Trump hatashinda japo na Kamala Harris hatauweza urais wa Marekani kipindi ambapo taifa hilo linadidimia

The Muslim American vote matters and it can no longer be taken for granted

 
Shukrani sana kwa muda wako kiongozi.

Kwenye upande wa ULIMWENGU kuendeshwa kwa Siri kubwa hapo ndo kuna msingi mkubwa wa swali langu. Of course niliuliza ili kukutega tu na umekuwa makini sana umeruka mtego. Salute sana🫡

Dunia imewekwa kwenye MATRIX, tunapangiwa vitu vya kujua na taarifa za kuzipata (wanao fanikiwa kutoka nje ya Matrix ni wachache sana na ndio ambao wanafanikiwa kuujua ukweli ambao upo nyuma ya pazia).

Andrew Tate na harakati zake za kutaka kuufungua ulimwengu unamcost, now wameshika mali zake zote na yeye mwenyewe.

They call it "THE CONSPIRACY OF EVERYTHING"

50% ULIMWENGU unalishwa taarifa za uongo kwa manufaa ya hao wakubwa.


So far uwe na wakati mwema mkuu 👏
 
Soma hapo juu Nyani Ngabu ameelezea vizuri. Itakuasaidia sana kuelewa Trump alishindaje uchaguzi
Wewe ndo u some VIZURI.

Wewe pamoja na huyo nani ngabu mnakiri kuwa popular votes hazichagui rais wa marekani jambo ambalo hata Mimi kwa kusoma vyanzo vya habari vya uhakika kama BBC najua Hilo kuwa popular votes hazichagui rais wa marekani na ndicho nilichomwambia mleta mada katika post yangu namba #30.
 
Kwamba watu 400+ ndio wanaweza ama wana haki ya kuthibitisha maamuzi ya watu zaidi ya 300M+ wao kama nani kuwazidi hao wengine Million walopiga kura?
Acha kudandia mambo yanayokuzid kimo, hujui chochote na hakuna kitu kibaya kama kujikweza unajua kumbe hujui kitu. Hao unaowaita 400+ bila shaka hujui wanapatikanaje!
Kama uingereza ile ndio imekufa kabisa kila angle Americant haijafika huko ila itafika nanatamani iwe chini ya kamala kama atashinda kura zao zamchongoma
Gharama ya ujinga ni mkubwa na kama taifa limejaa wajinga kama wewe, si ajabu yakatokea kama haya tunayoyashuhudia ya kijinga kama hapa kwetu.

Marekani (USA) ni nchi ya wahamiaji ambayo hadi sasa imefaulu kwa kiwango kikubwa kuishi pamoja duniani bila kujali tofauti zao kama rangi, dini, itikadi, kabila wala jinsia,

Marekani (USA) wapo binadamu kutoka bara zote duniani kuanzia Marekani kwenyewe, Ulaya, Asia na Afrika. Marekani ni jaribio (experiment) la binadamu tofauti kuishi pamoja.

Marekani kama jaribio (experiment) limefaulu kwa asilimia kubwa sana kuwaweka mamilioni ya binadamu waliozikimbia nchi zao wakisaka maisha bora ndani ya taifa hilo.

Wazungu kama Trump kwa mamilioni, Warusi kwa mamilioni. Wachina kwa mamilioni, Waafrika kwa mamilioni na Waarabu kwa mamilioni, wote wanaiita Marekani (USA) taifa lao.

Kwa sasa nitaachia hapo...!
 
Kwa maelezo yako mwenyewe ni ngumu kiasi gani kwako kukiri kuwa popular votes marekani haziamui nani awe raisi?
 
Nimekuelewa sana pia

Sasa kwanini matokeo ya mwisho tu kwamba Hillary alimshinda DT kwa kura nyingi yasiwe final say kwamba Hillary aingie ikulu

Kama kweli kura zawananchi pekee zatosha kua mwamuzi
Kura za jumla jumla zinaweza kuwa na Upendeleo, zinaweza zisiwe na picha nzima ya kuwakilisha wamerekani kutoka katika majimbo yote 50+.

Kumbuka ili uwe Rais wa USA unatakiwa uwe unakubalika kwenye majimbo mengi zaidi miongoni mwa majimbo yote (vinchi 50) ndani ya USA, hivyo mtu anaweza akapata kura zote za jimbo moja kubwa (labda kura milioni 10) lakini akakosa kura zote za majimbo mengine matano (labda yana jumla ya kura milioni 8). Matokeo katika majimbo sita yataonyesha ameshinda kura milioni 10 dhidi ya kura milioni 8, lakini ukichambua hicho kitu utagundua atakuwa amechaguliwa na jimbo moja na kukataliwa katika majimbo sita. Ni vipi awe rais wa USA?
 
