KERO Treni ya Dar-Tanga-Arusha imekwama, wanaohusika watoe mwongozo wa nini kinaendelea

KERO Treni ya Dar-Tanga-Arusha imekwama, wanaohusika watoe mwongozo wa nini kinaendelea

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
photo_2024-05-25_00-55-41.jpg

photo_2024-05-25_00-55-40.jpg

photo_2024-05-25_00-55-37.jpg
Ni muda wa miezi kadhaa sasa usafiri wa Treni za mizigo na abiria kati ya Mkoa wa Dar es Salaam, Tanga na Arusha umekwama kutokana na sababu kuu mbili.

Sababu ya kwanza ambayo nimeisikia na imekuwa ikitajwa ni kuwa reli ilikuwa inafanyiwa marekebisho ya hapa na pale.

Pili baada ya kukamilika marekebisho hayo, treni ilifanya kazi siku mbili, kilichofuata baada ya kunyesha kwa mvua mfululizo Bwawa la nyumba ya Mungu lililopo Moshi Mkoani kilimanjaro likajaa maji na hivyo kusababisha maji kutiririka na kujaa katika njia za reli.

Hali hiyo ikachangia usafiri wa Treni usitishwe kwa muda hadi hali itakapokaa ndipo usafiri wa treni utarudi tena.

Baadhi ya sisi abiria wa Arusha, Moshi na Tanga ambao tunatumia usafiri huo tumefika mara kadhaa zilipo ofisi za reli kuulizia ili kupata taratibu za safari lakini hakuna majibu ya kueleweka.

Kibaya zaidi hata tunapoenda kuulizia palepale kwenue ofisi zao, wahudumu wao nao hawajui kama ilivyo kwa abiria wengine, wanaenda ofisini wanakaa siku nzima bila kazi, wanasaini kisha wanarudi home na mwisho wa mwezi mshahara unaingia kama kawaida.

Naomba kama ni Serikali, mamlaka inayohusika kutoa taarifa juu ya nini kinachoendelea, kwani Treni mbali na kubeba abiria tunaitumia kusafirisha mizigo yetu mizito na mikubwa, kwa sasa tunalazimika kutumia njia mbadala wakati tumeshazoea Treni.

============

FB_IMG_1601399026602.jpg

Ratiba ya awali ilivyokuwa
Majibu ya TRC ~ TRC: Huduma ya Treni ya Arusha - Dar imerejea, ilisimama kutokana na sehemu ya njia ya reli kujaa maji
 
Watanzania watuwezi kuendesha chochote wenyewe. Tu wajinga wa kutupwa.
 
Route ya huko subirini Dec
Itakaa sawa 😄

Ova
 
Watanzania watuwezi kuendesha chochote wenyewe. Tu wajinga wa kutupwa.
Sema serikali ya CCM haiwezi kusimamia chochote na kukiendesha, imejaa wezi na wajinga.

Kama huamini hilo, embu jiulize, mmiliki wa Precious Air alikuwa ni mtanzania (kwa sasa ni marehemu) na kwa miaka karibu 30 ameweza kuendesha kampuni ya ndege kwa faida hapa Tz. Hali ni hiyo hiyo kwa wamiliki wa Azam marine, Abood bus service, Shabiby, Kilimanjaro bus nk. Kwanini wao wanaweza kwa mitaji yao halafu serikali yenye kumiliki kodi za watanzania inashindwaje kuendesha taasisi zake hata kwa kutoa huduma tu?
 
Nakaziaaaaa

Sahv tulichobakia kuweza ni kukata mauno tu..umbea udaku

Ova
Siyo sasa hivi tu, tulishindwa kujiendesha toka wakati wa Nyerere.

Tulifanya makosa ya msingi mwaka 1967 tulipowataifisha wenye viwanda na mashamba na kujimwambafai kuwa tunaweza wenyewe. Walipoondoka tu na Tanganyika ikafa kifo cha mende.

Bado tu wajinga na hatuwezzi kujiendesha wenyewe. Inabidi mpaka Watanzania wenyewe tuwe na viwango ndipo tutazweza kuiendesha.

Siku Watanzania watakapoanza kula chakula na kuwacha kusema kitoweo (Ugali na wali) kuwa ni chakula ndipo tutakapoanza kutia akili.

Nashauri sana serikali ielimishe na ipeleke nguvu kubwa kwenye mlo wa siku wa Mtanzania, chakula kiwe, Kuku, mayai, nyama, samaki, mboga, maziwa, ugali na wali viwe ni vitoweo.

Hapo ndipo tutaanza kujenga akili ya vizazi vyetu.
 
Siyo sasa hivi tu, tuishindwa kujiendesha toka wakati wa Nyerere.

Tulifanya makosa ya msingi mwaka 1967 tulipowataifisha wenye viwanda na mashamba na kujimwambafai kuwa tunaweza wenyewe. Walipoondoka tu na Tanganyika ikafa kifo cha mende.

Bado tu wajinga na hatuwezzi kujiendesha wenyewe. Inabidi mpaka Watanzania wenyewe tuwe na viwango ndipo tutazweza kuiendesha.

Siku Watanzania watakapoanza kula chakula na kuwacha kusema kitoweo (Ugali na wali) kuwa ni chakula ndipo tutakapoanza kutia akili.

Nashauri sana serikali ielimishe na ipeleke nguvu kubwa kwenye mlo wa siku wa Mtanzania, chakula kiwe, Kuku, mayai, nyama, samaki, mboga, maziwa, ugali na wali viwe ni vitoweo.

