True Crime Thread: Updated Regularly

True Crime Thread: Updated Regularly

Carl Tanzler

Huyu mwamba nimemuelewa, vip mkuu alikuwa anatumia kilevi gani haswa? ili nijiweke nacho mbali.
 
Hongera kwa mabandiko na ahsante kwa kutenga muda wako kushea nasi simulizi hizi.
Nilichojifunza ni kua japo serial/Psycho killer wengi hua na motive mbalimbali kwa mawazo yao zinazowafanya watende matendo hayo ila kubwa zaidi ni kua wengi wamepitia maisha ya kutopewa UPENDO. Upendo ni kitu muhimu kwa mwanadamu wengi hua hatujali jambo hili tunawaTreat watoto/watu vile tunavyoona sisi inafaa mwisho wa siku tunazalisha watu kama hawa mtoa mada anao waelezea.

Upendo unaweza kumfanya mtu mbaya kupita kiasi kua mwema na upendo unaweza kumfanya mtu mwema awe mbaya zaidi na zaidi. Tujitahidi kuwapa upendo wale walio karibu yetu
Maana kila mwanadamu anahitaji kuoendwa, since we're all need to belong to someone-thing.
Upendo ni factor lakini tabia ya binadamu ni dynamic kuna serial killers waliopata kila kitu utotoni na bado waliturn out kua janga la jamii. Mfano wa haraka ni Ted Bundy, John Wayne Gacy na somebody Love.
 
Kumekua na debates mbalimbali juu ya adhabu ya kifo, deep kidogo kumekua na debate za njia za kutumia kutekeleza adhabu ya kifo.

Zamani kulikua na njia nyingi za kutekeleza adhabu ya kifo kutegemea na eneo Ufaransa walikua wanatumia 'guillotine' ambapo mtu anawekwa kichwa chake usawa wa makali yanaponing'inia kisha hayo makali yanaachiwa yakiwa speed na kufikia kutenganisha kichwa na kiwiliwili. It was a famous practice and it was done in public view.

images (3).jpeg

Guillotine

Overtime hii practice ikawa banned isifanyike hadharani. Mtu wa mwisho kuadhibiwa na guillotine hadharani aliitwa Eugen Weidmann.

Eugen Weidmann alizaliwa mwaka 1908 nchini Ujerumani kipindi cha WW1 Eugen alipelekwa kuishi na babu na bibi yake katika kipindi hichi akaanza udokozi. Tabia ikakomaa na akiwa na miaka 20 Eugen akafungwa miaka 5 kwa kosa la wizi wa kutumia nguvu.
images (1).jpeg

Eugen Wedmann

Akiwa huko gerezani akapata marafiki watatu, Roger Million, Blanc na Fritz Frommer, urafiki wao ukabadilika na kua ushirika wa uhalifu. Walipotoka gerezani wakaamua wawe wanawateka na kuwaibia watalii wanaotembelea Ufaransa. Ili kutimiza adhma yao wakakodi na nyumba Saint Clous eneo ambalo ni karibu na Paris.

Jaribio la kwanza likafeli. Mhanga wao alikua mtata, hatulii wakalazimika kumuachia. Dancer maarufu kutoka New York Jean De Koven akawa jaribio la pili na jaribio hili likafanikiwa. Eugen mwenyewe ndiye akamuua na kumfukia Koven kwenye bustani ya nyumba waliyopanga.

Hiyo ilikua July mwaka 1937. Eugen ana miaka 29.

Kisha hiki kikundi kikampa hundi za Koven mchepuko wa Roger Million ili akazicash hizo hundi. Kupata pesa kwa urahisi hivyo kukachochea ari yao ya kuendelea kupata faida.

Mwaka huo huo mwezi wa 9 tarehe 1 Eugen akamkodi dereva bwana Joseph Couffy ili ampeleke pwani maarufu ya French Riviera, walipofika Eugen akamshoot Joseph kisogoni na kuiba gari. Mwezi wa 10 tarehe 17 mwaka 1937 Roger na Eugen wakapanga miadi na producer aliyeitwa Roger Le Blond wakimuahidi kuwekeza pesa katika moja ya filamu zake badala yake Eugen akamshoot kisogoni (Kama kawaida yake) na kuondoka na wallet yake.

Kisha Eugen akamshoot Raymond Lesobre, real estate agent aliyekua anamuonyesha Eugen mazingira ya nyumba. M.O ile ile alimshoot kisogoni na akaiba gari na wallet ya Raymond.

Kisha mwaka huo huo yeye na Roger Million wakamhadaa Janine Keller, nesi, kwamba wanataka kumpa kazi. Badala yake wakampeleka pangoni na kumuua kisha kuchukua mali zake na kutokomea nazo.

Huyo ndiye akawa mhanga wa mwisho wa Eugen Wedmann.

Maaskari walikuta business card ya Eugen ofisini kwa bwana Lesobre na walipoifuatilia na kufika kwenye nyumba waliyopanga majibizano ya risasi yakaanza. Baada ya kuzidiwa Eugen na wenzake wakakamatwa.

Eugen akakiri makosa yote. Mwezi wa 3 mwaka 1939 hukumu ikatoka. Eugen na Roger Million wakahukumiwa kifo. Blanc akafungwa miezi 20 jela na kimada wa Roger Million akaachiwa huru. Baadaye adhabu ya kifo ya Roger Million ikabadilishwa na kua kifungo cha maisha.

17th June 1939 Eugen akakatwa kichwa kwa kutumia Guillotine. Mtandaoni kuna video yake ikionyesha jinsi tukio lilivyotokea. Zamani watu walishangilia kushuhudia mhalifu kuuawa lakini watu wa 1939 walikua tofauti walilaani na 'hysteria' iliyowapata ikazuka na skendo zingine ikabidi Rais apige marufuku kukata wahalifu vichwa hadharani.

images (2).jpeg

Eugen Wedmann Siku ya Hukumu

Adhabu kwa kutumia guillotine ikaanza kufanywa behind closed doors. Adhabu hii iliendelea mpaka 1977 na mtu wa mwisho kuadhibiwa kwa Guillotine baada ya kuhamishwa na kufanywa kwa kificho aliitwa Hamida Djandoubi.
 
Kumekua na debates mbalimbali juu ya adhabu ya kifo, deep kidogo kumekua na debate za njia za kutumia kutekeleza adhabu ya kifo.

Zamani kulikua na njia nyingi za kutekeleza adhabu ya kifo kutegemea na eneo Ufaransa walikua wanatumia 'guillotine' ambapo mtu anawekwa kichwa chake usawa wa makali yanaponing'inia kisha hayo makali yanaachiwa yakiwa speed na kufikia kutenganisha kichwa na kiwiliwili. It was a famous practice and it was done in public view.

View attachment 2013836
Guillotine

Overtime hii practice ikawa banned isifanyike hadharani. Mtu wa mwisho kuadhibiwa na guillotine hadharani aliitwa Eugen Weidmann.

Eugen Weidmann alizaliwa mwaka 1908 nchini Ujerumani kipindi cha WW1 Eugen alipelekwa kuishi na babu na bibi yake katika kipindi hichi akaanza udokozi. Tabia ikakomaa na akiwa na miaka 20 Eugen akafungwa miaka 5 kwa kosa la wizi wa kutumia nguvu.
View attachment 2013840
Eugen Wedmann

Akiwa huko gerezani akapata marafiki watatu, Roger Million, Blanc na Fritz Frommer, urafiki wao ukabadilika na kua ushirika wa uhalifu. Walipotoka gerezani wakaamua wawe wanawateka na kuwaibia watalii wanaotembelea Ufaransa. Ili kutimiza adhma yao wakakodi na nyumba Saint Clous eneo ambalo ni karibu na Paris.

