True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

Get Rich ulimruhusu afanye mambo yake post story akijisikia imekuwaje tena mpenzi hahaha
😅😅😅😂😂 unajua mpenzi na mm ka arosto kameniingia sema tu naona soo kufos mambo😅😅

namuona mwamba Pettymagambo yuko online kule michezoni sasa anasauje mashabiki zake.. sijui anacheza rede huko na Chizi Maarifa ??😂😂
 
185
Tulifika bombani kwa kutangulizana, nilitangulia mimi huku tatu akiwasili dakika mbili baadae, tulingoja kidogo kwani foreni haikuwa ndefu sana muda huu.
Leta nikusaidie kuchota maji tatu, nilimwambia ili kuwafumba macho wengine waliokuwepo pale wasijue tulitoka kukifanya muda mfupi uliopita.

Mhh! Kweli wagombanao ndio wapatanao, aliongea mwanamke mmoja huku akijitwisha ndoo ya maji na kuondoka, sikujali kwani nilijua kila mmoja atakua anajua kilichotokea baina yangu na tatu wiki mbili zilizopita.

Tukiwa njiani tunarudi nyumbani, nilimsisitiza tatu kwamba nilikuwa nampenda mno na tusahau yaliyotokea, kweli alionekana kuwa mpole na mnyenyekevu tofauti kabisa na yule tatu niliemjua mimi.

Tulipofika mahala pakutawanyika nilimsisitiza asiache kunifata usiku kwani raha alizonipa sijawahi pewa.
Sifa nilizompa zilimlevya na kumfanya ukenue kila muda bila kujua kwamba alikuwa anauvaa mtego ambao mimi sikujua malengo ya mtego wenyewe.

Tulitanyika pale na kila m1 akashika njia yake.

Je nini kitatokea? Usikose.
Nimejiunga Jamiii Forum kwa ajiri ya Yunge Mkubwa na mdogo 😁.
Embu lete mambo kila dakika nachungulia kama Kuna muendelezo.
 
Back
Top Bottom