DOKEZO Treni ya SGR Dar-Moro inasafiri na nafasi wazi zaidi ya nusu wakati awali tiketi zilikuwa zinaisha siku 1 kabla; Tatizo ni nini? Ushahidi huu hapa

DOKEZO Treni ya SGR Dar-Moro inasafiri na nafasi wazi zaidi ya nusu wakati awali tiketi zilikuwa zinaisha siku 1 kabla; Tatizo ni nini? Ushahidi huu hapa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest

Habari wanabodi

Hapo awali treni ya SGR Morogoro - Dar inayochukua abiria takribani 900 ilikuwa inajaa siku 1 au 2 kabla ya safari. Ukiingia mtandaoni hupati tiketi.

Utafiti wangu nilioufanya kwa siku kadhaa kupitia mfumo wa mauzo ya tiketi na kuuhitimisha tarehe 25 Sept 2024, dakika 25 kabla safari (ikumbukwe zikibaki dk 20 kabla ya safari zoezi la ukataji tiketi hufungwa), nimebaini yafuatayo;

1. Ukijaribu kukata tiketi ya Dar-Moro, unakuta kati ya siti 900, siti zaidi ya 500 ziko wazi kutoka Dar kwenda Moro. Hii ina maana kwamba abiria takribani 400 kasoro ndio watakao anzia safari Dar. Hii haijalishi watashukia wapi.

2. TRC wanaweza sema wengine watapandia vituo vya njiani, lakini dakika hiyo hiyo ukirudia kukata ticket ya Soga-Moro unakuta nafasi zaidi karibia 600 kasoro. Hii maana yake ni kwamba; wanaopandia njiani si wengi zaidi ya wanaoshukia njiani, hivyo treni inatoka Dar hadi Moro ikiwa na abiria pungufu zaidi nusu.

Hali hii inatokea pia kwa safari za Moro-Dar.

Kwa kuzingatia hilo tutafakari yafuatayo kwa pamoja;
1. Abiria hawafurahii huduma hivyo wameisusa treni?
2. Mwanzo ilikuwa ni ushamba tu kwa hiyo hata asiyekuwa na safari aliiunda ghafla?
3. Ni hujuma ya abiria kukata tiketi za njiani huku wanafika mwisho wa safari?
4. Je, ukiingia ndani ya treni viti viko wazi kweli kusadifu mauzo hafifu ya tiketi au ndio tiketi haziuziki ila treni imejaa?
5. Kuna hujuma ya baadhi watumishi wa TRC kuingiza abiria bila ticket?

Ikumbukwe kuwa, mwezi Agosti 2024 mwanaJF aliripoti kuhusu ulanguzi wa tiketi, TRC wakaweka utaratibu wa vitambulisho. Ukaguzi wa vitambulisho wakati wa kuingia kwenye treni
umesaidia sana.

Baadae ikaripotiwa na TAKUKURU Morogoro kuwa baadhi ya abiria wanakata tiketi za Pugu huku wanakwenda Moro. TRC walitoa taarifa kuwa wameanza ukaguzi wa kieletroniki mwisho wa safari, kwamba abiria aliyepitiliza kituo, geti la kutokea stesheni halitofunguka. Hili si kweli, hadi sasa hilo halifanyiki. Abiria hukaguliwa mwanzo tu, hata ndani ya treni wakati wa safari hakuna ukaguzi wowote. Sijui kwanini TRC waliamua kudanganya.

Mapendekezo:
1. TRC na vyombo husika wachunguze kama kuna hujuma au abiria wamesusa. Kama ni hilo la pili waangalie abiria wanakwazwa na nini. Kuwe na platform rahisi ya kukusanya maoni ya abiria ikiwemo
kitufe cha maoni kwenye website ya booking.

2. Kama mifumo ya ukaguzi ya mageti ya kutokea stesheni haifanyi kazi, basi wakague mara kadhaa manually ndani ya treni. Mhudumu kila baada ya kituo kimoja au viwili akague abiria wake kama wana tiketi za kuwafanya wawepo walipo.

Hii tusione kama ni usumbufu kwa abiria, ndio jamii tuliyonayo inahitaji hilo. Bado tujajifunza ustaarabu polepole.

Nawasilisha

Dar-Moro



Moro-Dar

 

Attachments

  • video_20240926_094907_edit.mp4
    14 MB
Kuna siku nilitaka kumkatia mtu anaenda Dodoma akasema wale hawana uhakika kata bus tu
Abiria hupenda uhakika sana wa safari yake (tiketi) kama hana uhakika wa kupata tiketi basi hawezi kata
 
Saa 12 asubuhi
Saa 3:30 asubuhi
Saa 10:30 jioni
Saa 12:40 jioni
Sidhani kama kuna abiria wa kujaza mabehewa yote Kwa safari hizo nne Kwa kila siku
Zaidi ya abiria 3000 Kwa siku , sio rahisi
Abiria watakua wanapungua taratibu kadri siku zinavyokwenda
 
Kwa utafiti wako huo mkuu unaishauri serikali wasiuendeleze kufikaa mikoa mingene huu mradi wa tren Bali hzo pesa za miradi tufanyie nn Kwa Maoni yako
 
Waliokuwa wanajaza mwanzo n wale kipya kinyemi. Sasa tumebaki abiria halisi.
 