Jaribio la kwanza likafeli. Mhanga wao alikua mtata, hatulii wakalazimika kumuachia. Dancer maarufu kutoka New York Jean De Koven akawa jaribio la pili na jaribio hili likafanikiwa. Eugen mwenyewe ndiye akamuua na kumfukia Koven kwenye bustani ya nyumba waliyopanga.

Hiyo ilikua July mwaka 1937. Eugen ana miaka 29.

Kisha hiki kikundi kikampa hundi za Koven mchepuko wa Roger Million ili akazicash hizo hundi. Kupata pesa kwa urahisi hivyo kukachochea ari yao ya kuendelea kupata faida.

Mwaka huo huo mwezi wa 9 tarehe 1 Eugen akamkodi dereva bwana Joseph Couffy ili ampeleke pwani maarufu ya French Riviera, walipofika Eugen akamshoot Joseph kisogoni na kuiba gari. Mwezi wa 10 tarehe 17 mwaka 1937 Roger na Eugen wakapanga miadi na producer aliyeitwa Roger Le Blond wakimuahidi kuwekeza pesa katika moja ya filamu zake badala yake Eugen akamshoot kisogoni (Kama kawaida yake) na kuondoka na wallet yake.

Kisha Eugen akamshoot Raymond Lesobre, real estate agent aliyekua anamuonyesha Eugen mazingira ya nyumba. M.O ile ile alimshoot kisogoni na akaiba gari na wallet ya Raymond.

Kisha mwaka huo huo yeye na Roger Million wakamhadaa Janine Keller, nesi, kwamba wanataka kumpa kazi. Badala yake wakampeleka pangoni na kumuua kisha kuchukua mali zake na kutokomea nazo.

Huyo ndiye akawa mhanga wa mwisho wa Eugen Wedmann.

Maaskari walikuta business card ya Eugen ofisini kwa bwana Lesobre na walipoifuatilia na kufika kwenye nyumba waliyopanga majibizano ya risasi yakaanza. Baada ya kuzidiwa Eugen na wenzake wakakamatwa.

Eugen akakiri makosa yote. Mwezi wa 3 mwaka 1939 hukumu ikatoka. Eugen na Roger Million wakahukumiwa kifo. Blanc akafungwa miezi 20 jela na kimada wa Roger Million akaachiwa huru. Baadaye adhabu ya kifo ya Roger Million ikabadilishwa na kua kifungo cha maisha.

17th June 1939 Eugen akakatwa kichwa kwa kutumia Guillotine. Mtandaoni kuna video yake ikionyesha jinsi tukio lilivyotokea. Zamani watu walishangilia kushuhudia mhalifu kuuawa lakini watu wa 1939 walikua tofauti walilaani na 'hysteria' iliyowapata ikazuka na skendo zingine ikabidi Rais apige marufuku kukata wahalifu vichwa hadharani.

View attachment 2013844
Eugen Wedmann Siku ya Hukumu

Adhabu kwa kutumia guillotine ikaanza kufanywa behind closed doors. Adhabu hii iliendelea mpaka 1977 na mtu wa mwisho kuadhibiwa kwa Guillotine baada ya kuhamishwa na kufanywa kwa kificho aliitwa Hamida Djandoubi.


Huyu Hamida alifanya kosa gani?

Ukipata muda utaweka na ile ya Blue Eyed Butcher, pls.
 
Armin Meiwes - Rotenburg Cannibal, Der Mertzgermeister

images (2).jpeg


Baba alikua mkali, hakuwahi kumjali Armin, alipokua na miaka 8 baba yake na mama yake waliachana. Baba mtu akakata mawasiliano kwa miaka na miaka.

Mahakamani katika kutoa ushahidi baba yake alisema kwamba mwanae alikua mtoto mwenye tabia njema na alivutiwa sana na kitabu cha Hansel and Gretel. Haswa pale ambapo Hansel ananenepeshwa ili aliwe.

Baba akaondoka akabaki na mama katika saikolojia tunasema mtoto anahitaji uwepo wa mama na baba katika makuzi yake kumkosa baba kukapelekea Armin ajiundie 'imaginary friend' aliyemuita Franky. Franky alimsikiliza Armin, tofauti na mama yake.

Franky alimsikiliza Armin aliposema anatamani kuwala marafiki zake kwakua watakua sehemu ya maisha yake milele. Franky alikua rafiki na alikua father figure ambaye Armin alimkosa.

Mama yake alipofariki 1999 Armin akiwa na miaka 38 akadondokea kwenye kuangalia porn haswa BDSM porn. Na ni kwenye hizo sites ndipo akakutana na mtandao ulioitwa 'The Cannibal Cafe' ulikua ni mtandao uliowakutanisha watu wenye hamu ya kula nyama za watu.

Hatimaye Armin akawa amepata sehemu ambayo wanashare maoni. He was home. Mwaka 2000 akijiita Franky katika huo mtandao akapost tangazo la kutafuta mtu wa kumla.

ad-768x407.jpg


Tangazo lilisema 'Natafuta kijana mwenye mwili uliojengeka umri kuanzia 18 - 30 kwaajili ya kumla'

Mamia ya watu wakajibu tangazo lake lakini wengi walishikwa na uoga kabla tukio zima halijaisha. Kuna jamaa anaitwa Borg Jose alifika mpaka kwa Armin wakaandaa mazingira Borg akawekwa mezani ili kuchinjwa kuanze ila Borg akasema anajisikia vibaya hawezi kuendelea.

Armin hata hakuuliza mara mbili akamfungua kamba Borg akajiondokea.

Kisha tarehe 14 February 2001 Bernd Brandes, engineer, akajibu tangazo la Armin. Akasema yupo tayari kuliwa. Wakatumiana email wakipanga ni namna gani Brandes ataliwa Brandes akasema itakua vyema kama fuvu lake litatumika kama ashtray.

Brandes alikua bisexual. Tarehe 9 March 2001 Brandes akaenda nyumbani kwa Armin wakaanza kwa kufanya mapenzi walipomaliza ukawadia muda wa kuanza kumla Brandes. Kwa maandalizi Brandes akameza vidonge vya usingizi ishirini na kunywa cough syrup.
images (3).jpeg


Bernd Brandes

Wakaset up camera ili kuchukua tukio zima live.

Mpango wao wa awali ulikua ni kula nyama ya Brandes pamoja. Brandes akasema waanze kuula uume, akamuambia Brandes atumie meno kuutafuna na kuuondoa uume ila Armin akashindwa. Armin akachukua kisu akaukata uume wa Brandes kisha akampa Brandes autafune.

Wakashindwa kuutafuna kutokana na uume kua hautafuniki. Armin akauchukua ule uume na kuukaanga, akachanganya pilipili, tangawizi, mvinyo na vikorombwezo vingine. Akachota na fat kidogo kutoka mwilini mwa Brandes na kuichanganya katika upishi ila uume ukawa umeungua kiasi wakashindwa kuula.

Armin akampa mbwa wake nyama ya Brandes.

Kisha akamuogesha Brandes katika bath tub na kumuacha hapo yeye akaenda kusoma kitabu cha Star Trek. Akawa anarudi kumuangalia Brandes kila baada ya dakika 15.

Baraza lililoangalia hiyo video linasema kwamba Brandes alikua anazimia na kuzinduka huku akiendelea kupoteza damu. Saa 10 mbele tangu akatwe uume ukatwe Brandes bado alikua hai isipokua kupoteza fahamu mara kwa mara kulikua endelevu.

Armin anasema 'Rafiki yangu alienjoy kufa. Nilisubiri sana kabla sijamla. Kifo kilichukua muda mrefu' kwa kuona amesubiri muda mrefu huku akisali Armin akachukua kisu na kumchoma Brandes kwenye koo, alipohakikisha Brandes amekufa akauchukua mwili na kuuning'iniza kwenye ndoano ya nyama.

