Tsh. Bilioni 6.7 zatengwa kufadhili Wanafunzi 640 kwa 100%, ambaye hatafikisha GPA 3.8 ufadhili unasitishwa

Tsh. Bilioni 6.7 zatengwa kufadhili Wanafunzi 640 kwa 100%, ambaye hatafikisha GPA 3.8 ufadhili unasitishwa

Kila siku kununua vitu kipya badala kuendeleza vilivyopo kwa nia kutafuta sifa binafsi ya mtu. Kuona shule za kata zinazosaidia watu wengi zaidi hazina waalimu wala vifaa vya kufundishia. Shule hazina chakula. Mnataka misaada ya kibaguzi. Kuwabagua watoto kwa misingi ya akili ni dhambi. Watoto watakaopata misaada ni wale baba zao wana uwezo wamesoma shule binafsi za bei ghari. Hizo ndizo zenye waalimu bora zaidi kwa kuwa walipwa vizuri, wana vifaa na maabara nzuri. Shule za kayumba hazina hata burns burner hawezi kulipia tuition topic moja atafaulu wapi?
Pili wengi wataishia njiani kwa sababu mazingira waliosoma sekondari ni tofauti na vyuoni kwetu. Wengi wanashinda wakifika vyuoni. Huu ni usanii mtupu. Hawa Maraisi wetu wetu waliofeli sana shule ndiyo wanawawekea masharti magumu wanafunzi kama kuwakomoa. Uzoefu unaonesha wengi wao waliosoma shule za binafsi wakifika vyuo wanashuka hivyo hawatapata GPA ya 3.8 na siyo rais kupata GPA hiyo kwa masomo ya science
 
Huna akili. Hivi unajua kuna wanafunzi wengi wana uwezo darasani lakini wanashindwa kuendelea na masomo yao kwasababu ya umasikini wao?
Ni busara wangeanzia chini sekondari kuliko na watu zaidi hao waliofaulu form six si masikini ni matajiri. Nani atafaulu masomo bila tuition tena kwa mada moja moja
 
Kila siku kununua vitu kipya badala kuendeleza vilivyopo kwa nia kutafuta sifa binafsi ya mtu. Kuona shule za kata zinazosaidia watu wengi zaidi hazina waalimu wala vifaa vya kufundishia. Shule hazina chakula. Mnataka misaada ya kibaguzi. Kuwabagua watoto kwa misingi ya akili ni dhambi. Watoto watakaopata misaada ni wale baba zao wana uwezo wamesoma shule binafsi za bei ghari. Hizo ndizo zenye waalimu bora zaidi kwa kuwa walipwa vizuri, wana vifaa na maabara nzuri. Shule za kayumba hazina hata burns burner hawezi kulipia tuition topic moja atafaulu wapi?
Pili wengi wataishia njiani kwa sababu mazingira waliosoma sekondari ni tofauti na vyuoni kwetu. Wengi wanashinda wakifika vyuoni. Huu ni usanii mtupu. Hawa Maraisi wetu wetu waliofeli sana shule ndiyo wanawawekea masharti magumu wanafunzi kama kuwakomoa. Uzoefu unaonesha wengi wao waliosoma shule za binafsi wakifika vyuo wanashuka hivyo hawatapata GPA ya 3.8 na siyo rais kupata GPA hiyo kwa masomo ya science
Umeongea point. Ubaguzi siyo issue
 
Hizi hela watafute best brains wawapeleke kwenye world class universities tuwe na wasomi wa kidunia.
Hapo tutaweza hata kulinda na kutumia vema rasilimali zetu.

Tukubali madhaifu yetu tujipangie mikakati ya kujikomboa yuweze kushondana kwa kujiamini. Majirani zetu Rwanda na Kenya, hata Uganda wamejitawanya duniani huko kusaka fursa nasi tuamke.

Tupeleke vijana huko nje wakaibe teknolojia watuletee huku. Haijalishi watabaki huko au watarudi nyumbani, yote mawili ni neema kwa nchi.


Waziri Mkenda tafadhali dimamia hili!!
 
Badala mtoe ufadhili watu waende Marekani na Ulaya ili tupate watu wa kuleta ushindani Duniani huko mnatoa ufadhili wasome vyuo vyetu hivi hohe hahe.

Alafu kesho mnasema tunawasomi wa hovyo.
MABEBERU HATUTAKI, watoe ufadhili twende kwa marafiki zetu wapya, Iran, Syria, Afghanistan na Russia.
 
Mwaka wa Fedha wa 2022/2023 Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilianzisha ufadhili kwa wanafunzi wanaohitimu Kidato cha Sita wenye ufaulu wa juu katika tahasusi za sayansi (PCB, PCM, PGM, CBG, CBA, PMC na CBN) waliopata udahili katika fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, Hisabati na Tiba kwenye vyuo vya Elimu ya Juu nchini.

Ufadhili huu unajulikana kwa jina la SAMIA SCHOLARSHIP. Lengo la ufadhili huu ni kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya sayansi ili hatimaye taifa lipate rasilimali watu ya kutosha kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya nchi na watu wake.

Akizungumzia hilo Waziri wa Wizara hiyo, Profesa Adolf Mkenda, leo, Julai 27, 2023 amesema wakati huu ambapo wahitimu wa kidato cha sita wakiwa wanajiandaa kwenda katika masomo ya juu kuna fursa hiyo ya kutuma maombi kwa ajili ya kupata ufadhili huo kwa asilimia 100 (100%).
View attachment 2720606
Profesa Adolf Mkenda

Amesema Serikali ilitenga Tsh. Bilioni 3 kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 na jumla ya Wanafunzi 636 walinufaika na ufadhili huo, Wanawake wakiwa ni 231 (41%) na Wavulana 375 (59%), pia kulikuwa na Wanafunzi 12 wenye mahitaji maalum walifanyiwa tathimini peke yao nao walinufaika.

