TRA yawataka wafanyabiashara kusajili stoo za kuhifadhia bidhaa

TRA yawataka wafanyabiashara kusajili stoo za kuhifadhia bidhaa

Mfanyabiashara asipolipa kodi faini kubwa kubwa lkn wafanyakazi wa serikali wanafanya ufisadi hakuna hatua yoyote inachukuliwa
Upo sahihi kabisa CAG katoa report ya uwizi wa mabillion hakuna kiongozi aliechukuliwa hatua, wanabanwa wafanyabiashara hela anaenda kufaidi mtu mmoja
 
Kuna baadhi ya watu wanajifanya machinga wanatoa mzigo store wanasambaza Kwa vijana shida ndipo ilipoanzia hapo
Hili swala Siasa ndo imeingilia kati.

TRA wanajikuta wako kati na hawajui nini wafanye.

Wasipokamata mizigo na kudai risiti hakika mapato yatashuka.

Dawa ni kila aliye kariakoo apewe EFD haijalishi nani uwe machinga au usiwe.

Wakifanya hivyo TRA wao wakae watulie waanze kamata mizigo ambayo haina risiti na kuitaifisha.

Watu watatoa risiti na kuomba.

Hizo stoo wanazopigia kelele kusajiliwa huko ndo madudu hufanyika.
KKOO mtu ana duka dogo ila mizigo inapitishwa Stoo
 
ukiona mtu anafanya biashara Tanzania, na biashara yake imedumu kwa zaidi ya miaka mitano (5) ujue huyo mtu ana roho ngumu sana. Bila hivyo ndani ya miaka mitano lazma uwe chali.

Ili uweze kufanya baishara Tanzania lazima uwe kama John Wick au Rocky Balboa. Uwe na roho ya paka, na uwe na vitu vifwatavyo

1. Focus
2. Commitment
3. Sheer will
4. Perserverance

Wengi wanakuwa na number 1 na 2 na hao ndio wengi wanaishia njiani. Tanzania bila sheer will and perseverance, hufanyi biashara. Angalia watu unaopambana nao ukiwa mfanyabiashara Tanzania

1. TRA
2. Fire
3. OSHA
4. Manispaa
5. Bwana afya
6. Serikali za mitaa na madiwani
7. TMDA
8. Polisi
9. Wafanyakazi wako (muda wote wanawaza kukuibia)
10. Majirani, ndugu, na marafiki zako
11. Wafanyabiashara ambao mko sekta moja na ni majirani.
12. Majambazi na vibaka
13. Mafuriko na majanga ya moto
14. Maagano ya ancestors wako

na mengineyo mengi mno. Hapo inabidi uwe mwamba ndio utoboe!
Ndio maana nchi hii mtu akiwa ana pesa anaonekana mchawi 😃
 
Naona kuna watu watakimbia bidhaa zao soon

Wanajua mizigo inahifadhiwa sehemu nyingine
Hivi bidhaa zimeingia nchini zimelipiwa kodi sasa mimi nimeweka kwenye store inawahusu nini?

Kama kawaida yao
Urahisi wa uhakiki.
 
Back
Top Bottom