You see there is a reason Armin is known as The Master Butcher.

Kisha uandaaji wa nyama ukaanza. All the while kamera ikiendelea kurekodi kila kitu.

Akaukata mwili vipande vidogo vidogo kutosheleza finyango za nyama alizohitaji. Akaweka nyama kwenye freezer.

Lile pendekezo la Brandes kwamba fuvu lake liwe ashtray halikusikilizwa kwakua mifupa ilisagwa na kua unga.

Nyama ya zaidi kilo 30 ilipatikana. Na Armin alitumia miezi 10 kula kilo 20 ya mwili wa Brandes.

Nyama ilihifadhiwa kwenye friji kwenye maboksi ya pizza kwa kuona anaishiwa stock ya chakula chake pendwa akarudi tena kwenye mtandao wa 'The Cannibal Cafe' akaweka tena tangazo la kutafuta mtu wa kumla.

Safari hii tangazo likaonekana na mwanafunzi wa kiAustria ambaye akawaambia polisi juu ya uwepo wa tangazo la mtu anayetafuta mtu wa kumla.

Polisi wakavamia nyumbani kwa Armin wakakutana na video za porn za kutosha, nyama kwenye maboksi ya pizza zaidi ya kilo 15 na video iliyoonyesha tukio zima mwanzo mpaka mwisho.

Hii video ilitumika kama ushahidi mahakamani.

Armin hata hakusumbua polisi alikiri na kuelezea tukio bila hata usumbufu.

Askari walitumia miezi saba kukusanya ushahidi ili kuhakikisha katika hiyo kesi Armin hachomoki. 30 January 2004 Armin akahukumiwa kwenda jela miaka nane na nusu kwa kosa la kuua bila kukusudia.

Sababu zikiwa kwamba Brandes alienda akijua kabisa lengo la Armin ni nini na hata hivyo ilikua ngumu kumnasa na adhabu kali zaidi kwakua Ujerumani kula nyama ya mtu siyo kosa kisheria.

Wanasheria wa serikali wakaona hii adhabu ni masihara. Hivyo mwaka mbele wakakata rufaa ili kesi isikilizwe upya na safari hii walitaka mahakama ione kwamba kiukweli Armin alikua ana motive ya kufanya alichofanya na siyo kwamba alitaka tu kula nyama.

Motive waliyostick nayo ni kwamba Armin alifanya hivyo ili kujiridhisha kingono. Zile BDSM porn na wao kufanya mapenzi kabla ya cannibalism ilionyesha kwamba actually Armin aliua ili kupata sexual gratification.

This time mahakama ikamhukumu kifungo cha maisha gerezani.

Baada ya pale mpaka leo Armin aliamua kua vegetarian.
 
Jim Jones - Jonestown Massacre

Kama walivyo viongozi wengine wa dini Jim Jones alikua na haiba ya kuendana na kila mtu. Watu, hata wanasiasa, walijikuta wakimfuata, wakimsikiliza na kuamini kila anachoongea.

images (2).jpeg

Jim Jones
Kanisa lake la kwanza alilofungua halikua linahusiana na dhehebu lolote na kipindi hicho hakua amepata mafunzo yoyote ya uchungaji kipindi hicho aliliita Somerset Methodist Church.

Miaka hiyo ya 1950's kilikua kipindi ambacho ubaguzi wa rangi umeshamiri lakini kanisa lake halikubagua. Wafuasi wa kila rangi waliruhusiwa hii ilipelekea waumini kuongezeka.

Jones akawa anaagiza ngedere kutoka India, Calcutta, na anawauza ili mapato yasaidie kanisa. Si hivyo tu, ikawa zawadi kuu kutoka kwa Mchungaji Jones ni ngedere. Anasema kwamba hii strategy ya ngedere ilisaidia kuongeza wafuasi na mapato.

Mbali na ngedere pia Jones alifungua kituo cha kugawa nguo bure na mgahawa wa supu. Kila mtu alimpenda. Yeye na mkewe wakamuasili mtoto mweusi a bold move kwa Marekani ya miaka hiyo. Mzungu kumuasilia mtoto mweusi ilikua bado kusikika.
535f091f-c663-4253-ad2b-d5d17c297f32-INIBrd_09-17-2017_Star_1_A007__2017_09_16_IMG_jimjones.29...jpg

Mwaka 1960 kipindi hichi akiwa amebadilisha jina la kanisa na kuliita Peoples Temple kanisa lake likawa chini ya dhehebu la Disciples of Christ. Na miaka minne mbele Jones akafuzu mafunzo na kuteuliwa uchungaji chini ya hili kanisa.

Jones alitangaza mahubiri na kila anachofanya kwenye magazeti na redio hiko ndiyo kipindi kila mchungaji anavutia waumini kwa kujipa sifa mbalimbali. Wachache kama Jones wakathubutu kusema wanatenda miujiza pia, na siyo kwa mtu mmoja au watano, NO. Tangazo lake lilisema "Njoo ushuhudie ushuhuda wa miujiza kwa watu 1000"

Ferbruary 1961 Meya wa Indianapolis, Charles Boswell, akakutana na Jones na kumuomba awe mkurugenzi wa Indianapolis Human Rights Commission. Business is booming when politicians want to befriend you. At this point Peoples Temple ilikua na waumimi zaidi ya 3000. Hata nyumba aliyoishi safari hii ilionyesha jinsi gani maisha ameyapatia.

Ambacho meya na ambao siyo waumini wake hawakukiona ni yaliyokua yakiendelea kanisani Peoples Temple, muda milango ikifungwa, au maiki za redio zikizimwa maisha ya waumini yalikua ni kupigwa, kudanganywa na kutapeliwa. Haswa haswa nyumba kwa kuambiwa ni mchango wa kanisa.

Waumini wengi walitishiwa kwamba kutotii maagizo ya mchungaji Jones ni tiketi yako ya kupelekwa concentration camps. Hivyo wengi walitii.

Jones alikua akihubiri kuhusu Ujamaa na kuonyesha jinsi gani ana uhusudu pengine ndiyo maana alichukua mali za waumini as ujamaa unapinga kujilimbikizia mali. Watu wachache wakapenyeza taarifa kwenye vyombo vya habari navyo vikamkalia kooni juu ya swala hili au lile, jengo hili, uwanja ule. Kijana huyu na vidonda vyake wakati anaishi kanisani, pesa za mfuasi huyu n.k.

Maswali yalikua mengi na yakamkera, Jones akaona isiwe tabu nawaachia Marekani yenu. Akawatangazia waumini wake kwamba kanisa linahama, linaenda Guyana, nchi moja ipo huko Latin America.

Ingawa walienda Guyana 1977 ila Jones alikua anajenga makazi huko Guyana tangu miaka 3 nyuma haya makazi aliyaita Jonestown. Wakati anawaambia kwamba wanaenda Jonestown aliwaambia kwamba kuna ardhi nzuri ya kilimo, hali ya hewa ya baridi na hakuna nyoka wala wadudu. Baada ya kufika ikaonekana wazi kila kitu ni tofauti ardhi hailimiki hivyo chakula kikawa hakitoshi. Joto kali na nyoka walikua wa kutosha.
1-jonestown_everett_hisl034_ec367.jpg

Jonestown

Na kila aliyefika pale kwanza alinyang'anywa paspoti na pesa zote alizokua nazo. Maisha yakawa kinyume na walivyotarajia. Walienda watu zaidi ya 1000. Maisha yalikua ni kupigwa, kutishiwa kuuawa na mateso mbalimbali.

Na hapo Jonestown Jones alikua akikalia kiti cha kifalme akijifananisha na Yesu au Vladmir Lenin.

