True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

Success never come to people who listens to too many whistles.

My friend JF is a jungle with too many animals, braves to fools

Dont base to fools dear fella, those are dogs in the Cage, that make you lose direction, infact they can not bite

Fact, and now am back again to entertain my fans, enjoy my story.
πŸ˜€ in this thread I thought only few will get these but I am wrong πŸ˜€
Kumbe kuna wasomi🀣
 
Babu kakumbuka enzi zake[emoji23]
 
[emoji3] in this thread I thought only few will get these but I am wrong [emoji3]
Kumbe kuna wasomi[emoji1787]

Babu macho yaling’aa kama wale kwenye movie za Marvel [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
171
Nilichungulia chini ya kitanda {uvunguni} na kama nilivyotarajia niliziona siraha zangu mle ambazo sikuwa hata na ufungdi wowote wa kuzitumia.

Niupembe mdogo uliojipindapinda kama wa kondoo dume, vibuyu vidogo vitatu, usinga {mkia mfupi mweusi} na ngozi kubwa ya chui, hapo moyo ulifurahi sana na kabla sijapitisha mkono kuzichukua zile zana, nilimtazama babu na kumwona akitabasamu, tabasamu la matumaini huku akitikisa kichwa kuniruhusu niendelee na nilichokusudia.

Nilipitisha mkono chini ya kitanda na nikawa nabeba kitu kimoja baada ya kingine mpaka ikabaki ngozi pekee, nayo niliivuta na kuitoa uvunguni kisha nikaitandika pale chini kando ya kitanda.

Zima taa ndipo uendelee na harakati zako, aliniamuru babu nami nikazima taa kisha nikaanza kuzipanga zana zangu za mashambulizi pale juu ya ngozi, baada ya hapo niliushika ule usinga kwa mkono wangu wa kushoto na ghafla niliusikia mkono ukiwa mwepesi mno na maumivu yalikoma mara moja.

Safi sana na hongera, wewe ni shujaa wangu na tumaini langu katika vita.
 
172
Kitendo cha wewe kukumbuka kuwa unasiraha ambazo zinaweza kukusaidia ni ushindi tosha na hizi zana ndo msaada pekee kwetu kuliko hata hata bibi yako na majirani uliokuwa unawaita na kuomba msaada kwao, alisema babu.

Inamaana kumbe alikuwa ananisikia wakati naenda kuomba msaada nyumbani kwa kina yunge mdogo? Niliwaza.

Sasa nenda nyuma ya nyumba ukaniletee ile zana niliyokuwa nimeibeba wakati ule nakufanyia tiba kisha uje hapa, hakikisha ukiibeba zana hiyo hutoiweka chini mpaka uje unipe mikononi mwangu, alitoa angalizo babu akiwa gizani na hatuonani kabisa.

Nilifika nyuma ya nyumba na bila kuhangaika kutafuta nilikifikia tu kile kitu kilichoonekana kama chungu kidogo sana huku kimezungushiwa matambala madogo meusi na mekundu makuukuu, nilishangaa licha ya giza zito lakini kilionekana vyema tu.

Nilikisogelea haraka huku nikiangaza macho huku na kule kuhakiki usalama wangu, nilikifikia na kuinama haraka, nilikitwaa na ghafla nilihisi mkono wangu wa kushoto kukakamaa na misuli kubana.
Nilitoka nduki...!
 
173
Nilikimbia mpaka ndani huku mkono niliobebea kile chungu ukiwa umekakamaa na misuli kunisimama, nilifika chumbani na kumkabidhi babu aliyekuwa gizani.

Safi sana rafiki yangu, sasa mambo yatakua murua na tutakomesha wapuuzi wote watakao tuletea ujuaji hapa, hatutaonea mtu, alisema babu.

Mkono ulirejea katika hali yake na nilianza kuhisi kunakitu kinanitekenya mkononi lilipokuwa jeraha la kuingiliwa na mikia ya mijusi, nilimwomba babu niwashe taa ili tuone kunanini kinajiri pale mkononi.

Washa tu, alisema babu nami nikabonyeza swichi ya kisola na taa ikawaka,
Tulitupia macho mko wangu wa kushoto tukaona kama mng'aro kama wa kamasi zilizokaukia.

Ebu mulika pale chini, alisema babu nami nikamulika chini, tuliwaona konokono wawili wadogo wakiwa wamekauka.
Umepona mwanangu, alisema babu na kuoitaka niwatupe nje wale konokono.

Hawa watu wanataka kutujaribu akili hawa, alisema babu.
Kinanani hao babu? Nilimwuliza babu.
Bibi yako na yange wanataka kunimaliza, ila nitawanyoosha, naomba tu unisaidie jambo moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…