TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete

TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
sgr.jpg


TAARIFA KWA UMMA
HITILAFU YA UMEME KATI YA KILOSA NA KIDETE

Dar es Salaam, Tarehe 31 Julai 2024

Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete na kusababisha treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) siku ya tarehe 30 Julai 2024.

Pia soma: Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme

Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system). Hitilafu ilisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku.

Mafundi wa TRC walifanikiwa kutatua changamoto na kurejesha umeme saa 6:30 usiku na treni kuendelea na safari kuelekea Dodoma, na kuwasili Dodoma majira ya saa 7:57 usiku.
Shirika la Reli Tanzania linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
 
Kumekucha!
Wameisha anza hujuma zao. Wanafikiri watanzania hawana akili na hawakumbuki kauli zao wanazoziongea mbele ya waandishi wa habari.

Tuliambiwa tren zetu zina mifumo miwili,
1) umeme
2) mafuta
Ukikatika umeme injini inapiga kazi kwa mafuta.

Na walisema haitakuja kutokea umeme ukakosekana kwenye tren hiyo. Ukikosekana maana yake inchi nzima iko gizani.

Sasa tunawauliza kwa nini wasitumie diesel baada ya umeme kukatwa?
Na je wamewalipa fidia abiria kwa hasara waliyoipata?

Hawa wanahujumu mradi kwa makusudi.
 
Walisema umeme ukikatika Kuna Kuna umeme wa ziada hii nchi ni hovyo sana 😂😁😁

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete ambayo imesababisha Treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inafanya safari zake kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea jijini Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) Julai 30.2024
20240731_081927.jpg
 
Kumekucha!
Wameisha anza hujuma zao. Wanafikiri watanzania hawana akili na hawakumbuki kauli zao wanazoziongea mbele ya waandishi wa habari.

Tuliambiwa tren zetu zina mifumo miwili,
1) umeme
2) mafuta
Ukikatika umeme injini inapiga kazi kwa mafuta.

Na walisema haitakuja kutokea umeme ukakosekana kwenye tren hiyo. Ukikosekana maana yake inchi nzima iko gizani.

Sasa tunawauliza kwa nini wasitumie diesel baada ya umeme kukatwa?
Na je wamewalipa fidia abiria kwa hasara waliyoipata?

Hawa wanahujumu mradi kwa makusudi.
Nani alipe fidia kwa mafala wa Kitanzania?
 
Back
Top Bottom