Mara zote akiwahubiria kile alichokiita kama 'Revolutionary Suicide' na akawa anawaambia kwamba kuna siku itafika watatakiwa kujiua kanisa zima. Mara kwa mara alikua akiwafanyisha mafunzo ya jinsi gani ya kujiua kwa kutumia sianidi.

Powerful chemical yenye matumizi mbalimbali kuanzia kuua wadudu mpaka kusafishia dhahabu. Na ili kuipata kwa wingi sianidi ilibidi Jones atafute leseni ya kuonyesha kwamba yeye ni sonara.

Haya majaribio yakawa yamezoeleka pale Jonestown.

November 14, 1978 mwakilishi wa US kutoka California bwana Leo Ryan akiwa na ndugu wa baadhi ya waumini walioishi Jonestown na waandishi wa habari wakaenda pale ili kutafuta uthibitisho wa kwamba kuna wengine hawaishi pale kwa hiyari yao.

Jones alishawafundisha cha kusema waumini wake ama niseme aliwafundisha cha kudanganya. Kwahiyo majibu yalikua ni 'Tunakula nyama na mkate' 'Hapana tuna furaha'

Ryan kwa kuridhishwa na hayo majibu akaazimia kuondoka. Hapo ndipo pabaya, kati ya waliomsindikiza Ryan wengine wakagoma kurudi Jonestown, in fact Ryan akagundua amepenyezewa kikaratasi kilichosema kwamba kila alichoonyeshwa pale Jonestown ni uongo na wanahitaji msaada.
jonestown-leo-ryan-hisl034_ec400.jpg

Congressman Ryan akiwa na wakazi wa Jonestown
Huku Jones alikua ameshatoa agizo kwamba Ryan na kila aliyekuja naye wauawe. Majibizano ya risasi yakafika mpaka kwenye uwanja wa ndege ambao Ryan na wenzake ilitakiwa wautumie kuondoka.

But not today.

Wakafa watu 5 akiwemo Ryan mwenyewe na waandishi 4, watu 11 wengine wakajeruhiwa miongoni mwao ni waliotaka kutoroka na Ryan.

Taarifa iliporudi kwa Jones akaamuru zoezi la Revolutionary Suicide lianze.

Ukiingia mtandaoni ukisearch 'Jonestown death tape' utaletewa mahubiri ya mwisho kabla hii 'Revolutionary Suicide haijafanywa. Mahubiri yalikua ni kulaumu ujio wa Ryana na Jones alikua akisema kwamba Ryan amekuja kuharibu amani yao.

'If we can't live in peace let us die in peace' watu walipiga makofi.

Ukiisikiliza audio kuna hadi watu wanauliza maswali kuna mwanamke anauliza 'Kwani tumechelewa kwenda Urusi?' na Jones anajibu 'It is too late'

Hii death tape mwanzo ilishikiliwa na CIA na watu wengi waliamini waumini walikubali kunywa sumu kwa hiyari yao.

Lakini ukweli hakua huo. Jones alipowakusanya waumini wote ukumbini nyuma ya waumini wakawekwa watu wenye mitutu ili kulinda asiwepo wa kuondoka. Na kuhakikisha kwamba watu hawapingi tukio Jones alianza na watoto na vichanga. Jones anawaambia wazazi 'Msiwaambie watoto wenu kama wanakufa mnawatisha'

jonestown-getty-517432316.jpg

Vikombe na mabomba ya sindano yenye sianidi
Sianidi iliwekwa kwenye bomba la sindano na kunyunyiziwa midomoni kwa watoto. Waumini kwa kudhani ya kwamba bado wapo kwenye practice walikua wametulia ila baada ya kuona jinsi vichanga vikilia na kujikunja kwa maumivu ya tumbo ndipo wakajua kumbe leo ni leo.

And hell broke loose kwa vilio.

Inaaminiwa kwamba watoto kuanza kuuawa iliwafanya wazazi waone hawana sababu ya kuishi na hawana cha kupoteza hivyo watu wengi wakakubali kunywa sumu ya sianidi. Kuna usemi unaitwa 'drinking kool aid' ulizaliwa hapa kutokana na hili tukio.

Mwanamke mmoja Hyacinth Thrash alikua chini ya uvungu wa kitanda akiwa amepitiwa na usingizi. Alipoamka kesho yake alikutana na maiti za watu 913 mojawapo ikiwa ya Jones mwenyewe iliyosababishwa na jeraha la risasi ya kichwa.

Inaaminiwa kwamba Jones alijiua.

Ukijumlisha watu 5 waliofia uwanja wa ndege jumla ya vifo inakua 918.
 
Watu wachache wanaweza kufanya makosa halafu wasiadhibiwe kwa makosa yao. No I lied. Actually ni wengi, just mwezi uliopita watu walianzisha petition ya kutaka kijana mmoja aachiwe huru.

Kosa lake? Anatuhumiwa kuua.

Sababu ya kuachiwa? Ana sura nzuri.

Just that.

Now going through history tunakutana na watu ambao wamewahi kuachiwa huku wamefanya makosa. Mmoja wa hao watu ni Issei Sagawa, mJapan aliyemuua, kumbaka na kumla mwanafunzi mwenzake mHolanzi Renee Hartevelt

images (8).jpeg

Issei Sagawa


Sagawa ni maarufu anajulikana kama celebrity cannibal au Pang na umaarufu wake umeletwa na uhalifu wake alioufanya tarehe 11 June 1981. Crime doesn't pay, huh?

Sagawa anasema alianza kutamani kula binadamu tangu akiwa mtoto na alitamani kula mwanamke wa kizungu, alitamani kumla Grace Kelly, akiwa na miaka 23 huko kwao Japan akavamia nyumba ambayo kuna mwanamke wa Kijerumani aliishi.

Akafanikiwa kuingia ndani na kujaribu kumbana lakini Sagawa ana mwili mdogo, urefu wa futi 5'0, mwembamba mno utajiri wa baba yake haukusaidia kumpa mwili mkubwa.
Bahati nzuri mwanamke alishtuka kabla Sagawa hajafanikiwa azma yake na mwanamke mwenyewe alikua na nguvu kumzidi hivyo polisi walipofika walikuta Sagawa kabananinshwa hawezi kufurukuta.

Alipofikishwa kituoni akaandikiwa mashtaka ya sexual assault baba yake akatoa kitita kwa yule mwanamke ili aachane na ile kesi. As we know money talks so kesi ikafa.

Ambacho hawakujua ni kwamba Sagawa hakuvamia ile nyumba kwa ajili ya kubaka aliingia mule ili aende kumla yule mwanamke so ikabidi aendelee kushikilia fantasy zake zikisubiri muda mwingine.

Sagawa akaenda Ufaransa kusoma katika chuo cha Osborne alienda kusomea maswala ya lugha na fasihi, miongoni mwa classmates wake alikuepo Renee Hartevelt. Sagawa anasema alikua akileta madada poa kwenye apartment yake karibia kila siku kwa nia ya kumtafuna mmoja wapo lakini hakuweza kutekeleza dhamira yake.

Kisha siku ikafika Sagawa akamualika Renee nyumbani haikua mara ya kwanza kwenda kwa Sagawa kwahiyo haikua tatizo. Alipofika akawa anasoma shairi Sagawa akatokea nyuma ya Renee akiwa na bunduki na kumshoot shingoni.

images (3).jpeg

Renee Hartevelt

Anadai kwamba alitamani kuita ambulance lakini akaona kwamba kama siyo leo lini tena?

So akaanza kwa kuibaka maiti ya Renee. Anasema ni siku ambayo alisikia raha kuliko siku zote alizowahi kulala na mwanamke. Alipomaliza sasa ndipo upishi na ulaji ukaanza.

