TRC: Seti ya Kwanza ya Treni ya Kisasa ya EMU, Vichwa Vitano vya Umeme na Mabehewa Matatu ya Abiria imewasili

TRC: Seti ya Kwanza ya Treni ya Kisasa ya EMU, Vichwa Vitano vya Umeme na Mabehewa Matatu ya Abiria imewasili

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Screenshot 2024-04-03 142119.png

Behewa.png
TAARIFA KWA UMMA
KUWASILI KWA SETI YA KWANZA YA TRENI YA KISASA EMU

Dar es Salaam, Tarehe 03 Aprili 2024
Shirika la Reli Tanzania TRC linautaarifu umma kuwa Seti ya kwanza ya treni ya kisasa ya EMU, vichwa vitano vya umeme na mabehewa matatu ya abiria yamewasili katika bandari ya Dar es Salaam.

Serikali kupitia TRC ilifanya manunuzi ya Seti kumi (10) za treni za kisasa zijulikanazo kama Electric Multiple Unit kutoka kwa watengenezaji kampuni ya Hyundai Rotem ya nchini Korea Kusini.

Seti moja ya EMU ina uwezo wa kubeba abiria 589 na kutembea kwa kasi wa kilomita 160 kwa saa. EMU ni treni iliyoundwa kwa teknolojia ya kisasa inayomuwezesha abiria kupata huduma muhimu ikiwemo huduma ya mtandao (Wi-FI), sehemu za kukaa watu wenye mahitaji maalum, mifumo ubaridi na kamera za usalama (CCTV Camera).

Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania imepokea jumla ya mabehewa 65 ya abiria, vichwa 9 vya umeme na Seti moja ya EMU. Seti zingine za EMU zitaendelea kuwasili kila mwezi hadi Oktoba 2024.

Kuwasili kwa vitendea kazi kunaifanya TRC kuwa tayari kuanza huduma za usafirishaji abiria katika reli ya kiwango cha kimataifa

Maendeleo ya Mradi wa SGR awamu ya kwanza yamefikia asilimia 98.90 kwa kipande cha Dar es salaam Morogoro (KM 300), asilimia 96.51 kipande cha Morogoro Makutupora, asilimia 13.98 kipande cha Makutupora - Tabora, asilimia 5.44 kipande cha Tabora - Isaka, asilimia 54.01 kipande cha Mwanza - Isaka.

Jamila Mbarouk
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano

Treniiii.png

Treniii.png

Teni.png

Trenii.png

Kichwa.png

WhatsApp Image 2024-04-03 at 13.55.33_a6e89b62.jpg
 
Usalama upi mkuu train inapita kwenye njia yake, kuna train huko China zinakwenda 500km/h
Hio 160 hata wenye gari private wanakanyaga wengine hadi 200km/h.
Mmmmmhh 500km/h yaan dar to shinyanga kwa dakika 60 au.....huyu mama akifanikiwa hz kitu zikafanya kazi na bei ikawa kama ile ya mabus au chini kidogo afu kwa spid hata ya 130km/h atakuwa kafanikiwa sana. Cha muhim ahakikishe sgr na bwawa la Mwal. nyerere yanafanya kazi kwa ubora hasa.
 
Usalama upi mkuu train inapita kwenye njia yake, kuna train huko China zinakwenda 500km/h
Hio 160 hata wenye gari private wanakanyaga wengine hadi 200km/h.
Reli za train kuanzia speed 300+ sio hizi, mkuu, zile gurudumu la chuma linajishika kwa kui lock reli.
Reli hizi sio za kisasa kwa ulimwengu ulipofikia, hizi rail wenzetu huko ngambo ni za miaka ya 50s-70s ndipo zilipamba moto, LAKINI RELI HIZI ZA SGR ZILIBUNIWA RASMI 12-NOV - 1922,WAKATI BABA WA TAIFA ANAZALIWA!.
Ilibuniwa na vijana saba, waliokuwa wakufundisha science, Butler University!, 1922.
 
mmmmmhh 500km/h yaan dar to shinyanga kwa dakika 60 au.....huyu mama akifanikiwa hz kitu zikafanya kazi na bei ikawa kama ile ya mabus au chini kidogo afu kwa spid hata ya 130km/h atakuwa kafanikiwa sana...cha muhim ahakikishe sgr na bwawa la mwal.nyerere yanafanya kazi kwa ubora hasa
Kila kitu pongezi kwa mama.
 
Walau baadhi ya vichwa vinavyoletwa safari hii vinafanana kidogo na treni halisi za umeme za wenzetu.

Ila siyo kile kichwa cha majaribio kutoka Dar kwenda Morogoro ile siku ya majaribio!
Maana hakina tofauti na ile treni kimeo ya dizeli ya Kenya, waliyobambikwa na Wachina. Halafu wakaambiwa eti ni SGR!!
 
Chipsi ndogo, kuku nusu. Mbona vichwa ni vingi kuliko mabehewa?
Umesahau hivyo vichwa vitahitaji matengenezo, bado kuna matatizo ya kiufundi yanaweza kujitokeza! nk. Kwa hiyo ni sahihi kabisa vikiletwa vya kutosha.
 
Back
Top Bottom