezi sita au mwaka we unafikiri nan kweupeee atakwepa kupeleka hiyo kodi ya zuio?

Unajua nchi zilizoendelea sio kwamba wananchi wake wanapenda saaaaaana kulipa kodi but wamewekewa mifumo ambayo kukwepa kodi na kutokujulikana kabisaa ni ngumu sana so automatically wanajikuta kodi wanalipa tu.
 
Hata kuuziwa vocha na makampuni ya simu ni huduma.
Makamouni ya simu yanafanya biashara yenye kupata faida

Ulisikia wapi mwenye nyumba ya kupangisha kwa makazi anapata faida wewe?
 
udalali ni ajira labda waweke regulation dhidi yao sio TRA kuchukua jukumu vijana wengi wamejiajiri huku acheni mawazo potofu ukilipa ya mwezi ni fresh kwani unalipa tena
Wapangaji wengi hawawezi kulipa kodi juu ya miezi mitatu. Wangepewa 10%. Mwenye nyumba 5% na mpangaji 5%.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…