Akaukata mkundu, akaukaanga ila harufu ilikua kali akashindwa kuutafuna akaachana nao. Akahamia kwenye maziwa, kisha lips. Halafu akaanza kula vigimbi vya miguu.
images (7).jpeg

Mwili wa Renee

Alitumia siku mbili kuanzia kumuua Renee mpaka kumla na kuona ameikinai nyama. Akatoka kwenda kununua mabegi mawili makubwa na kuhifadhi mabaki ya mwili wa Renee. Akaita taxi na kumuambia dereva taxi ampeleke Bois de Boulougne, public park, alidhamiria kwenda kutupa mwili hapo.

Dereva taxi akiwa anamsaidia kubeba mabegi akamtania Sagawa 'Mabegi mazito sana kuna maiti nini humu?' Sagawa akacheka bila kujibu na safari ikaanza.

Kutegemea na wapi unaenda kuconsult sources zako juu ya hii kesi kuna sources zinasema alikamatwa hapo hapo na askari walioitwa baada ya kuona mabegi yanavuja damu na zingine zinasema hakukamatiwa hapo badala yake ni watu wakiwa wanajog wakaona mabegi yameachwa hapo huku yakivujia damu.
images (9).jpeg

Mojawapo ya begi

Kwa msaada wa dereva taxi wakapapata anapoishi Sagawa na kufanya ukaguzi wa kushtukiza.

Ambacho sources zinakubaliana ni vyombo vilivyokutwa na nyama, kitambulisho cha Renee na mvinyo. Sagawa akakamatwa na kupelekwa katika taasisi ya magonjwa ya akili ili ifanye tathmini kama ni legally sane kusimama kizimbani.

Hapa ndipo ucelebrity ulipoanzia.

images (2).jpeg


Alikaa hapo kwa miaka 2 katika hiyo miaka 2 akaandika kitabu alichokiita 'In the Fog' na kikawa bestseller because people love to read about murder.

Anyway, baba yake kwa pesa alizonazo akakodi wakili mwenye influence nene tu hivyo majibu yakaja kusema Sagawa ni chizi hivyo hawezi kushtakiwa.

Akakaa miaka 2 mingine katika taasisi ya magonjwa ya akili.

Kisha yule wakili akaishawishi mahakama kwamba ni vyema zaidi kama Sagawa ataenda kupata matibabu yake kwao Japan.

Mahakama ikakubali.

Sagawa akarudishwa Japan.

Japan akafikia taasisi nyingine ya magonjwa ya akili ambayo baada ya evaluation majibu yakasema kwamba Sagawa ana bipolar disorder ila siyo chizi hivyo anaweza kupelekwa mahakamani.

Ufaransa ikasema haina nia ya kuendelea na kesi.

Sagawa akaandika vitabu zaidi ya 20 akawa ana column yake kwenye gazeti, akaonekana katika interviews mbalimbali, akaonekana katika filamu, akatoa reviews za migahawa na akaonekana katika filamu ya porn ambayo alionekana akimng'ata tako porn actress.

Sagawa became famous at the expense of Renee's life.

Sasa hivi ana miaka 72 ila anasema anataka kabla hajafa amle nyama mtu mwingine.
 
Watu wachache wanaweza kufanya makosa halafu wasiadhibiwe kwa makosa yao. No I lied. Actually ni wengi, just mwezi uliopita watu walianzisha petition ya kutaka kijana mmoja aachiwe huru.

Kosa lake? Anatuhumiwa kuua.

Sababu ya kuachiwa? Ana sura nzuri.

Just that.

Now going through history tunakutana na watu ambao wamewahi kuachiwa huku wamefanya makosa. Mmoja wa hao watu ni Issei Sagawa, mJapan aliyemuua, kumbaka na kumla mwanafunzi mwenzake mHolanzi Renee Hartevelt

View attachment 2030871
Issei Sagawa


Sagawa ni maarufu anajulikana kama celebrity cannibal au Pang na umaarufu wake umeletwa na uhalifu wake alioufanya tarehe 11 June 1981. Crime doesn't pay, huh?

Sagawa anasema alianza kutamani kula binadamu tangu akiwa mtoto na alitamani kula mwanamke wa kizungu, alitamani kumla Grace Kelly, akiwa na miaka 23 huko kwao Japan akavamia nyumba ambayo kuna mwanamke wa Kijerumani aliishi.

Akafanikiwa kuingia ndani na kujaribu kumbana lakini Sagawa ana mwili mdogo, urefu wa futi 5'0, mwembamba mno utajiri wa baba yake haukusaidia kumpa mwili mkubwa.
Bahati nzuri mwanamke alishtuka kabla Sagawa hajafanikiwa azma yake na mwanamke mwenyewe alikua na nguvu kumzidi hivyo polisi walipofika walikuta Sagawa kabananinshwa hawezi kufurukuta.

Alipofikishwa kituoni akaandikiwa mashtaka ya sexual assault baba yake akatoa kitita kwa yule mwanamke ili aachane na ile kesi. As we know money talks so kesi ikafa.

Ambacho hawakujua ni kwamba Sagawa hakuvamia ile nyumba kwa ajili ya kubaka aliingia mule ili aende kumla yule mwanamke so ikabidi aendelee kushikilia fantasy zake zikisubiri muda mwingine.

Sagawa akaenda Ufaransa kusoma katika chuo cha Osborne alienda kusomea maswala ya lugha na fasihi, miongoni mwa classmates wake alikuepo Renee Hartevelt. Sagawa anasema alikua akileta madada poa kwenye apartment yake karibia kila siku kwa nia ya kumtafuna mmoja wapo lakini hakuweza kutekeleza dhamira yake.

Kisha siku ikafika Sagawa akamualika Renee nyumbani haikua mara ya kwanza kwenda kwa Sagawa kwahiyo haikua tatizo. Alipofika akawa anasoma shairi Sagawa akatokea nyuma ya Renee akiwa na bunduki na kumshoot shingoni.

View attachment 2030874
Renee Hartevelt

Anadai kwamba alitamani kuita ambulance lakini akaona kwamba kama siyo leo lini tena?

So akaanza kwa kuibaka maiti ya Renee. Anasema ni siku ambayo alisikia raha kuliko siku zote alizowahi kulala na mwanamke. Alipomaliza sasa ndipo upishi na ulaji ukaanza.

Akaukata mkundu, akaukaanga ila harufu ilikua kali akashindwa kuutafuna akaachana nao. Akahamia kwenye maziwa, kisha lips. Halafu akaanza kula vigimbi vya miguu.
View attachment 2030877
Mwili wa Renee

Alitumia siku mbili kuanzia kumuua Renee mpaka kumla na kuona ameikinai nyama. Akatoka kwenda kununua mabegi mawili makubwa na kuhifadhi mabaki ya mwili wa Renee. Akaita taxi na kumuambia dereva taxi ampeleke Bois de Boulougne, public park, alidhamiria kwenda kutupa mwili hapo.

Dereva taxi akiwa anamsaidia kubeba mabegi akamtania Sagawa 'Mabegi mazito sana kuna maiti nini humu?' Sagawa akacheka bila kujibu na safari ikaanza.

Kutegemea na wapi unaenda kuconsult sources zako juu ya hii kesi kuna sources zinasema alikamatwa hapo hapo na askari walioitwa baada ya kuona mabegi yanavuja damu na zingine zinasema hakukamatiwa hapo badala yake ni watu wakiwa wanajog wakaona mabegi yameachwa hapo huku yakivujia damu.
View attachment 2030876
Mojawapo ya begi

Kwa msaada wa dereva taxi wakapapata anapoishi Sagawa na kufanya ukaguzi wa kushtukiza.

Ambacho sources zinakubaliana ni vyombo vilivyokutwa na nyama, kitambulisho cha Renee na mvinyo. Sagawa akakamatwa na kupelekwa katika taasisi ya magonjwa ya akili ili ifanye tathmini kama ni legally sane kusimama kizimbani.

