TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Naona imekufa sasahivi hata ukimwita fundi hafiki.
Ni shida kwelikwe
 
Shirika lina wazee tupu, almost wote, hawawezi kwenda na uhitaji wa sasa..!!
 
TTCL Naona imekufa sasahivi hata ukimwita fundi hafiki.
Ni shida kwelikwe
Uzembe umetamalaki watu hawafanyi kazi wanaenda ofisini kupiga soga kitu cha kufanyika ndani ya dakika kadhaa kinachukua miezi kadhaa shirika litatengeneza vipi faida kwa mwendo huo hakuna mteja atataka huduma zao maana ni mbovu kupindukia halaf unasubirishwa bila sababu za msingi
 

TTCL pamoja na gharama zote za kutandaza Fibre Mpaka maporini mnashindwa unganisha watu mjini?

Kweli nyie ni watu wa hovyo.
 
Sahihi kabisa lakini hata vijana wapo ila nao washakuwa kama wazee hawajali bora liende tu
Niseme kitu kimoja, si unawaona wale madereva wa viongozi walivyo na nidhamu kwenye kazi zao, sasa siku dereva huyo huyo wa kiongozi, akihamia kwenye kuendesha bodaboda, naye atakuwa kama walivyo madereva wengine wa bodaboda. HIVYO HATA HAO VIJANA WALIOKO TTCL LEO, wanaharibiwa na wazee waliopo pale. Sasa ukute mzee ndiyo bosi, ni hatari zaidi.

Binafsi nimefanya kazi kwenye private telecom company, nawajua TTCL. