DOKEZO Treni ya SGR ya Dar - Dodoma imesimama Morogoro kwa Saa Mbili, kisha imezima tena kabla ya kufika Dodoma

DOKEZO Treni ya SGR ya Dar - Dodoma imesimama Morogoro kwa Saa Mbili, kisha imezima tena kabla ya kufika Dodoma

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
yupo busy kuhonga mbowe hela wakat nchi ina vitu vya msingi havipo sawa.hopeless woman
 
Mimi ni mmoja wa Wasafiri wa Treni ya SGR, nilikata tiketi ya kuondoka asubuhi ya Saa 12:00 leo Januari 8, 2025 lakini ulipofika muda huo safari ikasogezwa mbele kwa nusu saa.

Safari yangu ni kuelekea Dodoma, matarajia ya kuwasili yalikuwa Saa 3:30 asubuhi baada ya hapo ilikuwa nielekee kwenye kikao sehemu fulani ambacho kilipangwa kuanza Saan ne kamili asubuhi.

Safari ilianza vizuri tu na kwa mwendo wa kasi, ilipofika maeneo fulani ambayo siyakumbuki kasi ikaanza kupungua.

Tulipofika Morogoro tukasimama hapo muda mrefu, hadi muda huu saa tano bado tupo Morogoro na hatujui nini kinaendelea.

Safari iliyotarajiwa kufikia tamati saa tatu na nusu, hadi sasa nis aa tano bado tupo Morogoro.

===============

UPDATES...
IMESIMAMA TENA KABLA YA KUFIKA DODOMA

Ilipofika Saa tano na dakika 40 flani hivi Treni ikawashwa tukaendelea na safari, muda wa saa saba na nusu Mchana kabla ya kufika Dodoma, mzigo umezima tena, hatujajua hapa ni wapi ila ndio tunasikilizia kujua nini kinaendelea.

Abiria wote tumeambiwa tushuke kwenye Treni, hatujui nini kinachoendelea.

Imagine niliamka saa tisa ili niwahi Treni ya Saa kumi na mbili na saa tatu na nusu niwe nimefika, mpaka sasa saa saba na nusu mchana hatujafika Dodoma, si bora ningepanda basi nijue moja.

TUNASHUKA, TUNAPANDISHWA KWENYE MABASI
Abiria wote baada ya kuambiwa tushuke, tumeambiwa kuna mabasi ambayo yanakuja kutuchukua hapa tulipo kutupeleka Dodoma Mjini kwa kuwa inaonekana kuna kama Kilometa zaidi ya 20 kabla ya kufika Dodoma.
Aisee poleni sana.imagine kilikuwa ni kikao cha tenda ndiyo utakuwa umeikosa.Kwenye ndege ikitokea hivyo huwa wanawanunulia chakula pia.

Naamini bado wanafanya testing,itatengemaa tuu.maana nadhani pia hata lqst wiki watu walikalishwa Kilosa for more than 3 hrs na hiyo hiyo SGR
 
Mkuu hiyo train ni Used siyo mpya ukiona vifaa used vinakuja Nchini uko vinapotoka vinakua vimeshapitwa na muda, ni sawa ununue Nokia Lumia used.
Acha stori za vijiweni. Treni zinazofanya kazi zote mpya. Zimetengenezwa South Korea. Mara nyingi hitilafu wala sio treni yenyewe.
 
Ukizingatia awaruhusu msosi, mchana itawakuta hapohapo.

Ndio maana mimi huwa napanda na vitumbua vyangu nakula sina habari na mtu.
Pale walipo ni porini kuna matunda mengi sana wakati huu pamoja na wadudu waliwao. Si vibaya kuishi maisha ya Kihazabe for a day.
 
Mimi ni mmoja wa Wasafiri wa Treni ya SGR, nilikata tiketi ya kuondoka asubuhi ya Saa 12:00 leo Januari 8, 2025 lakini ulipofika muda huo safari ikasogezwa mbele kwa nusu saa.

Safari yangu ni kuelekea Dodoma, matarajia ya kuwasili yalikuwa Saa 3:30 asubuhi baada ya hapo ilikuwa nielekee kwenye kikao sehemu fulani ambacho kilipangwa kuanza Saan ne kamili asubuhi.

Safari ilianza vizuri tu na kwa mwendo wa kasi, ilipofika maeneo fulani ambayo siyakumbuki kasi ikaanza kupungua.

Tulipofika Morogoro tukasimama hapo muda mrefu, hadi muda huu saa tano bado tupo Morogoro na hatujui nini kinaendelea.

Safari iliyotarajiwa kufikia tamati saa tatu na nusu, hadi sasa nis aa tano bado tupo Morogoro.

===============

UPDATES...
IMESIMAMA TENA KABLA YA KUFIKA DODOMA

Ilipofika Saa tano na dakika 40 flani hivi Treni ikawashwa tukaendelea na safari, muda wa saa saba na nusu Mchana kabla ya kufika Dodoma, mzigo umezima tena, hatujajua hapa ni wapi ila ndio tunasikilizia kujua nini kinaendelea.

Abiria wote tumeambiwa tushuke kwenye Treni, hatujui nini kinachoendelea.

Imagine niliamka saa tisa ili niwahi Treni ya Saa kumi na mbili na saa tatu na nusu niwe nimefika, mpaka sasa saa saba na nusu mchana hatujafika Dodoma, si bora ningepanda basi nijue moja.

TUNASHUKA, TUNAPANDISHWA KWENYE MABASI
Abiria wote baada ya kuambiwa tushuke, tumeambiwa kuna mabasi ambayo yanakuja kutuchukua hapa tulipo kutupeleka Dodoma Mjini kwa kuwa inaonekana kuna kama Kilometa zaidi ya 20 kabla ya kufika Dodoma.
SGR apewe mwekezajj mzungu ndio itaendeshwa vizuri, serikali ibaki tu kusimamia ubora wa huduma kwa wananchi na prices, but kuendesha huu mradi haiwezi, PERIOD!
 
Acha stori za vijiweni. Treni zinazofanya kazi zote mpya. Zimetengenezwa South Korea. Mara nyingi hitilafu wala sio treni yenyewe.
Zipo baadhi ya treni siyo mpya(brand new) bali ni za mtumba (used or second hand). Hata Rais SSH aliwahi kulizungumzia suala hili na kuuthibitishia umma juu ya uwepo wa suala hili.
 
Zipo baadhi ya treni siyo mpya(brand new) bali ni za mtumba (used or second hand). Hata Rais SSH aliwahi kulizungumzia suala hili na kuuthibitishia umma juu ya uwepo wa suala hili.
Nimeandika ZINAZOTUMIKA SASA HIVI ZOTE NI MPYA. That's a fact. Used yapo mabehewa ya ghorofa vichwa vyake havijafika bado hayatumiki. EMU na hii locomotive ni brand new za SK.
 
Kuna muda matatizo tunayaleta sisi wenyewe wananchi, mara ngapi watu wanakamatwa kwa kuharibu miundombinu ya hiyo SGR, watu wanakamatwa kwa kuiba kopa... Tunajirudisha nyuma wenyewe
 
SGR apewe mwekezajj mzungu ndio itaendeshwa vizuri, serikali ibaki tu kusimamia ubora wa huduma kwa wananchi na prices, but kuendesha huu mradi haiwezi, PERIOD!
Yani tujenge sisi kwa pesa zetu na kutumia wataalamu wetu halafu kuendesha wapese wawekezaji? Walikuwepo wapi hao wawekezaji wakati tunaona fursa?
 
Back
Top Bottom