Hapa ndipo ucelebrity ulipoanzia.

View attachment 2030878

Alikaa hapo kwa miaka 2 katika hiyo miaka 2 akaandika kitabu alichokiita 'In the Fog' na kikawa bestseller because people love to read about murder.

Anyway, baba yake kwa pesa alizonazo akakodi wakili mwenye influence nene tu hivyo majibu yakaja kusema Sagawa ni chizi hivyo hawezi kushtakiwa.

Akakaa miaka 2 mingine katika taasisi ya magonjwa ya akili.

Kisha yule wakili akaishawishi mahakama kwamba ni vyema zaidi kama Sagawa ataenda kupata matibabu yake kwao Japan.

Mahakama ikakubali.

Sagawa akarudishwa Japan.

Japan akafikia taasisi nyingine ya magonjwa ya akili ambayo baada ya evaluation majibu yakasema kwamba Sagawa ana bipolar disorder ila siyo chizi hivyo anaweza kupelekwa mahakamani.

Ufaransa ikasema haina nia ya kuendelea na kesi.

Sagawa akaandika vitabu zaidi ya 20 akawa ana column yake kwenye gazeti, akaonekana katika interviews mbalimbali, akaonekana katika filamu, akatoa reviews za migahawa na akaonekana katika filamu ya porn ambayo alionekana akimng'ata tako porn actress.

Sagawa became famous at the expense of Renee's life.

Sasa hivi ana miaka 72 ila anasema anataka kabla hajafa amle nyama mtu mwingine.

[emoji1550][emoji1550]kwamba aliukaanga mkundu halufu ikawa kali akaahirisha kuutafuna[emoji2][emoji2],visa vingine haivifai kuvisoma kama wew eni mtu wa karibu wa mhanga,unaweza muua mharifu mbele ya polisi.
 
Credonia Mwerinde - Kanungu District Massacre

Katika historia kuanzia ya kale mpaka sasa mwanamke ameonyeshwa kama kiumbe dhaifu ambaye anamtegemea mwanaume kwa kila kitu. Ukikaza macho kidogo katika historia utakutana na wanawake ambao walitenda uhalifu, mauaji na uhuni sawasawa na wanaume na wengine wamewazidi wanaume.

King Tamara (Wafuasi hawakumuita Queen) amewazidi wanaume wengi ila Credonia (Walitamka Keredonia) Mwerinde yupo level moja na Jim Jones.

Ulaghai, utapeli na mauaji vyote unakutana navyo ukiangalia historia ya Mwerinde. Ingawa historia nyingine inamtaja kama kahaba aliyejiuza katika kilabu chake cha pombe za kienyeji lakini aliyekua mume wake anasema ni kweli Mwerinde alikua malaya ila alikua hajiuzi. Hakuwa akilipwa kwa ajili ya ngono.

Mume wa Credonia Mwerinde Bwana Eric Mazima anasema kwamba biashara yao ilipata changamoto ikafa kisha 24th August 1988 Credonia akamuambia kwamba amepata maono kutoka kwa bikira Maria na sasa anataka kugeukia dini.

Wiki moja mbele Credonia akaondoka nyumbani.

images (2).jpeg

Credonia Mwerinde

Akiwa na wenzake watatu safari yake ikamchukua mpaka Nyamitanga, akawa ana shughuli ya kutoa ushuhuda juu ya maono anayopata kutoka kwa Bikira Maria. Akiwa hapa akakutana na Joseph Kibwetere, Kibwetere alikuja Nyamitanga na mkewe ili kuja kusikiliza hizi shuhuda. Hata yeye Kibwetere alidai anapokea maono kutoka kwa Bikira Maria, alitaka kukutana na mwenzake siku hiyo.

Juvenal Mugambwa, mtoto wa Kibwetere, anasema Credonia akamuambia baba yake kua "Nimepewa maono nimtafute mtu anayeitwa Kibwetere na tushirikiane kueneza injili" Juvenal anasema hiyo jioni baba yake alirudi nyumbani na Credonia, dada yake Credonia, marafiki zake wawili na mama yake wakati aliondoka nyumbani na mama pekee.

Credonia na Kibwetere wakaanzisha kanisa waliloliita Restoration of the Ten Commandments of God, kanisa lilikusanya watawa na mapadri ambao walitengwa na kanisa katoliki. Hili kanisa jipya likawa kimbilio la mabaki ya kanisa katoliki.

images (3).jpeg

Joseph Kibwetere

Kisha pale nyumbani zikaanzishwa sheria mbalimbali, ikawa hamna kuongea badala yake mawasiliano yakawa kwa ishara, hamna kula pipi ni ushetani, hakuna kutumia sabuni na mpangaji wa maisha ya pale alikua ni Mwerinde mwenyewe, na yeye alitoa maelekezo kutoka kwa Bikira Maria na Bikira Maria alimfikishia ujumbe Credonia kwa kupitia simu.

Simu ilikua ni kifaa chochote ambacho Credonia ataamua kiwe simu. Kwahiyo angeweza kutumia kikombe, kijiko au sahani kama simu ya siku hiyo ya kupokelea maagizo kutoka kwa Bikira Maria. Kanisa likazidi kukua na pale nyumbani pakawa hapatoshi wakatafuta sehemu mpya huko Kanungu, Kibwetere akamuacha mkewe na kumuambia ameamua kwenda na Credonia ili kusambaza injili vizuri.

Juvenal Mugambwa anasema inawezekana baba yake na Credonia walikua na uhusiano uliosababisha wagandane ila anaamini sababu zingine ni Credonia alihitaji mwanaume atakayekua sura ya kanisa, pia baba yake alikua ni tajiri kwa viwango vya Uganda ya 1970s hivyo hakuna namna Credonia angemuachilia Kibwetere.

Kanisa likazidi kukua. Sheria kali zilikua pale pale makosa yaliambatana na adhabu kali, kuongea uongo ilikupasa kusali rozali mara elfu moja. Kosa kubwa zaidi ilikupasa kumuomba msamaha Bikira Maria moja kwa moja, wakati mwingine inabidi uende kwenye jiwe lililosemwa ni kiwakilishi cha Bikira Maria na uende kuomba msamaha hapo.

_111327484_2b284666-615d-4f4a-95f3-fb3da7ff39a6.jpg
Jiwe lililofanana na Bikira Maria

Kanisa liliamini dunia itaisha. Na kutii amri kumi za Mungu ndiyo njia pekee ya kuokoka, kanisa lilivuna waumini kupitia hii nadharia, lilivuna na mali za waumini pia kupitia hii nadharia.

. . . Baadaye kidogo . . .
 
Credonia Mwerinde - Kanungu District Massacre

Katika historia kuanzia ya kale mpaka sasa mwanamke ameonyeshwa kama kiumbe dhaifu ambaye anamtegemea mwanaume kwa kila kitu. Ukikaza macho kidogo katika historia utakutana na wanawake ambao walitenda uhalifu, mauaji na uhuni sawasawa na wanaume na wengine wamewazidi wanaume.

King Tamara (Wafuasi hawakumuita Queen) amewazidi wanaume wengi ila Credonia (Walitamka Keredonia) Mwerinde yupo level moja na Jim Jones.

Ulaghai, utapeli na mauaji vyote unakutana navyo ukiangalia historia ya Mwerinde. Ingawa historia nyingine inamtaja kama kahaba aliyejiuza katika kilabu chake cha pombe za kienyeji lakini aliyekua mume wake anasema ni kweli Mwerinde alikua malaya ila alikua hajiuzi. Hakuwa akilipwa kwa ajili ya ngono.

Mume wa Credonia Mwerinde Bwana Eric Mazima anasema kwamba biashara yao ilipata changamoto ikafa kisha 24th August 1988 Credonia akamuambia kwamba amepata maono kutoka kwa bikira Maria na sasa anataka kugeukia dini.