Treni inajaa sana weekend. Alhamisi hadi jumapili. Kuanzia jumatatu hadi jumatano ni kawaida tu.
Mwanzo ilikuwa inajaa kila siku kwasababu ya upya tu. Haiwezi kujaa kila siku.
 
View attachment 3107120
Habari wanabodi

Hapo awali treni ya SGR Morogoro - Dar inayochukua abiria takribani 900 ilikuwa inajaa siku 1 au 2 kabla ya safari. Ukiingia mtandaoni hupati tiketi.

Utafiti wangu nilioufanya kwa siku kadhaa kupitia mfumo wa mauzo ya tiketi na kuuhitimisha tarehe 25 Sept 2024, dakika 25 kabla safari (ikumbukwe zikibaki dk 20 kabla ya safari zoezi la ukataji tiketi hufungwa), nimebaini yafuatayo;

1. Ukijaribu kukata tiketi ya Dar-Moro, unakuta kati ya siti 900, siti zaidi ya 500 ziko wazi kutoka Dar kwenda Moro. Hii ina maana kwamba abiria takribani 400 kasoro ndio watakao anzia safari Dar. Hii haijalishi watashukia wapi.

2. TRC wanaweza sema wengine watapandia vituo vya njiani, lakini dakika hiyo hiyo ukirudia kukata ticket ya Soga-Moro unakuta nafasi zaidi karibia 600 kasoro. Hii maana yake ni kwamba; wanaopandia njiani si wengi zaidi ya wanaoshukia njiani, hivyo treni inatoka Dar hadi Moro ikiwa na abiria pungufu zaidi nusu.

Hali hii inatokea pia kwa safari za Moro-Dar.

Kwa kuzingatia hilo tutafakari yafuatayo kwa pamoja;
1. Abiria hawafurahii huduma hivyo wameisusa treni?
2. Mwanzo ilikuwa ni ushamba tu kwa hiyo hata asiyekuwa na safari aliiunda ghafla?
3. Ni hujuma ya abiria kukata tiketi za njiani huku wanafika mwisho wa safari?
4. Je, ukiingia ndani ya treni viti viko wazi kweli kusadifu mauzo hafifu ya tiketi au ndio tiketi haziuziki ila treni imejaa?
5. Kuna hujuma ya baadhi watumishi wa TRC kuingiza abiria bila ticket?

Ikumbukwe kuwa, mwezi Agosti 2024 mwanaJF aliripoti kuhusu ulanguzi wa tiketi, TRC wakaweka utaratibu wa vitambulisho. Ukaguzi wa vitambulisho wakati wa kuingia kwenye treni
umesaidia sana.

Baadae ikaripotiwa na TAKUKURU Morogoro kuwa baadhi ya abiria wanakata tiketi za Pugu huku wanakwenda Moro. TRC walitoa taarifa kuwa wameanza ukaguzi wa kieletroniki mwisho wa safari, kwamba abiria aliyepitiliza kituo, geti la kutokea stesheni halitofunguka. Hili si kweli, hadi sasa hilo halifanyiki. Abiria hukaguliwa mwanzo tu, hata ndani ya treni wakati wa safari hakuna ukaguzi wowote. Sijui kwanini TRC waliamua kudanganya.

Mapendekezo:
1. TRC na vyombo husika wachunguze kama kuna hujuma au abiria wamesusa. Kama ni hilo la pili waangalie abiria wanakwazwa na nini. Kuwe na platform rahisi ya kukusanya maoni ya abiria ikiwemo
kitufe cha maoni kwenye website ya booking.

2. Kama mifumo ya ukaguzi ya mageti ya kutokea stesheni haifanyi kazi, basi wakague mara kadhaa manually ndani ya treni. Mhudumu kila baada ya kituo kimoja au viwili akague abiria wake kama wana tiketi za kuwafanya wawepo walipo.

Hii tusione kama ni usumbufu kwa abiria, ndio jamii tuliyonayo inahitaji hilo. Bado tujajifunza ustaarabu polepole.

Nawasilisha

Dar-Moro
View attachment 3107120


Moro-Dar

View attachment 3107120

Mtu wewe ni mzalendo wa kweli. Umeandika kwa uchungu sana. TRC fanyieni kazi maoni haya.
 
Nakubaliana na no.2
Wengi walipanda kutoa ushamba! Baada ya hapo wanaona ni kawaida tu.
Mwisho tutasema ni hujuma za akina Abood!
 
Back
Top Bottom