Hapo ndipo tutaanza kujenga akili ya vizazi vyetu.
Comment bora kabisa
Dada yangu kipenzi


Ova
 
Sema serikali ya CCM haiwezi kusimamia chochote na kukiendesha, imejaa wezi na wajinga.

Kama huamini hilo, embu jiulize, mmiliki wa Precious Air alikuwa ni mtanzania (kwa sasa ni marehemu) na kwa miaka karibu 30 ameweza kuendesha kampuni ya ndege kwa faida hapa Tz. Hali ni hiyo hiyo kwa wamiliki wa Azam marine, Abood bus service, Shabiby, Kilimanjaro bus nk. Kwanini wao wanaweza kwa mitaji yao halafu serikali yenye kumiliki kodi za watanzania inashindwaje kuendesha taasisi zake hata kwa kutoa huduma tu?
Hakuna cha serikali ya CCm wala nyingine yeyote ambayo itafanikisha kuondoa ujinga wa Mtanzania kama bado lishe yetu ni ugali na wali.

Ugali na wali viwe kitoweo. Chakula bora ni kuku, maytai, samaki, nyama za aina yote, kasoro nguruwe, mboga.

Siku ukipika chakula au ukiagiza chakula hoteli na bila kusema nipeni nyama, au samaki au kuku. Ugali na wali ukabaki kuwa kitoweo tena cha bure ujuwe bado ujinga haujatutoka.
 
Watanzania watuwezi kuendesha chochote wenyewe. Tu wajinga wa kutupwa.
Mbona wakati wa Magufuli tuliweza kujiendesha? Si useme tu ukweli kuwa Samia ameshindwa?


Mtanikumbuka kwa mazuri na si kwa mabaya --- Magufuli
 
Ni muda wa miezi kadhaa sasa usafiri wa Treni za mizigo na abiria kati ya Mkoa wa Dar es Salaam, Tanga na Arusha umekwama kutokana na sababu kuu mbili.

Sababu ya kwanza ambayo nimeisikia na imekuwa ikitajwa ni kuwa reli ilikuwa inafanyiwa marekebisho ya hapa na pale.

Pili baada ya kukamilika marekebisho hayo, treni ilifanya kazi siku mbili, kilichofuata baada ya kunyesha kwa mvua mfululizo Bwawa la nyumba ya Mungu lililopo Moshi Mkoani kilimanjaro likajaa maji na hivyo kusababisha maji kutiririka na kujaa katika njia za reli.

Hali hiyo ikachangia usafiri wa Treni usitishwe kwa muda hadi hali itakapokaa ndipo usafiri wa treni utarudi tena.

Baadhi ya sisi abiria wa Arusha, Moshi na Tanga ambao tunatumia usafiri huo tumefika mara kadhaa zilipo ofisi za reli kuulizia ili kupata taratibu za safari lakini hakuna majibu ya kueleweka.

Kibaya zaidi hata tunapoenda kuulizia palepale kwenue ofisi zao, wahudumu wao nao hawajui kama ilivyo kwa abiria wengine, wanaenda ofisini wanakaa siku nzima bila kazi, wanasaini kisha wanarudi home na mwisho wa mwezi mshahara unaingia kama kawaida.

Naomba kama ni Serikali, mamlaka inayohusika kutoa taarifa juu ya nini kinachoendelea, kwani Treni mbali na kubeba abiria tunaitumia kusafirisha mizigo yetu mizito na mikubwa, kwa sasa tunalazimika kutumia njia mbadala wakati tumeshazoea Treni.

============

View attachment 2998798
Ratiba ya awali ilivyokuwa
Kadogosa yuko Kwenye siasa siku hizi
Anaenda na upepo wa Rais aliyepo Kwa kipindi hicho. Wao wanafikiri SGR Ndio kila kitu sasa kuona ina boost credit za Shangazi
Wanatengeneza Hiki wanaua hizi Sasa huko Sio kujua kiuchumi. 1+1 = 2 Kadogosa yeye anafanya 1+1-1 Ili kupunguza stress
Anyway Ndio wasomi wetu
Na Ndio Serikalini yetu
Tanzania ni yetu
Kadogosa ni wetu
Hili nalo Mkaliangalie
 
Ndugu wadau kiukweli nibora relli hii kubinafsishwa labda itafanya kazi wiki Ile nyingine sikumbuki tarehe nilienda ofisi za treni Moshi ilikua jumatano nikaikuta treni imepaki nikauliza utaratibu nikajibiwa maeneo kabla ya same maji yamejaa ambayo yanatoka nyumba ya mungu lakini wanafanya ukarabati kuyaondoa maji ili treni iendelee na safari wakaniambia jumatatu itakua tayari lakini jumatatu nilipoenda tena niliambiwa hata wao hawajapewa taarifa kama tayari au bado sasa kama uwezo wakuendesha hawana kwann serikali isiachie njia reli ikawa biashara huru ya ushindani ili tusipate tabu watumiaji
 
Mbona wakati wa Magufuli tuliweza kujiendesha? Si useme tu ukweli kuwa Samia ameshindwa?


Mtanikumbuka kwa mazuri na si kwa mabaya --- Magufuli
Reli umeipokea toka Muingereza alipotoka miaka zaidi ya 60 iliyopita unaipima kwa kuendeshwa mwaka mmoja?
 
Back
Top Bottom