Wiki moja mbele Credonia akaondoka nyumbani.

View attachment 2042297
Credonia Mwerinde

Akiwa na wenzake watatu safari yake ikamchukua mpaka Nyamitanga, akawa ana shughuli ya kutoa ushuhuda juu ya maono anayopata kutoka kwa Bikira Maria. Akiwa hapa akakutana na Joseph Kibwetere, Kibwetere alikuja Nyamitanga na mkewe ili kuja kusikiliza hizi shuhuda. Hata yeye Kibwetere alidai anapokea maono kutoka kwa Bikira Maria, alitaka kukutana na mwenzake siku hiyo.

Juvenal Mugambwa, mtoto wa Kibwetere, anasema Credonia akamuambia baba yake kua "Nimepewa maono nimtafute mtu anayeitwa Kibwetere na tushirikiane kueneza injili" Juvenal anasema hiyo jioni baba yake alirudi nyumbani na Credonia, dada yake Credonia, marafiki zake wawili na mama yake wakati aliondoka nyumbani na mama pekee.

Credonia na Kibwetere wakaanzisha kanisa waliloliita Restoration of the Ten Commandments of God, kanisa lilikusanya watawa na mapadri ambao walitengwa na kanisa katoliki. Hili kanisa jipya likawa kimbilio la mabaki ya kanisa katoliki.

View attachment 2042300
Joseph Kibwetere

Kisha pale nyumbani zikaanzishwa sheria mbalimbali, ikawa hamna kuongea badala yake mawasiliano yakawa kwa ishara, hamna kula pipi ni ushetani, hakuna kutumia sabuni na mpangaji wa maisha ya pale alikua ni Mwerinde mwenyewe, na yeye alitoa maelekezo kutoka kwa Bikira Maria na Bikira Maria alimfikishia ujumbe Credonia kwa kupitia simu.

Simu ilikua ni kifaa chochote ambacho Credonia ataamua kiwe simu. Kwahiyo angeweza kutumia kikombe, kijiko au sahani kama simu ya siku hiyo ya kupokelea maagizo kutoka kwa Bikira Maria. Kanisa likazidi kukua na pale nyumbani pakawa hapatoshi wakatafuta sehemu mpya huko Kanungu, Kibwetere akamuacha mkewe na kumuambia ameamua kwenda na Credonia ili kusambaza injili vizuri.

Juvenal Mugambwa anasema inawezekana baba yake na Credonia walikua na uhusiano uliosababisha wagandane ila anaamini sababu zingine ni Credonia alihitaji mwanaume atakayekua sura ya kanisa, pia baba yake alikua ni tajiri kwa viwango vya Uganda ya 1970s hivyo hakuna namna Credonia angemuachilia Kibwetere.

Kanisa likazidi kukua. Sheria kali zilikua pale pale makosa yaliambatana na adhabu kali, kuongea uongo ilikupasa kusali rozali mara elfu moja. Kosa kubwa zaidi ilikupasa kumuomba msamaha Bikira Maria moja kwa moja, wakati mwingine inabidi uende kwenye jiwe lililosemwa ni kiwakilishi cha Bikira Maria na uende kuomba msamaha hapo.

View attachment 2042302Jiwe lililofanana na Bikira Maria

Kanisa liliamini dunia itaisha. Na kutii amri kumi za Mungu ndiyo njia pekee ya kuokoka, kanisa lilivuna waumini kupitia hii nadharia, lilivuna na mali za waumini pia kupitia hii nadharia.

. . . Baadaye kidogo . . .
Lakini hii nadharia ikawa inaelekea kufeli kwakua kila tarehe iliyotabiriwa kua ni mwisho wa dunia, dunia haikuisha. Ikapelekea kuzalishwa kwa minong'ono ya chini kwa chini juu ya uongo na utapeli wa Mwerinde na wenzake.

Hii ilimaanisha wanahitaji kuja na suluhisho haraka ama dunia iishe au warudishe mali walizotoa kwa waumini. Kiendacho kwa mganga hakirudi na pili ile nadharia ya dunia kuisha? Mwerinde & co walijua kabisa hakuna kitu kama hicho so kabla mamlaka kidogo waliyobaki nayo wakayatumia kuita kusanyiko.

Kusanyiko lilikua ni kwaajili ya kua pamoja siku dunia inaisha. Na ikaamuliwa kusanyiko liwe tarehe 17 March 2000.

Ukiangalia pattern za matukio ya wauaji kuna points mbili au tatu utapata zinazoweza saidia kutabiri baadhi ya matukio mfano, Mwerinde kabla hajahamia kwa Kibwetere aliwahi kuchoma moto nyumba ya mwanakijiji mwenzake na akapotea hilo eneo akarudi wiki mbele. Akadai amechanganyikiwa, kipindi hicho alikua na miaka 20.

Kisha kuna madai ya kumtongoza dereva pikipiki, usiku walivyolala akamuua na kumuibia pesa. Kuna ripoti pia ya kaka zake 3 kufa mmoja mmoja kabla hajabaki peke yake na kurithi nyumba ya baba yao. Haya matukio yameelezwa katika barua iliyoandikwa na rafiki wa karibu wa familia ya Mwerinde.

Kisha tukio la mwisho kabla hajahama nyumbani kwa Kibwetere lilikua la kumchomea moto mke wa Kibwetere kabati lake la nguo. Hii kazi alimpa mdogo wake Ursula Mwerinde, yeye akachukua kazi ya kumshushia kipigo Bi Teresa Kibwetere. Bi Teresa alikimbia kukwepa kipigo.

Kama unashangaa mume alikua wapi mume alikuepo na alikua anasupport.

Kwa haya matukio na pattern iliyopo vyovyote iwavyo 17th March ilitakiwa iwe siku ngumu. Ripoti za mwanzo zilisema baada ya kukutana wakajifungia kwenye jengo lao la makao makuu wakajimwagia petroli na kujiwasha moto.

Lakini kama watu walienda kudai mali na pesa zao au dunia iishe hivi utawamwagia petroli wakuangalie? Haiingii akilini na ndivyo uchunguzi ulivyothibitisha.

Baada ya wote kuingia ukumbini milango ikafungwa kwa nje, sehemu ambazo zingeweza kutoa upenyo wa kutoka zikagongelewa misumari na petroli ikamwagwa kuzunguka jengo zima.

And then the building was set on fire.

Maeneo ya kanungu ni ya milimani na mabondeni wenyeji wanasema mlipuko wa moto wa ghafla na vilio ulitawala eneo la Kanungu. Kisha ikafuatiwa na harufu kali ya nyama inayochomwa kiasi kwamba ilibidi wachukue majani yenye harufu kuziba pua kukata harufu ya nyama.

Ripoti zinasema hata baada ya moto kuzimika harufu ya nyama ilitawala eneo lote kiasi kwamba wenyeji walishindwa kula nyama mwezi baada ya tukio kuisha.

Askari walipofika eneo la tukio walikuta miili inayokadiriwa kufikia 600 ikiwa imekua mikaa, wakaripoti tukio zima kama mass suicide na kutulia, walipoanza kuchunguza viwanja vilivyokua chini ya umiliki wa Movement wakagundua kuna makaburi ya pamoja mengi yaliyokutwa na maiti zaidi ya 300. Kaburi moja urefu wake ulifikia hecta 40.

Miili iliyokutwa humo ilikua na majeraha ya visu, kupigwa na kitu kizito kichwani na kulishwa sumu askari wakabadili walichoripoti. Wakasema hii ni mass murder na wakatoa hati ya kimataifa ya Mwerinde na Kibwetere kukamatwa popote walipo.

