TRA waunde kitengo cha upangishaji wa nyumba, kila mwenye nyumba aripoti TRA anapotaka kupangisha na iwe kwa mujibu wa sheria

TRA waunde kitengo cha upangishaji wa nyumba, kila mwenye nyumba aripoti TRA anapotaka kupangisha na iwe kwa mujibu wa sheria

Mimi ni miongoni mwa watu naopinga sana madalali kutaka kulipwa kodi ya mwezi mmoja kwani ni kuumiza wapangaji kwa kuwaongezea gharama za maisha. Kibaya zaidi, wako wenye nyumba hawapangishi mtu bila kupitia madalali wao hata kama inawezekana kupanga bila kupitia hao madalali.

Hivyo, nakubaliana na Lukuvi wenye nyumba wawalipe madalali na jambo hili litungiwe sheria na sheria itoe adhabu ya kifungo au faini au vyote kwa pamoja kwa atakaekaidi.


Wazo zuri. Hili naliandika ktk diary yangu bali litakuwa na marekebisho madogo. Nitagombea Urais 2025 tukiwa hai. Nikishinda urais kwanza nyumba zote zilizotaifishwa na Serikali nitazirudisha kwa wamiliki, nyumba zote zilizojemgwa na serikali wanasiasa wakauziana nitazitaifisha na kumilikiwa na sheirika la nyumba. Utaanzishwa sheria ya upangaji ili mpangaji alipe kodi kwa mwezi na isizidi kodi ya miezi miwili. Yaani mwezi mmoja na mwezi unaofata. Na mwezi unaofata utalipa mwezi mmoja mmoja. Na iwe sheria kutolipwa Kofi kwa siku 60 ni sawa na kumwambia mwenye nyumba kuwa hutoendelea kupanga na anahaki ya kuleta mpangaji mwengine. Ila kwa huruma yake anaweza kukuvumilia.

Usimamizi wa walipa Kofi utakuwa chini ya hamlshauri na wenyeviti wa serikali za mitaa badala ya TRA.

Moja ya Sera ktk chama nitakachogombea kitafata Serikali ya majimbo 10 (autonomous) yatakayopewa mamlaka zaidi ya kujiamulia mambo yao wenyewe sawa na mamlaka yaliyopo jimbo la Zanzibar ktk mfumo wa serikali ya ccm.

Na majimbo hayo 10 tutayapa mamlaka zaidi ya jimbo la Znz kwasasa
 
TRA ni mbali naona serikali ya mitaa inaweza kupewa Jukumu hili na ikawa rahisi sana yaani nikitaka kupanga chumba mtaa fulani naenda moja kwa moja ofisi ya serikali za mitaa napewa sifa ya nyumba zilizopo basi naonyeshwa. inaweza hata kuwekwa kiwango cha TSH 10,000 Kwa kila mpangaji ikakuza mifuko ya SM
 
TRA ni mbali naona serikali ya mitaa inaweza kupewa Jukumu hili na ikawa rahisi sana yaani nikitaka kupanga chumba mtaa fulani naenda moja kwa moja ofisi ya serikali za mitaa napewa sifa ya nyumba zilizopo basi naonyeshwa. inaweza hata kuwekwa kiwango cha TSH 10,000 Kwa kila mpangaji ikakuza mifuko ya SM
Kodi za majengo tu Halmshauri ziliwashinda, ndio ije kuwa hii ya kukusanya kodi zinazotokana na kupangisha?
 
Kwani mtumishi wa umma anaelipa PAYE anafanya biashara gani ya kupata faida kupitia hiyo kazi alioajiriwa na serikali?
Anafanya biashara ya kuwahudumia walipa Kodi kwa kutumia taaluma yake.
 
Mimi ni miongoni mwa watu naopinga sana madalali kutaka kulipwa kodi ya mwezi mmoja kwani ni kuumiza wapangaji kwa kuwaongezea gharama za maisha. Kibaya zaidi, wako wenye nyumba hawapangishi mtu bila kupitia madalali wao hata kama inawezekana kupanga bila kupitia hao madalali.

Hivyo, nakubaliana na Lukuvi wenye nyumba wawalipe madalali na jambo hili litungiwe sheria na sheria itoe adhabu ya kifungo au faini au vyote kwa pamoja kwa atakaekaidi.

