Trump anapanga Kujitoa UN na NATO

Trump anapanga Kujitoa UN na NATO

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Bilionea Elon Musk ameonyesha kuunga mkono wazo la Marekani kujiondoa katika Umoja wa Mataifa (UN) na Muungano wa Kijeshi wa NATO.

Akijibu chapisho la mtandaoni jana Jumapili lililohimiza hatua hiyo, Musk, ambaye anaongoza Idara ya Ufanisi wa Serikali ya Marekani (DOGE), aliandika kwa ufupi: "Ninakubaliana."

Rais wa Marekani, Donald Trump, na wabunge wa chama cha Republican wameahidi kutathmini upya ushiriki wa Washington katika UN na NATO.

Mnamo Februari, Seneta Mike Lee wa Utah aliwasilisha mswada wa DEFUND Act, unaopendekeza Marekani ijiondoe kabisa kutoka UN. Lee alikosoa Umoja wa Mataifa kama “jukwaa la madikteta” linalopinga Marekani na washirika wake, akisema licha ya ufadhili mkubwa, UN imeshindwa kuzuia vita, mauaji ya kimbari, ukiukwaji wa haki za binadamu, na majanga ya kiafya.

Nipashe

====

My Take
Sawa tuu ajitoe kwani lazima awepo? Dunia inakoelekea ni kutamu. Na chawa wake bwana Musk yeye Huwa ni kusema ndio Mzee tu.
 
New York ilikuwa inafanya biashara sana wakati wa vikao vya UNGA na mahoteli yalikuwa yakiingiza fedha nyingi sasa watu wa New York watakuwa wamepoteza biashara aisee hivi huyu Trump bado anafanya biashara za Hoteli?
 
Makao makuu ya UN yahamishiwe Afrika.
Asilimia zaidi ya 60% ya bajeti ya matumizi ya AU yanatolewa na wafadhili ambao mfadhili mkubwa ni Marekani.

Kama mnashindwa hata kufadhili matumizi ya taasisi yenu wenyewe, mkiletewa UN mtaweza kweli?

Naunga mkono wazo la Marekani kukata misaada ulimwenguni hasa Afrika ili tuchangamke, viongozi wengi afrika wao wana matumizi makubwa yasiyo na msingi wowote, matumizi ya juu kwenye vitu visivyoongeza thamani kwenye uchumi. Wao wanasubiri tu misaada.
 
Back
Top Bottom