Tetesi: Tsh Bilioni 425 za Mwekezaji zadaiwa kuzuiliwa Tanzania, Kenya yamshawishi ahamie kwao

Hapo kuna tatizo na hao shareholders wa ndani. Tatizo la JF hii habari ipo mwaka mzima na inaandikwa nusu nusu kukidhi matakwa ya wanaoneemeka na huo mradi. Wasitutishe kuondoa pesa zao tumejipanga vizuri wala hatutetereki wengine wawekezaji watakuja kama wao wameamua kudhulumiana.
 
Spasiiba Residentura
 

Hivi unajua sehemu iliyokuwa ya kijinga hata benki nyingi kutaka kuja ni tanzania kutokana na ushenzi uliokuwepo zamani,dunia nzima tanzania ndio benki zenye riba za ajabu sehemu kote hakuna.sheria ikifatwa malalamiko lazimo yawepo kama ulikuwa mshenzi
 
Hivyo visingizio vya Alshabab mara ugaidi ndiyo hutumika kuharalisha ushetani wa kupora pesa za watu kwa njia haramu za kishamba mno, Nchi kibao hawana vikwazo vya fedha na hakuna ugaidi Malawi Zambia Bank kuu hawana vikwazo Mbona hakuna ugaidi, kwa Taarifa yako magaidi hawapendi kuweka pesa zao Bank hutembea na cash na wanajua kusafirisha pesa zao kwa njia zote pasipo kujulikana, acheni kutumia visingizio vya kishamba kupora watu pesa zao
 
Mfumo wa kibenk Tanzania ni wa hovyo bado hata watu wengi hawana imani na bank kabsa,
 

Umesoma au umeadithiwa kijiweni na baa,ushafika hata mipakani na kujua kiasi cha pesa au unazani pesa unabeba tu kama nguo za kwenda kugawa sikukuu.
Maada za kahawa mbaya
 
Tuwakumbushe watawala wa Afrika kuwa kushika hatamu haukufanyi ugeuke kuwa injinia, daktari, mhasibu, mwanasayansi au mtaalam zaidi! Power doesn’t suddenly increase your knowledge or qualify you to be anything more than you were! Waache u-much-know wawe humble!
 
Habari hii ina zengwe mbona inamtaja mwekezaji kwa majina yote na familia yake lakini haiwataji hao wawekezaji wazawa......it smells fishy somewhere.

Kuna jambo kubwa ndani ya hii issue nahisi kuna wakubwa walitaka kutakatisha pesa zirudi nyumbani.

Sasa mnatumia hizi magazeti zinazoishi kwa michongo kuitisha serikali...eti wakenya wanawashawishi???

Kwa magufuli hakuna kona kona lazima kuna tatizo mahala tena kubwa tu mambo ya richmond enzi hizo
 
Hamisha tu tanzania ilikuwepo kabla yako na itaendelea kuwepo hata ukihama wewe kabisa na sio biashara tu.
 
habari y kuibiwa kura kwenye uchaguzi imekosa mvuto sasa mnahamia huku, huyo mwekezaji mwambie ahame hata kesho maana sio lazima kila mwekezaji awekeze tanzania tu hata somalia na sudani kusini wanahitaji wawekezaji, mwambie akaangalie fursa huko pia pia, tanzania ilikuwepo, ipo n itaendelea kuwepo.
 
Ati nji ya Viwanda......!!!
Huku CCM wanazuia au kuwachelewesha mwekezaji wa Viwanda.....!!!
 

Hayo ni majibu ya kihuni toka vijiweni. Uwekezaji unahitaji mazingira rafiki na diplomasia ya Hali ya juu!
 
Kuna mzungu mmoja aliwekeza milions of dollars kule kigoma kwenyemradi wa solarpannel kwa ajili ya kuiuzia umeme tanesco yaliotokea yanafurahisha
 
Ficheni ujinga wenu. Pesa isiyo na maelezo ingewahusisha BOT na TIC?? Kama mlikuwa na shida zenu mkala pesa za watu semeni sio kuleta visingizio
 
Mfanya biashara Ramadhani Ntunzwe aliongea hadharani mbele ya wenye nchi lakini bado analia na kusaga meno.
 
Hii story kwanini itoke leo,kwanini hatukuisikia kipindi Cha uchaguzi?
Biashara zimeanza kufungwa,na hili linaibuka?kwanini leo?na sio Jana?au ni mwendo wa kuchafuana tu

Tukitathmini yanayofanywa chini uongozi huu wa awamu ya tano, bado stori iko relevant. Haijalishi stori imetoka lini, swala hapa nikuona yanayofanywa na watendaji na namna ya kuondokana na mawazo mgando.
 
THE UNITED REPUBLIC OF GANGSTARS.

Watanyang'anya kwa kila mtu. Subiri wakati ufike.
 
Hujui kitu mamlaka zinazoweza kuzuia pesa yoyote iliyoko kwenye account za benki kwa mujibu wa sheria zetu ni law enforcement agencies (Police and PCCB) na mahakama tu and not otherwise!
Endelea kukalili madesa ya nyambali nyangwine
 

Na mbna unakimbilia kutoa conclusion kabla hujapata reason, we unadhan kila investor ni angel investor wengine wanatafuta namna ya kusafisha pesa zao waweze kuzirudisha nchini kwao. na wengi sana hua wanajifanya ni charitable organisations!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…