Sambamba na hilo, TRA waanzishe kitengo cha upangishaji nyumba ambapo wenye nyumba watatakiwa kutoa taarifa TRA wanapotaka kupangisha, kisha jukumu la kutafuta wapangaji liwe la TRA, ila mwenye nyumba aruhusiwe kuweka mpangaji bila kupitia TRA mradi tu alipe kodi.

Utaratibu huu ukiwekwa kisheria, sio tu utaondoa unyonyaji wa madalali, bali uta-facilitate ukusanyaji wa kodi kupitia nyumba za kupangisha na ambao teyari upo kwa mujibu sheria.

Mwanachi yoyote anaetaka nyumba ya kupangisha, atakiwe(kwa mujibu wa sheria) kufika katika ofisi za TRA, na kisha TRA kupitia kitengo husika, watakuwa na jukumu la kuwapangisha wananchi na hapo hapo kukusanya kodi ya serikali.

Tena TRA wanaweza kufanya kazi hii katika mazingira bora zaidi kwa kuwapeleka wateja kwa kutumia magari yao, pikipiki au bajaji maalumu ziitazonunuliwa kwa kutumika fedha zitazokusanywa kupitia upangishaji wa aina hii.

Hakuna kinachoshindikana kama dhamira ipo. Kama kupata baadhi ya huduma tunalazjmika kwanza kupitia TRA, kwani hili la kupangisha kupitia TRA lishindikane?

Haingiii akilini hata kidogo kwa mtumishi wa serikali mwenye mshahara wa shilingi 300,000 kwa mwezi, alipe kodi(PAYE), halafu dalali au mwenye nyumba anaeingiza malaki au mamilion kadhaa anapopangisha, asilipe kodi(huu ni uwendawazimu kabisa).
Ujumbe huu umfikie Waziri mwenye dhamana Mhe. Mwiguru Lameck Nchemba.
Wazo zuri sana hili
 
Nauli ya kuzunguka kukutafutia nyumba nzuri dalali huwa unamlipa wewe?

Kutumia dalali hujalazimishwa katafute mwenyewe basi hujazuiwa pita kila nyumba gonga hodi uliza Kama wanapangisha Kama unaona kazi ya dalali haina maana

Si kila dalali hupewa kazi ya kutafuta mpangaji na mwenye nyumba .Yeye aweza tu kukutafutia ukampa chake Kodi yote ukamalizana na mwenye nyumba yeye hapati hata Mia toka kwa mwenye nyumba

Siku ukihamia mji mgeni na wewe humjui mtu Ndipo utakapojua umuhimu wa dalali iwe utatafuta nyumba ya kupanga ,fremu au kiwanja

Hata akipata pesa kote kote shida iko wapi so ndio kujiajiri kwenyewe? Inaposemwa watu wajiajiri maana yake Nini?
Hauna point hapa Chief.
Who is dalali? Simply ni agent wa kumuunganisha mteja na mwenye nyumba.
Sasa why adai kodi ya mwezi mmoja? Kwanini usiwepo utaratibu akalipwa na mwenye nyumba maana ndiye alompa kazi ya kusaka wateja?

Kwanini isiwepo means nzuri ya wenye nyumba kupata platform ya kutangaza nyumba zao zinazopangishwa na watu wakapata nafasi ya kuziona ma katika malipo hayo Serikali ikakusanya kodi?

Dalali kama ni muhimu kwanini formula yake inaumiza mpangaji pekee?
 
Sawa, ila kaa ukijua TRA wenyewe ni moja ya taasi failure hapa nchini..
Sio kila kazi wafanye wenyewe, sema labda tungesajili madalali ili nao walipe kodi, maana kumbuka mwenye nyumba analipa kodi kupitia kodi ya majengo.
Ni kweli TRA kuna vitu inafeli. Ila wakiamua kuweka mifumo madhubuti ya kukusanya kodi hii ya zuio kwenye kodi za nyumba wanaweza kuongeza makusanyo sana tu. Hii kodi ya zuio kwenye kodi za nyumba/majengo kiuhalisia analipa mpangaji, akishalipa anampa cheti mwenye nyumba kuwa amemkata kodi na amepeleka TRA.
 
Hauna point hapa Chief.
Who is dalali? Simply ni agent wa kumuunganisha mteja na mwenye nyumba.
Sasa why adai kodi ya mwezi mmoja? Kwanini usiwepo utaratibu akalipwa na mwenye nyumba maana ndiye alompa kazi ya kusaka wateja?