Ameeleza kuwa katika mwaka huo uliopita walisajiliwa na kudahiliwa katika Vyuo 18 Nchini ikiwepo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).
View attachment 2700490
Akizungumzia mchakato mpya katika Mwaka wa 2023/2024, Serikali inatarajiwa kutoa ufadhili kwa wahitimu wa kidato cha sita takribani 640, jumla ya Tsh. Bilioni 6.7 zimetengwa kuwagharamia wanufaika wanaoanza na wanaoendelea na hivyo kufanya jumla ya wanufaika ambao watakuwa vyuoni kuwa 1,276.

Amesema "Ufadhili huu ni kwa masomo ya Shahada ya Kwanza kwa wanafunzi waliopata ufaulu wa juu katika Mitihani ya Kidato cha Sita mwaka 2023 inayoendeshwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) katika tahasusi za Sayansi kama zilivyoainishwa hapo juu.

"SAMIA SCHOLARSHIP inagharamia kwa asilimia mia moja (100%) masomo ya Chuo Kikuu kwa Wanafunzi hao ambao wamepata udahili katika fani za Teknolojia, Uhandisi, Hisabati na Tiba.

“Masharti ya ufadhili kwa wanaoendelea kusoma chini ya Ufadhili wa Samia, wanatakiwa wasishuke ufaulu wa GPA 3.8, watakaoshuka hapo wataondolewa kwenye ufadhili na kuingizwa kwenye mikopo ili waendelee kusoma.

“Tunahimiza wanaopata ufadhili waendelee kuonesha ufaulu wao wa kidato cha sita ulikuwa wa haki.”

Ameongeza kuwa majina ya watakaoteuliwa yatakuwa wazi, ufaulu wao utakuwa wazi pia, vigezo vipo wazi na majina yao yatawekwa kwenye tovuti ya Wizara.

Katika Wanafunzi 640 wapo ambao hawatataka kufanya masomo ya Sayansi watalazimika kuomba mkopo wa kawaida, watakaoenda nje ya nchi kwa sasa ufadhili huo haufiki huko, hivyo kukitokea nafasi watachukuliwa waliochini ya wale walioteuliwa awali.
View attachment 2700489
Katibu aelezea
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Prof. Carolyne Ignatius Nombo amesema vyuo vilivyonufaika kwa kuwa na Wanafunzi hao ni Vyuo Vikuu vya Serikali ni 13 wakati Vyuo Vikuu visivyo vya Serikali ni vitano.

Vyuo vilivyokuwa na idadi kubwa ya wanufaika ni MUHAS walikuwa na Wanafunzi 233 ambayo ni 36% huku UDSM wanufaika wakiwa ni 311 (48%).

Amesema “Ufadhili huo unazingatia Ada ya Mafunzo, Posho ya chakula na malazi, Posho ya Vitabu na Viandikwa, Mahitaji Maalum ya Vitivo, Mafunzo kwa Vitendo, Utafiti, Vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu na Bima ya Afya."

Maombi ya Samia Scholarship yatawasilishwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa njia ya mtandao https://olas.heslb.go.tz kuanzia Jumatatu, Septemba 25, 2023. Hii inatokana na ukweli kwamba katika kipindi hicho kila mwanafunzi atakuwa amepata udahili katika chuo cha Elimu ya Juu nchini.

"Wizara inahamasisha Wanafunzi wote nchini kuendelea kupenda na kujiimarisha katika masomo ya Sayansi na hatimae kujiunga na Elimu ya Juu katika programu za Sayansi, Teknolojia Uhandisi na Hisabati (STEM) ambapo watanufaika na mpango huu mahsusi," amesema.

Tanzania ndio nchi pekee ambayo ukifuatilia, ukichambua, ukidadavua baadhi ya maamuzi yake tena ya kitaifa na kwenye sector kubwa na nyeti unaweza kutoa machozi. Hivi malengo na madhumuni ya Board loarn yalikuwa ni nini? na malengo na madhumuni ya hii Mama Samia Loarn ni nini? Ebu nipeni utofauti. Sioni tofauti zaidi ya kuchukua selection criteria iliyokuwa ikimzuia mtoto aliyetoka familia tajili kutopata mkopo 100% from Laon boards na kumtengenezea njia mbadala ya kupata mkopo 100% tena kwa uhakika kuliko wale wengine.

Wote tunajua more than 85% ya wanaofaulu vizuri wanatoka shule bora, shule za kishua, shule za wazazi wanaojiweza, nyingi kama si asilimia 95% basi na zaidi ni shule za private. Sasa hawa walikuwa hawa meet preliquesite qualification za Nationa Loan Boards, tumewatengenezea njia mbadala wa kufadhiliwa nje ya Loan board , tena bila usumbufu wa wenzao. Hiyo ndio Tanzania.

Hivi lengo sasa ni inclusion or exclusion, na fairness? na equality iko wapi kwa walio watanzania wengi ambao watoto wao wengi wana division II na kuendelea. Kwanza unajua karo ya private nyingi kwa mwaka ni zaidi ya fees na matumizi ya vyuo vikuu vingi kwa mwaka?, kwa hiyo huyu mzazi hasingeshindwa kumlipia mtoto wake. Ebu nambie mzazi wa kajamba nani Nyamtumbo, Tanganyika Katavi, Karagwe Kagera ambaye ameuza sehemu ya kiwanja kumsomesha mtoto wake mpaka form six, tunataka auze nini kilichobakia. Kweli nimekubali kazi na iendelee.
 
Back
Top Bottom