Trump sijui atatoboa, Kura za Maoni zinamkataa

Trump sijui atatoboa, Kura za Maoni zinamkataa

Mleta mada ameleta mada kwa usahihi kabisa kiupeo lakini wachangia wa mada walio wengi hapa JF katika hili mpaka sasa wameonyesha upeo duni mnoo.

Ngoja nichangie kitu.
1. Upepo wa kura za maoni uliokuwa unampa Trump nafasi ya kushinda hapo awali wakati akichuana na Biden umeendelea kubadilika kwa kasi tangu Kamala ateuliwe, na kwa sasa upepo huo unampa Kamala nafasi nzuri ya kushinda. Hii ina maanisha nini? Trump ana wakati mgumu zaidi na huenda akaangushwa ikiwa hali hii itaendelea hivi hivi na ikiwa kura hizo za maoni zinaakisi maoni halisi.

2. Mleta mada ameleta kura za maoni kutoka taasisi kadhaa tofauti tofauti za USA ambazo huendesha zoezi la kura za maoni kwa weredi mkubwa. Ni taasisi hizo hizo pia hapo awali zilionyesha Trump akiongoza dhidi ya Biden, na ziliendelea kuonyesha Trump akiongoza dhidi ya Kamala pale mwanzoni japokuwa kwa tofauti ndogo. Kwa sasa zinaonyesha Kamala Harris anaongeza. Hii inamaanisha nini? Kwa sehemu kubwa kura hizo za maoni huenda zimebeba uhalisia kuliko agenda ya kumpigia kampeni mgombea fulani.

3. Kura hizo za maoni hulenga mfumo mzima wa kumpata Rais wa USA na huchukua maoni kiujumla na kimajimbo. Kura hizo za maoni hutumiwa na vyama na wagombea wa pande zote katika kujitathimini na kujipanga zaidi. Kupitia kura hizo za maoni chama cha Democrat na Biden mwenyewe waliamua kufanya maamuzi magumu ya kubadili mgombea wake na kumpitisha Kamala Harris dakika za mwishoni.
 
Marekani sio vichaa wamchague raisi mwanamke aongoze nchi kipindi hiki, Utaona kura zitavyopinduka.

Huyu wetu nae labda kura ziibwe. Kinyume na hapo hatoboi!

Ukiona mwenzako ananyolewa, Nawe zako tia maji.
 
Republicans walijua mpinzani wao atakuwa Rais wa sasa Biden, kisaikolojia wakajiona wameshamshinda hasa kwa zile kete zao mbili za uzee na ugonjwa.

Lakini ghafla Democrats wakaibuka na Kamala, hapo automatically hizo kete mbili za Reps zikafa natural death, tena mbaya zaidi kete moja ya uzee ndio ikamgeukia mgombea wao Trump.

Now ukitazama kampeni zao zinavyokwenda, clearly unaona kabisa Trump hana sera nzito ya kuwashawishi wamarekani wamuelewe dhidi ya Kamala, labda kufanyia kampeni zake kwenye kioo kisichopitisha risasi ndio kunaweza kumpa kura za huruma.
 
Kwa jamii ya Watu waliostaarabika, kumchagua Trump kuwa Rais wa nchi ni makosa makubwa sana.

Trump ni mtu ambaye Hana adabu hata kidogo.
Kwa sababu alisema inatakiwa mtawaliwe tena ndo kawa hana adabu?
Trump ni msema kweli bwashee! Wewe nchi mnapewa misaada halafu bado viongozi went wanaiba na wanaficha hela hukohuko zilikotoka
 
Hivi unaelewa kweli namna Mfumo wa Uchaguzi wa Rais wa nchi ya Marekani ulivyo?
Upigaji Kura kwa Uchaguzi wa Rais wa Marekani upo kwenye Vipengele viwili, navyo ni'-
1. Popular Votes.
2. College Votes.

Ushindi wa Rais katika Uchaguzi wa Marekani hutegemea zaidi kwenye College Votes. Wala siyo Popular Votes.
Katika uchaguzi wa Rais wa Marekani, kuna aina mbili za kura zinazotumika: kura za wananchi (popular votes) na kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi (electoral votes).

1. Kura za Wananchi (Popular Votes):
  • Hizi ni kura zinazopigwa na wananchi wa Marekani katika kila jimbo.
  • Kura hizi zinaamua kiasi gani cha kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi atakavyopewa mgombea katika kila jimbo.
  • Katika majimbo mengi, mgombea anayepata kura nyingi zaidi katika jimbo anapata zote au sehemu kubwa ya kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi za jimbo hilo (sawa na mfumo wa "winner-takes-all").

2. Kura za Wajumbe wa Baraza la Uchaguzi (Electoral Votes):
  • Kura hizi zinatolewa na wajumbe wa baraza la uchaguzi, ambao wana idadi maalum kulingana na ukubwa wa jimbo (idadi ya wajumbe inategemea idadi ya wawakilishi wa jimbo katika Bunge la Marekani).
  • Jumla ya kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi ni 538. Ili kushinda urais, mgombea anahitaji kupata angalau kura 270.

Nguvu ya Kura:
  • Kura za Wajumbe wa Baraza la Uchaguzi ndio zinazoamua mshindi wa urais. Hii ni kwa sababu mfumo wa uchaguzi wa Marekani umeundwa ili mgombea apate kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi, si kura za wananchi moja kwa moja.
  • Hivyo, ingawa kura za wananchi zina umuhimu mkubwa katika kuonyesha mapenzi ya umma, mshindi wa urais anatambulika kwa kupata kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi.

Mfumo huu ulianzishwa kwa sababu ya maelezo ya kihistoria na kikatiba, kwa lengo la kuzingatia usawa kati ya majimbo yenye idadi kubwa na ndogo ya watu, na kuhakikisha kwamba majimbo yote yanajumuishwa katika mchakato wa uchaguzi.



Akili hatuna, lakini kuna akili mnemba (IA
 
Hapana Trump!

Inategemea wenye nchi wanataka nani awe Rais!

Kumbuka hasta secretary Clinton alishinda dhidi ya Trump kwenye popular votes lakini Trump akapewa coz alishinda kwenye kura za house of representatives!
Kitu kama haukijui, uliza. Acha kuandika porojo.
 
Duu marekani elecrote college zinaamuliwa na majimbo yenye kura nyingi ukishinda popular votes kwenye strong states mfani san fransico ,Florida and etc ni lazima chama chako kichukue electrote college zote na hapo mshindi anapatika wazi..
Huyo kamara haris anapata umaarufu TU kama WA secretary Clinton!lakini anaweza shinda popular votes akashindwa house of representatives votes!

Hapo ndipo.mtego ulipo hapo!!Kura za masenetor ndio huwa zinamweka Raid madarakani!
Aisee re
 
Katika uchaguzi wa Rais wa Marekani, kuna aina mbili za kura zinazotumika: kura za wananchi (popular votes) na kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi (electoral votes).

1. Kura za Wananchi (Popular Votes):
  • Hizi ni kura zinazopigwa na wananchi wa Marekani katika kila jimbo.
  • Kura hizi zinaamua kiasi gani cha kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi atakavyopewa mgombea katika kila jimbo.
  • Katika majimbo mengi, mgombea anayepata kura nyingi zaidi katika jimbo anapata zote au sehemu kubwa ya kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi za jimbo hilo (sawa na mfumo wa "winner-takes-all").

2. Kura za Wajumbe wa Baraza la Uchaguzi (Electoral Votes):
  • Kura hizi zinatolewa na wajumbe wa baraza la uchaguzi, ambao wana idadi maalum kulingana na ukubwa wa jimbo (idadi ya wajumbe inategemea idadi ya wawakilishi wa jimbo katika Bunge la Marekani).
  • Jumla ya kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi ni 538. Ili kushinda urais, mgombea anahitaji kupata angalau kura 270.

Nguvu ya Kura:
  • Kura za Wajumbe wa Baraza la Uchaguzi ndio zinazoamua mshindi wa urais. Hii ni kwa sababu mfumo wa uchaguzi wa Marekani umeundwa ili mgombea apate kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi, si kura za wananchi moja kwa moja.
  • Hivyo, ingawa kura za wananchi zina umuhimu mkubwa katika kuonyesha mapenzi ya umma, mshindi wa urais anatambulika kwa kupata kura za wajumbe wa baraza la uchaguzi.

Mfumo huu ulianzishwa kwa sababu ya maelezo ya kihistoria na kikatiba, kwa lengo la kuzingatia usawa kati ya majimbo yenye idadi kubwa na ndogo ya watu, na kuhakikisha kwamba majimbo yote yanajumuishwa katika mchakato wa uchaguzi.



Akili hatuna, lakini kuna akili mnemba (IA
Wewe ndio umeeleza kwa kina!
Popular votes haziamui ushindi wa Rais bali Baraza la wajumbe,hapo sawa!
 
Kamala hajamshinda Trump kwa chochote ni kwa vile media zipo upande wa blue.

Ila Trump anakubalika sana kwa sasa USA.
Trump atakuwa rais ila kwa anguko la USA kiuchumi na kushuka kwa kasi kiushawishi wake duniani kunakoenda kutokea muda mchache sana ujao ataongoza kwenye mazingira magumu sana
 
Nilichogundua hautaki mtu mwingine azijue habari za marekani unataka uzijue wewe pekeyako...wasukuma ninyi ni washamba sana na wabinafsi mno
Hujagundua chochote.

Unaweza kuniambia senator votes ndo nini kuhusiana na uchaguzi wa Rais Marekani?

Usiumie moyo unapoona najua kitu flani ambacho labda wewe hukijui 🤣.

Hakuna senator votes zinazomchagua Rais wa Marekani.

Unabisha?
 
Japo Kamala Harris Hana ushawishi mkubwa sana Kama Donald Trump, lakini ni vyema Sana kwa Wananchi wa Marekani wamchague Mama huyu kuwa Rais wao, Trump atawatia misukosuko sana endapo kama watamchagua tena kuwa Rais wao.
Ishu ya uhamiaji , hata pia ishu za LGBT trump zinamtafuna
 
Trump anarudi White House.

Huyu makamu ni swala la muda atajua haiwezekani.

Trump yeye anahubiri ni America kwanza. Ana mapungufu mengi lakini..
Acha Trump aje aisafishe dunia turudi kwenye mstari.

Ni sawa na jiwe alisema Tz kwanza thou alikuwa na mapungufu yake but
 
Back
Top Bottom