Trump atishia kusitisha uhusiano na China

Trump atishia kusitisha uhusiano na China

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kusitisha mahusiano na China kutokana na dhima ya taifa hilo katika kusambaa kwa virusi vya corona ambavyo hadi sasa vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 300,000 duniani.

Katika mahojiano yaliyorushwa jana Alhamis Rais Trump amerejea shutuma zake dhidi ya China akisema ilificha ukweli kuhusu ukubwa wa janga hilo wakati virusi vilipozuka mjini Wuhan mwishoni mwa mwaka uliopita.

Akuzungumzia hatua ambazo nchi yake inaweza kuchukua dhidi ya China, Rais Trump amesema Washington inaweza kusitisha uhusiano wote uliopo na Beijing.

Hadi sasa Marekani imerikodi zaidi ya vifo 86,000 kutokana na virusi vya corona, ambayo ni idadi kubwa zaidi kuliko taifa jingine lolote huku ikiwa na karibu theluthi ya maambukizi ya virusi hivyo duniani.


DW
 
Anangojea nini sasa [emoji16][emoji16] huyu mzee bana kweli hana akili timamu

Ila hakuna taifa linaloweza kukata mahusiano na UCHINA moja kwamoja kwasasa hakuna labda mbeleni hukooo...

Sent using My COVID-19
 
Anangojea nini sasa [emoji16][emoji16] huyu mzee bana kweli hana akili timamu

Ila hakuna taifa linaloweza kukata mahusiano na UCHINA moja kwamoja kwasasa hakuna labda mbeleni hukooo...

Sent using My COVID-19
We trust in Trump... yeye kazi yake ni kubonyeza button tu kazi kwisha...
BullshitButton-main.jpg
 
mi sioni makali ya corona maana kama mpaka sasa hatujafa hata laki 5 hv sasa hii ndio mnaita janga la dunia ?

yaani tasmini yangu nilijua ndani ya mwezi mmoja hapa kwetu tuko zaidi ya milioni 60 kwa haraka haraka mpaka sasa nilijua tungekua tumeshaondoka hata milioni 10 hivi ila mpaka sasa mimi katika ndugu,jamaa na marafiki naowajua hakuna hata mmoja mwenye ana corona au amekufa kwa corona.

sasa yowe za nini ?
 
mi sioni makali ya corona maana kama mpaka sasa hatujafa hata laki 5 hv sasa hii ndio mnaita janga la dunia ?

yaani tasmini yangu nilijua ndani ya mwezi mmoja hapa kwetu tuko zaidi ya milioni 60 kwa haraka haraka mpaka sasa nilijua tungekua tumeshaondoka hata milioni 10 hivi ila mpaka sasa mimi katika ndugu,jamaa na marafiki naowajua hakuna hata mmoja mwenye ana corona au amekufa kwa corona.

sasa yowe za nini ?
@kamdudu nahisi kama vile akili yako inawazia mali za urithi kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo.
 
@kamdudu nahisi kama vile akili yako inawazia mali za urithi kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo.
sasa nitarithi nikiwa nimekufa au ?
sasa umadahi tukifa milioni hata 10 hv mi nitabaki ?
 
Mkubwa kishasema, sisi vinchi vingine vyenye utapiamloo tufunge mabakuli yetu.
 
Natizama sasa hivi BBC Swahili,uzalishaji China ktk viwanda umekuwa kwa 4% tokea waondoe lockdown.Naona hapo ndipo Trump anapopagawa,wakati yeye kasimama wenzake wameanza kukimbia.
 
Trump mzozo wako wa kidiplomasia na china hauna afya kwa sasa. Huu ni wakati wa dunia moja dhidi adui mmoja.. corona.
 
mi sioni makali ya corona maana kama mpaka sasa hatujafa hata laki 5 hv sasa hii ndio mnaita janga la dunia ?

yaani tasmini yangu nilijua ndani ya mwezi mmoja hapa kwetu tuko zaidi ya milioni 60 kwa haraka haraka mpaka sasa nilijua tungekua tumeshaondoka hata milioni 10 hivi ila mpaka sasa mimi katika ndugu,jamaa na marafiki naowajua hakuna hata mmoja mwenye ana corona au amekufa kwa corona.

sasa yowe za nini ?
Haswaaa ata Mie nashangaaa at janga la dunia wakati apa Tz hawajafa ata buku
 
Rais Trump amesema Washington inaweza kusitisha uhusiano wote uliopo na Beijing.
SO FAR KIUHALISIA HAKUNA MAHUSIANO MAZURI YA UKWELI BAINA YA MATAIFA HAYO MAWILI, EVERYBODY KNOWS. SASA HAYO MATISHO HAYAMSHTUI MTU YYTE DUNIANI. MALIZANENI TU WENYEWE KWA WENYEWE HUKO, SISI TUNAPIGA NYUNGU NA MOLA ANATUSITIRI.
 
Back
Top Bottom