Trafiki watatu wakamatwa wakipokea rushwa, mmoja atoroka

Trafiki watatu wakamatwa wakipokea rushwa, mmoja atoroka

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Polisi Trafiki watatu walikamtwa jana Alhamisi 30/11/2023 asubuhi eneo ambalo maafisa wa kupambana na rushwa walisema ni maarufu kwa kukusanyia rushwa kando ya Barabara ya Mai Mahiu katika makutano ya Karagita huko Naivasha, Kaunti ya Nakuru

Kulingana na Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa (EACC), afisa mwingine alikataa kujisalimisha na kukimbia huku akifyatua risasi kuzuia maafisa hao wa uchunguzi walokuwa wanamfuatilia. Hakuna majeruhi yaliyorekodiwa kutokana na majibizano hayo ya risasi, imesema shirika hilo.

Maafisa wa uchunguzi walipata ganda la risasi wakati wanawasafirisha matrafiki waliopokea rushwa kutoka Naivasha kwenye Kituo cha Polisi cha Tume hiyo kwaajili ya kutoa maelezo.


Afisa Trafiki watatu waliokamatawa wakipokea rushwa katika makao makuu ya EACC kwa ajili ya kuandikisha maelezo kabla ya kufikishwa mahakamani.

Citizens Digital
 
Wanawaonea tu hao maofisa. Hicho ni we call it a pet corruption, which is for survival.
 
Huku kwetu haiwezekanai hiyo maana wote walaji...
 
Polisi Trafiki watatu walikamtwa jana Alhamisi 30/11/2023 asubuhi eneo ambalo maafisa wa kupambana na rushwa walisema ni maarufu kwa kukusanyia rushwa kando ya Barabara ya Mai Mahiu katika makutano ya Karagita huko Naivasha, Kaunti ya Nakuru

Kulingana na Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa (EACC), afisa mwingine alikataa kujisalimisha na kukimbia huku akifyatua risasi kuzuia maafisa hao wa uchunguzi walokuwa wanamfuatilia. Hakuna majeruhi yaliyorekodiwa kutokana na majibizano hayo ya risasi, imesema shirika hilo.

Maafisa wa uchunguzi walipata ganda la risasi wakati wanawasafirisha matrafiki waliopokea rushwa kutoka Naivasha kwenye Kituo cha Polisi cha Tume hiyo kwaajili ya kutoa maelezo.

View attachment 2830107
Afisa Trafiki watatu waliokamatawa wakipokea rushwa katika makao makuu ya EACC kwa ajili ya kuandikisha maelezo kabla ya kufikishwa mahakamani.

Citizens Digital
Tamaa mbaya sana.

Kwa nini hawahawavua kwanza sare za Kijeshi? Pingu na gwanda😀
 
Nadhani Kenya inaweza ikawa inaongoza kwa rushwa Afrika mashariki, kati hadi kusini.
 
Back
Top Bottom