Kwanini isiwepo means nzuri ya wenye nyumba kupata platform ya kutangaza nyumba zao zinazopangishwa na watu wakapata nafasi ya kuziona ma katika malipo hayo Serikali ikakusanya kodi?

Dalali kama ni muhimu kwanini formula yake inaumiza mpangaji pekee?
Wapangaji ndio huenda kuwaomba madalali wawatafutie nyumba za kupanga Sasa unataka mwenye nyumba amlipe kwa lipi?

Wewe unaenda kuomba huduma ya dalali halafu eti ohh mwenye nyumba amlipe kwa lipi wakati mkataba wa kikazi Ni wewe mtafuta nyumba ya kupanga mumeingia na dalali wako uliyemkuta kijiweni au popote kuwa nitafutie nyumba.Wewe ndio umlipe kwa hiyo huduma aliyokuwa na huyo dalali huyo ndie uende ukamripoti TRA

Ieleweke wazi contract ya kikazi ya kutafuta nyumba Ni yako wewe na dalali wako sio mwenye nyumba

Waziri alivyoliweka haliko sawa kisheria .Watu wanaenda wenyewe kwa madalali kwa hiari yao bila shuruti na kuingia mikataba nao ya kutafuta nyumba at a fee of course ambayo Ni Kodi ya mwezi mmoja
 
Ujumbe huu umfikie Waziri mwenye dhamana Mhe. Mwiguru Lameck Nchemba.
Wazo zuri sana hili
Halina chochote Hilo wazo ujinga mtupu

Mpangaji ndie humfuata dalali amtafutie nyumb
Kwa maneno mengine kazi ya kutafuta nyumba dalali hupewa na mpangaji ndio maana dalali aweza hangaika na kumuonyesha mpangaji nyumba kibao achague atakayo

Dalali hamfuati mpangaji Bali mpangaji ndie humfuata dalali kumuomba amsaidie kazi .Mwajiri wa Dalali Ni mpangaji aliyempa kazi ya kutafuta nyumba
 
Wenye nyumba wanalipa kodi,inaitwa With holding Tax,mpangaji huwa analipa kwa niaba ya mwenye nyumba,inaitwa with holding tax(kodi ya zuio),halafu wanakatana kwenye kodi.n

Nina zaidi ya miaka 15 ya kupangisha nyumba sijawahi kulipa hiyo kodi Kwenye biashara yangu ya upangishaji
Kodi ya Ardhi tu ndio wameanza kulipa wapangaji kupitia huu mfumo wa luku
 
udalali ni ajira labda waweke regulation dhidi yao sio TRA kuchukua jukumu vijana wengi wamejiajiri huku acheni mawazo potofu ukilipa ya mwezi ni fresh kwani unalipa tena
Ni wizi kwa sababu hawalipi kodi yoyote, na kama alivyosa Lukuvi mlipaji anatakiwa awe mwenye nyumba, lakini pia wasilipwe kodi ya mwezi...
 
Kutumia dalali hujalazimishwa katafute mwenyewe basi hujazuiwa pita kila nyumba gonga hodi uliza Kama wanapangisha Kama unaona kazi ya dalali haina maana
Mmeshawaroga wenye nyumba hata nyumba ikiwa empty na ukajua analazimisha uende kwa dalali...Kwa kifupi ni asilimia 0.001 ya nyumba zinapangishwa bila dalali. Kiasi kwamba inaondoa maana nzima ya udalali...

Chukueni tu asilimia kadhaa, mwezi mmoja jamani??
 
Umekaa sijui chumba ca kupanga, Sijui kea shemeji yako.

Umeshiba kiporo Cha makande unaanza kuwadis walotoka jasho kugharamikia usingizini wako kiazi wewe.

Yaan,
Ungejua Ni jins gani ujenzi unaumiza Wala usingethubutu kuongea Ayo maneno yako mbofu mbofu.

Jenga nyumba yako afu uje Tena na huu utopolo wako humu.
Wenye nyumba mnajikutaga mmemaliza maisha ila elfu 70 70 za wapangaji mnazitaka.

Yaani mnataka kufanya biashara bila running costs au sio? Maana kodi ya ardhi sijui majengo tunawalipia kwenye umeme
 
Back
Top Bottom