True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

165
Babu aliongea maneno mengi kwa kikabila ambapo baadhi niliyaelewa na mengine yalinipita bila kuambulia maana yake.
Nilimsikia akisema ndugu zangu, nimeishika leo hii silaha yenu ya maangamizi si kwa lengo la kulipa kisasi ama kumwadhibu mbaya wangu, bali naomba msaada kijana wangu ameonewa na msichana ambae ni mkuu wa miliki ya giza kwa upande wa kati, tena pasipo kujua aliingia nae maagano ya damu kwa kumvua usicha wake, sasa anataka kumsumbua na mimi sitaki kumwumiza binti yule, kama nilivyokwisha kuwaambia ndugu zangu sitaki tena kumwaga damu ya mtu, nataka niishi maisha yangu ya uzeeni kwa amani kabisa, aliongea maneno yale babu akiwaomba watu wasioonekana.

Nikiwa nimefumba macho huku nayatafakari maneno yale ya babu, ilionekana zamani alikuwa mwanga huyu naye, kwani amejuaje kwamba yunge alikuwa ni mkuu wa kanda ya kati? Pia nilimsikia akisema hataki tena kumwaga damu ya mtu, huyu mzee ni mlozi naye tu, niliwaza.

Shusha mkono chini na uunyoshe kwa mbele, alinambia babu nami nikafanya vile.

Paaah!
 
Mzee baba tupooo nzehe bega kwa bega mpaka yunge akomeshwe
 
166
Nilipigwa na kitu kizito juu ya mkono, ajabu nilisikia sauti ya kike ikilia kwa uchungu masikioni mwangu, "bhuhabhi mnataka kumwua mwanenuuu" nilielewa kabisa ilikuwa sauti ya yunge mkubwa, nilifumbua macho na kuangaza nimwone huyo mwanetu tunaetaka kumwua, nilistaajabu kumwona babu akiwa amebadirika mwili ukiwa mweusi pii na macho yaking'aa kama tochi, haraka nilifumba macho kwa hofu.

Ahsante mpenzi kwa kumwokoa mwanetu kipenzi, niliisikia tena sauti ya yunge kisha hali ikawa shwari kwani sikumsikia tena babu kuongea na maumivu ya mkono yalirudi kwa nguvu, hapa ikumbukwe mara baada ya babu kinipiga pale mkononi na kitu ambacho nilihisi kama chupa kubwa na tupu ya maji maumivu yalikoma ghafla, ila baada ya kufumbua macho tu na kumwona babu katika hali ya kutisha, maumivu yalirudi tena kwa nguvu.

Nililia kwa nguvu kwani maumivu yalikuwa makali mno, sikumsikia babu akiongea wala kufanya jambo lolote lililoashiria uwepo wake pale karibu na mimi, hatimae nilifumbua macho nione babu alikuwa katika hali ipi.
 
Woyoooo


Yaan hapo kama ndo DJ MACK
Utasikia BONGE la mluzi
Yaan ile ile
Uchawi uchawi
Unyambisi unyambisi


Shusha vituu mkuu
 
167
Nilitahamaki kumwona babu kalala tuli pale chini huko macho yake yang'ayo kama ya mnyama yakiwa wazi, kwa muda nilisahau maumivu yangu ya mkono na nikatoka nduki kwenda kumwita bibi ambae sikumwona pale nyumbani.

Nilikimbia mpaka kwao yunge mdogo kwani ndo majirani waliokuwa karibu zaidi na kwetu, nilibisha hodi nisimwone mtu yeyote pale, nipaza sauti kumwita yunge mdogo huku nikilia kuomba msaada lakini palikuwa kimya kabisa.

Nilirudi mpaka pale nyumbani na kumwita bibi, lakini hakuitika.

Kilio sasa kilikuwa cha hofu na mashaka juu ya hali ya babu yangu kule nyuma ya nyumba kwani sasa niliogopa hata kwendako kwa hofu iliyotokana na hali aliyokuwa nayo babu.

Niliingia ndani kumtafta bibi labda alikuwa amesinzia, lakini palikuwa patupu, nilitoka nje na nikawa najishauri kama niende kule nyuma ya nyumba nilikomuacha babu akiwa katika hali tatanishi ama nibaki pale.

Hapana, mwanaume haogopi kifo, niliwaza huku nikianza kuzipiga hatua kuelekea nyuma ya nyumba.

Nisaidie mwananguu, aliniomba babu akilia.
 
Uongo
 
Maskin babu wa watu
 
168
Niliona mafisi makubwa mawili yenye macho yang'aayo yakiwa yanamvuta babu kuelekea vichakani huku kila moja limeshika kwa meno mkono mmoja wa babu ambae macho yake bado yalikuwa yanang'aa kama zamani.

Nilichanganyikiwa kumwona babu yangu kipenzi akiwa anavutwa chini tena na mafisi, hapa niliijiwa na picha mbaya sana kichwani, yaani babu yangu kipenzi aliwe na fisi? Nililia kwa sauti lakini hakuna aliyetokea.

Nilitimua mbio na mpaka nikamfikia babu na kumshiki miguu kwa ujasiri, nilianza kushindana nayale mafisi kumvuta babu ambae alilia kwa maumivu ya kuvutwa huku na huku, nilimwachia babu kwa ghafla na yale mafisi yalipigiza matako chini kwani hayakutegemea kama ningefanya kitendo kile ghafla vile.

Ondoka hapa hatuna shida na wewe, ilisikika sauti ya mwanamke kutoka kinyani mwa mmoja wa yale mafisi, nilishangaa sana fisi kuongea.
Naomba mniachie babu yangu msimle nyama, nilibembeleza.
Mpumbavu sana wewe, ondoka haraka kabla hatujakutafuna, aliongea kwa sauti yule fisi mwingne.

Siondoki, nililia mno.
 
Pamojaa mkuu
 
169
Nililia kwa nguvu huku nikiwafata wale fisi ambao ghafla tu walimezwa nagiza wasionekane, bahati nzuri walimwacha pale babu akiwa kalala akigugumia kwa maumivu makali, niliangaza huku na kule nione labda huenda wale mafisi walikuwa karbuh sikuwaona, nilimshika babu kiunoni nakumwinua huku nikilia kwa uchungu, nilimkokota kuelekea ndani mwake lakini tulipofika katikati ya kiwanja pale nyumbani alikataa kwenda ndani mwake na kunitaka twende ndani mwangu.

Tulifika ndani mwangu nikamkarisha babu juu ya kitanda ambapo sasa godoro na nguo zangu zilikuwepo.

Umeniingiza kwenye matatizo makubwa mjukuu wangu na sasa hawa watu wameniweza na watakula nyama yangu mimii! Aliongea kwa majonzi babu huku akinitupia lawama nisijue kosa langu.

Nilijiinamia tu huku maumivu ya mkono yakiendelea bila kukoma na machozi yalinitiririka sana tu, nimefanya nini tena babu anasema mimi nimesababisha matatizo? Niliwaza sana bila kupata majibu.

Mwanangu, wakati tukiwa kule nyuma ya nyumba ulifumbua mcho? Aliniuliza babu...!
 
Doh,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…