Miaka hiyo, njia za mawasiliano zilikua hafifu zilitosha kufanya hawa wawili wasikamatwe. Kibwetere ilisemekana amejificha Malawi lakini Uganda walipofuatilia walishindwa kumpata.

Jeshi la Polisi la Uganda linaamini Mwerinde na Kibwetere wapo hai na kuna mahali wamejificha.
 
Lakini hii nadharia ikawa inaelekea kufeli kwakua kila tarehe iliyotabiriwa kua ni mwisho wa dunia, dunia haikuisha. Ikapelekea kuzalishwa kwa minong'ono ya chini kwa chini juu ya uongo na utapeli wa Mwerinde na wenzake.

Hii ilimaanisha wanahitaji kuja na suluhisho haraka ama dunia iishe au warudishe mali walizotoa kwa waumini. Kiendacho kwa mganga hakirudi na pili ile nadharia ya dunia kuisha? Mwerinde & co walijua kabisa hakuna kitu kama hicho so kabla mamlaka kidogo waliyobaki nayo wakayatumia kuita kusanyiko.

Kusanyiko lilikua ni kwaajili ya kua pamoja siku dunia inaisha. Na ikaamuliwa kusanyiko liwe tarehe 17 March 2000.

Ukiangalia pattern za matukio ya wauaji kuna points mbili au tatu utapata zinazoweza saidia kutabiri baadhi ya matukio mfano, Mwerinde kabla hajahamia kwa Kibwetere aliwahi kuchoma moto nyumba ya mwanakijiji mwenzake na akapotea hilo eneo akarudi wiki mbele. Akadai amechanganyikiwa, kipindi hicho alikua na miaka 20.

Kisha kuna madai ya kumtongoza dereva pikipiki, usiku walivyolala akamuua na kumuibia pesa. Kuna ripoti pia ya kaka zake 3 kufa mmoja mmoja kabla hajabaki peke yake na kurithi nyumba ya baba yao. Haya matukio yameelezwa katika barua iliyoandikwa na rafiki wa karibu wa familia ya Mwerinde.

Kisha tukio la mwisho kabla hajahama nyumbani kwa Kibwetere lilikua la kumchomea moto mke wa Kibwetere kabati lake la nguo. Hii kazi alimpa mdogo wake Ursula Mwerinde, yeye akachukua kazi ya kumshushia kipigo Bi Teresa Kibwetere. Bi Teresa alikimbia kukwepa kipigo.

Kama unashangaa mume alikua wapi mume alikuepo na alikua anasupport.

Kwa haya matukio na pattern iliyopo vyovyote iwavyo 17th March ilitakiwa iwe siku ngumu. Ripoti za mwanzo zilisema baada ya kukutana wakajifungia kwenye jengo lao la makao makuu wakajimwagia petroli na kujiwasha moto.

Lakini kama watu walienda kudai mali na pesa zao au dunia iishe hivi utawamwagia petroli wakuangalie? Haiingii akilini na ndivyo uchunguzi ulivyothibitisha.

Baada ya wote kuingia ukumbini milango ikafungwa kwa nje, sehemu ambazo zingeweza kutoa upenyo wa kutoka zikagongelewa misumari na petroli ikamwagwa kuzunguka jengo zima.

And then the building was set on fire.

Maeneo ya kanungu ni ya milimani na mabondeni wenyeji wanasema mlipuko wa moto wa ghafla na vilio ulitawala eneo la Kanungu. Kisha ikafuatiwa na harufu kali ya nyama inayochomwa kiasi kwamba ilibidi wachukue majani yenye harufu kuziba pua kukata harufu ya nyama.

Ripoti zinasema hata baada ya moto kuzimika harufu ya nyama ilitawala eneo lote kiasi kwamba wenyeji walishindwa kula nyama mwezi baada ya tukio kuisha.

Askari walipofika eneo la tukio walikuta miili inayokadiriwa kufikia 600 ikiwa imekua mikaa, wakaripoti tukio zima kama mass suicide na kutulia, walipoanza kuchunguza viwanja vilivyokua chini ya umiliki wa Movement wakagundua kuna makaburi ya pamoja mengi yaliyokutwa na maiti zaidi ya 300. Kaburi moja urefu wake ulifikia hecta 40.

Miili iliyokutwa humo ilikua na majeraha ya visu, kupigwa na kitu kizito kichwani na kulishwa sumu askari wakabadili walichoripoti. Wakasema hii ni mass murder na wakatoa hati ya kimataifa ya Mwerinde na Kibwetere kukamatwa popote walipo.

Miaka hiyo, njia za mawasiliano zilikua hafifu zilitosha kufanya hawa wawili wasikamatwe. Kibwetere ilisemekana amejificha Malawi lakini Uganda walipofuatilia walishindwa kumpata.

Jeshi la Polisi la Uganda linaamini Mwerinde na Kibwetere wapo hai na kuna mahali wamejificha.
Asante sana mwamba
 
John Wayne Gacy Jr
Siku inapoanza kwa John ilikua ama yupo bize kukuza kampuni yake ya ujenzi, anaandaa party kwa ajili ya marafiki na majirani zake au atakua hospitali za Chicago akiwafurahisha wagonjwa kwa kuvaa mavazi ya 'clown'.

Kila mtu alimpenda John. Alikua mfano wa kuigwa na aliaminiwa hata na baadhi ya wazazi ambao walimuachia watoto wao awalindie. I mean who wouldn't? Mfanya kazi kwa bidii, anayecheka na kila mtu si ni mtu sahihi huyu, ama?

Tarehe 22, May 1978 Jeffrey Ringall alikua ametokea vacation Florida na amerudi Chicago, siku hiyo akaamua kuelekea New Town eneo maarufu kwa kua na baa na vilabu lengo ni kutengeneza marafiki. Njiani akakutana na Oldsmobile nyeusi, dereva, mnene hivi kipande cha mtu, akatoa kichwa na kumsifia Ringall ngozi yake.

Kisha akamkaribisha Ringall ndani ya gari ili wavute bangi pamoja huku wakizunguka eneo la New Town. "Kuvuta bangi ndani ya gari na mtu simjui hata kidogo?" Ringall akakubali. Akaingia kwenye gari wakaanza kupasiana kijiti.

Katikati ya kupasiana kijiti Ringall akashangaa amefunikwa usoni na tambara hata kabla hajaju nini kinaendelea akapoteza fahamu. Tambara lilikua limejazwa klorofomu. Ringall akawa anazinduka na kupoteza fahamu kabla hajajua alipo akafunikwa tena tambara lenye klorofomu.

Safari hii akazinduka akiwa ndani ya nyumba anajiona yupo uchi akiangalia chini anaona madildo mengi yamesambaa. Na yule jamaa waliyepasiana kijiti akimtambia kwamba hayo madildo yote atayatumia naye.

Ringall akazinduka kesho asubuhi akiwa chini ya sanamu eneo la Chicago Lincoln Park. Akiwa amebakwa na kuumizwa sehemu mbali mbali za mwili, akaenda kwa mpenzi wake kisha wakaenda hospitali ambako alikaa kwa siku 6. Akatoa taarifa polisi lakini ikawa ngumu askari kuanza uchunguzi kutokana na kutokua na details zote.

Alikua amechanwa na kuunguzwa sehemu mbalimbali za mwili na ini lake likapata madhara ya kudumu kutokana na klorofomu, lakini alikua na bahati kubaki hai. Ringall akawa miongoni mwa wahanga wachache wa John Wayne Gacy ambao hawakukutwa na umauti.

Kwa muda wa miaka mitatu Gacy alibaka, aliwatesa na aliwaua vijana wa kiume zaidi ya thelathini. Miili yao ilikutwa kwenye mto na mingine ilikutwa chini ya floor board ya nyumba ya Gacy.

. . . Tutaendelea . . .
 
Back
Top Bottom