Tetesi: Treni iliyokuwa iondoke Dsm kuelekea Zambia imeshindwa kuanza safari sababu ya kutokuwa na diesel.

Tetesi: Treni iliyokuwa iondoke Dsm kuelekea Zambia imeshindwa kuanza safari sababu ya kutokuwa na diesel.

Treni iliyotarajiwa kuondoka kutoka Dar es Salaam kwenda Kapiri Mposhi, Zambia, kwa saa 9:50 jioni, bado haijaanza safari hadi saa 2 usiku, huku sababu ya kuchelewa kwao ikiwa bado haijatolewa rasmi. Kwa mujibu wa tetesi, kuchelewa huko kunaweza kuhusishwa na ukosefu wa mafuta (diesel) kwa ajili ya treni hiyo. Hali hii inaashiria kuwa kuna uwezekano mkubwa wa safari hiyo kushindwa kufanyika leo.

Ni muhimu sana kuwa uongozi wa shirika linalohusika na usafiri wa treni utoe taarifa za wakati kwa abiria wanapotokea changamoto zozote zilizo kinyume na taratibu za kawaida. Hii itasaidia abiria kujipanga na kuepusha hali ya kusubiri bila kujua hatma yao.

Tunatoa wito kwa Serikali kuingilia kati na kuhakikisha kuwa abiria wanapata msaada unaohitajika. Mimi nikiwa mmoja wa abiria wanaosubiri, naona ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa hali kama hizi hazirudiwi tena na kwamba huduma za umma zinakuwa na uwajibikaji zaidi.
"naona ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa hali kama hizi hazirudiwi tena"! Mimi abiria niko nyumbani kwangu nitawezaje kununua hiyo dizeli ili tuweze kusafiri kwa wakati.
 
Treni iliyotarajiwa kuondoka kutoka Dar es Salaam kwenda Kapiri Mposhi, Zambia, kwa saa 9:50 jioni, bado haijaanza safari hadi saa 2 usiku, huku sababu ya kuchelewa kwao ikiwa bado haijatolewa rasmi. Kwa mujibu wa tetesi, kuchelewa huko kunaweza kuhusishwa na ukosefu wa mafuta (diesel) kwa ajili ya treni hiyo. Hali hii inaashiria kuwa kuna uwezekano mkubwa wa safari hiyo kushindwa kufanyika leo.

Ni muhimu sana kuwa uongozi wa shirika linalohusika na usafiri wa treni utoe taarifa za wakati kwa abiria wanapotokea changamoto zozote zilizo kinyume na taratibu za kawaida. Hii itasaidia abiria kujipanga na kuepusha hali ya kusubiri bila kujua hatma yao.

Tunatoa wito kwa Serikali kuingilia kati na kuhakikisha kuwa abiria wanapata msaada unaohitajika. Mimi nikiwa mmoja wa abiria wanaosubiri, naona ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa hali kama hizi hazirudiwi tena na kwamba huduma za umma zinakuwa na uwajibikaji zaidi.
 

Attachments

  • images (93).jpeg
    images (93).jpeg
    38.2 KB · Views: 2
Back
Top Bottom