Trump Ataja Korolokwini kama ni Dawa Inaweza Kutibu au Kufubaza Virusi vya Corona

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Dakika chache tu zilizopita, Rais wa Marekani Bw. Donald J. Trump, katangaza kuwa shirika la madawa la Marekani, FDA, limeruhusu dawa ya malaria, ambayo wengi wetu tumeitumia sana, kuanza kutumika katika kutibu virusi vya Corona.

Chloroquin, ndo dawa yenyewe. Matumizi yatakuwa kwenye hatua ya clinical trial.

Idadi ya vidonge vya chloroquin nilivyovimeza maishani mwangu haihesabiki. Achilia mbali sindano zake. Dozi ya sindano ilikuwa ni 1x3.

Hats off kwa “mabeberu”.

Sisi tuna wachawi wengi sana na waganga wengi tu wa kienyeji.

Kama kweli hawa wataalamu wetu wana huo ujuzi ambao hudaiwa wanao, kwa nini washindwe kwenye hili la kutibu Corona?

Heko Marekani. Mchango wake kwenye advancement of humanity hauelezeki kwa maneno.

 
Hiyo dawa ilinitesa sana utotoni, ilikua inaniwasha balaa, navimba vimba mwili kila mahali. Noma sana ile

Sent using Jamii Forums mobile app

Dawa chungu sijapata kuona!

Kuimeza ilikuwa ni songombingo!

Sindano zake ukichomwa unajisikia hali flani hivi ya kukereketwa kooni halafu inakulewesha.

Sitoisahau hiyo dawa.

Ila sasa kwamba eti yaweza kuwa ndo tiba ya Corona?

Talk about coming full circle ⭕️
 
yaan ukiwa unakaribia kupona muwasho wa hiyo dawa haumithiliki na kwabahati mbaya unazidi usiku wakati wa kulala huku masikio yakiwa yamejazwa kelele usiyojua imetoka wapi
 
Usiwalaumu Waganga wa jadi tu ongeza na wachungaji ambao huleta matumaini ya uongo wa wazi. Wanachagua magonjwa yasiyoonekana. Hutawasikia wakiponya kipindupindu na sijawasikia wakiponya corona. Kikubwa tuwalaumu wanaoshinda makanisani wakitegemea miujiza ishuke miilini mwao.
 

Hivi mtu anaweza kurogwa akapata malaria?
 
So nikusema sasa hivi tusiwe na shaka nikiupata nameza zangu chloroquine maisha yanaendelea?

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Halafu, kwani kuna ‘perfect’ society hapa ulimwenguni?
Hakuna perfect society mkuu. Ujue watu wengi hasa Africa hawana access ya habari zilizothibitika so mara nyingi wanailaumu USA sababu wanasikia mabaya yakitangazwa na wakuu wa kisiasa while yaliyo mazuri yanafichwa kwa maslahi ya wachache.
 
Nyani Ngabu,
Hatari sana ni mkubwa wagu alikuwa anasagia kwenye kijiko anachanganya na maji ndio ninywe utoto wangu sikuweza meza vidonge.
Uchungu wake usiupimie
 
Hakuna perfect society mkuu. Ujue watu wengi hasa Africa hawana access ya habari zilizothibitika so mara nyingi wanailaumu USA sababu wanasikia mabaya yakitangazwa na wakuu wa kisiasa while yaliyo mazuri yanafichwa kwa maslahi ya wachache.
Mazuri ya US hayafichiki....,mabaya vilevile... Labda wewe si mfuatiliaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…