TRC: Seti ya Kwanza ya Treni ya Kisasa ya EMU, Vichwa Vitano vya Umeme na Mabehewa Matatu ya Abiria imewasili

TRC: Seti ya Kwanza ya Treni ya Kisasa ya EMU, Vichwa Vitano vya Umeme na Mabehewa Matatu ya Abiria imewasili

Kwamba seti ya kwanza ya vichwa vitano vya treni na mabehewa matatu ya abiria yamewasili na kwamba seti moja ina uwezo wa kubeba abiria 589. Ina maana hiyo seti moja iliyofika yenye mabehewa matatu ndiyo ina uwezo wa kubeba idadi yote hiyo ya abiria 589? Mbona ni idadi kubwa sana au mimi ndiye sijaelewa.
 
TAARIFA KWA UMMA
KUWASILI KWA SETI YA KWANZA YA TRENI YA KISASA EMU

Dar es Salaam, Tarehe 03 Aprili 2024
Shirika la Reli Tanzania TRC linautaarifu umma kuwa Seti ya kwanza ya treni ya kisasa ya EMU, vichwa vitano vya umeme na mabehewa matatu ya abiria yamewasili katika bandari ya Dar es Salaam.

Serikali kupitia TRC ilifanya manunuzi ya Seti kumi (10) za treni za kisasa zijulikanazo kama Electric Multiple Unit kutoka kwa watengenezaji kampuni ya Hyundai Rotem ya nchini Korea Kusini.

Seti moja ya EMU ina uwezo wa kubeba abiria 589 na kutembea kwa kasi wa kilomita 160 kwa saa. EMU ni treni iliyoundwa kwa teknolojia ya kisasa inayomuwezesha abiria kupata huduma muhimu ikiwemo huduma ya mtandao (Wi-FI), sehemu za kukaa watu wenye mahitaji maalum, mifumo ubaridi na kamera za usalama (CCTV Camera).

Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania imepokea jumla ya mabehewa 65 ya abiria, vichwa 9 vya umeme na Seti moja ya EMU. Seti zingine za EMU zitaendelea kuwasili kila mwezi hadi Oktoba 2024.

Kuwasili kwa vitendea kazi kunaifanya TRC kuwa tayari kuanza huduma za usafirishaji abiria katika reli ya kiwango cha kimataifa

Maendeleo ya Mradi wa SGR awamu ya kwanza yamefikia asilimia 98.90 kwa kipande cha Dar es salaam Morogoro (KM 300), asilimia 96.51 kipande cha Morogoro Makutupora, asilimia 13.98 kipande cha Makutupora - Tabora, asilimia 5.44 kipande cha Tabora - Isaka, asilimia 54.01 kipande cha Mwanza - Isaka.

Rangi za vichwa na mabehewa hazi-reflect alama yoyote ya Tanzania, wameshindwa hata kupaka rangi mojawapo iliyopo kwenye bendera ya taifa , nembo ya taifa au hata mlima Kilimanjaro.

Vv
 
Ile treni ya kisasa ya Umeme aliyotuahidi Shujaa Magufuli akiiita Mjusi imefikishwa bandarini DSM

Vimewasili vichwa 5 Vya Umeme na mabehewa 3 ya Abiria

Source: Ayo TV
 
Mmmmmhh 500km/h yaan dar to shinyanga kwa dakika 60 au.....huyu mama akifanikiwa hz kitu zikafanya kazi na bei ikawa kama ile ya mabus au chini kidogo afu kwa spid hata ya 130km/h atakuwa kafanikiwa sana. Cha muhim ahakikishe sgr na bwawa la Mwal. nyerere yanafanya kazi kwa ubora hasa.
Kwa nauli haiwezi kuwa Sawa na Mabasi na nauli itakuwa juu kuliko basi kaa mkao wa kula
 
Sawa hongereni kwa kuleta treni.

Ila sasa huu umeme ambao bwawa likijaa maji wanazima mitambo na bwawa likikosa maji wanazima pia tutafika kweli??
 
TAARIFA KWA UMMA
KUWASILI KWA SETI YA KWANZA YA TRENI YA KISASA EMU

Dar es Salaam, Tarehe 03 Aprili 2024
Shirika la Reli Tanzania TRC linautaarifu umma kuwa Seti ya kwanza ya treni ya kisasa ya EMU, vichwa vitano vya umeme na mabehewa matatu ya abiria yamewasili katika bandari ya Dar es Salaam.

Serikali kupitia TRC ilifanya manunuzi ya Seti kumi (10) za treni za kisasa zijulikanazo kama Electric Multiple Unit kutoka kwa watengenezaji kampuni ya Hyundai Rotem ya nchini Korea Kusini.

Seti moja ya EMU ina uwezo wa kubeba abiria 589 na kutembea kwa kasi wa kilomita 160 kwa saa. EMU ni treni iliyoundwa kwa teknolojia ya kisasa inayomuwezesha abiria kupata huduma muhimu ikiwemo huduma ya mtandao (Wi-FI), sehemu za kukaa watu wenye mahitaji maalum, mifumo ubaridi na kamera za usalama (CCTV Camera).

Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania imepokea jumla ya mabehewa 65 ya abiria, vichwa 9 vya umeme na Seti moja ya EMU. Seti zingine za EMU zitaendelea kuwasili kila mwezi hadi Oktoba 2024.

Kuwasili kwa vitendea kazi kunaifanya TRC kuwa tayari kuanza huduma za usafirishaji abiria katika reli ya kiwango cha kimataifa

Maendeleo ya Mradi wa SGR awamu ya kwanza yamefikia asilimia 98.90 kwa kipande cha Dar es salaam Morogoro (KM 300), asilimia 96.51 kipande cha Morogoro Makutupora, asilimia 13.98 kipande cha Makutupora - Tabora, asilimia 5.44 kipande cha Tabora - Isaka, asilimia 54.01 kipande cha Mwanza - Isaka.

Serikali kazi yake iwe kujenga reli, treni zinunuliwe na kuendeshwa na makampuni na watu binafsi ndio tutaona ufanisi
 
Mmmmmhh 500km/h yaan dar to shinyanga kwa dakika 60 au.....huyu mama akifanikiwa hz kitu zikafanya kazi na bei ikawa kama ile ya mabus au chini kidogo afu kwa spid hata ya 130km/h atakuwa kafanikiwa sana. Cha muhim ahakikishe sgr na bwawa la Mwal. nyerere yanafanya kazi kwa ubora hasa.
Wacha basi na wewe! Dar to Shy kilomita 500?
 
Back
Top Bottom