Nimekuelewa vizuri sana mkuu, Kumbe ndio maana huwa kuna majimbo yanagombaniwa sana kumbe sababu ni hiyo,

Utaratibu mzuri sana
 
Kwa maelezo yako mwenyewe ni ngumu kiasi gani kwako kukiri kuwa popular votes marekani haziamui nani awe raisi?
Mimi nimesema Electoral college votes(kura za wajumbe) ni hitimisho la maamuzi ya Popular votes (kura za wananchi wote). Popular votes ndio huzaa electoral college votes.
Na ndio maana nikakwambia kabla ya kupigwa kura za Popular votes hakuna anayejua mshindi ni nani, lakini baada ya kupigwa kura za popular votes kila mtu anamjua mshindi, na hakuna anayewaza tena mshindi kuja kupatikana kupitia Electoral college votes ambayo huja kupigwa wiki kadhaa huko baadaye.

Mwisho kabisa kwanini hujiulizi wagombea wanatumia muda mwingi, pesa na mbinu mbalimbali kupiga kampeni USA kuwafikia mamilioni ya wamerekani ili kupigiwa kura za Popular votes badala ya kwenda kuwasaka hao wajumbe 400 wa Electoral college votes ikiwa kura za hao wajumbe ndio huamua rais wa USA?
 
wewe na Nyani Ngabu nimewaelewa sana, asante
 
Nadhani huenda hautaelewa tena kuhusu hili ikiwa tumekuelewesha mpaka basi. Nenda katazame hizo kura milioni mbili za zaidi alizopata Hillary zimetokea wapi halafu nenda kawaze Rais wa USA anachaguliwa na wamerekani kutokea majimbo 52. Halafu njoo tujadili upya.
 
Huo ndo utaratibu waliojiwekea usiumize sana kichwa
 
Marekani kuwa kwenye mbaya ya kiuchumi umeitoa wapi?
 
Majimbo 52 Marekani? Yamekuwa 52 toka lini?
 

Huwezi utenganisha Uislam na uarabu.
Uislam NI uarabu lakini Uarabu siô Uislam.

Yàani uarabu umezaa Uislam ila Uislam Kamwe hauwezi kuzaa Uarabu.

Mtu anayetenga Uislam na uarabu NI mtu àmbaye aidha hajui Uislam ni nini au ameamua makusudi kabisa kudanganya Akili Yake.

Bila Uarabu Hakuna Uislam
 
Hao Mia tano wanapatikanaje , Ushawaji jiuliza hilo?
 
Wewe utakuwa mwana CCM, maana unafikiri Wamerika wapumbavu. Wenzako wanafanya uchaguzi wa haki na unaojali wapiga kura wanachokitaka
 
Wewe utakuwa mwana CCM, maana unafikiri Wamerika wapumbavu. Wenzako wanafanya uchaguzi wa haki na unaojali wapiga kura wanachokitaka
Usisahau kuwa hilo taifa lipo kwenye dimbwi la matope.Kila wanakoelekea wanajitapakazia mtindo mmoja.
Uchaguzi wa mwaka huu ndio utakaondika historia ya kuanguka kwa Marekani.
 
Asante kwa uzi,hizo siasa za ubaguzi na kuitenga Marekani na jumuia za kimataifa ndiyo zilizompa uraisi Trump kwenye ule uchaguzi aliopita,halafu hiyo point ya mwisho hapo uliyoielezea kuhusu udhaifu wa raisi mwanamke kwenye siasa za dunia ambazo kwa sasa zimegubikwa na vita na migogoro mikubwa isioisha,zilimuangusha pia Hilary Clinton na Trump akapeta,Marekani bado haipo tayari kutawaliwa na raisi mwanamke,Kuna undi kubwa la wapiga kura ambao wana hiyo mentality ya kutaka Marekani iendelee kuwa mbabe duniani wanahitaji Kiongizi kama Trump,kwa Mimi binafsi na uzoefu wangu wa kufuatilia chaguzi mbalimbali duniani,namuona Trump akirejea madarakani na Chama chake cha Republican,japo hayo siyo matarajio ya watu waliowengi duniani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…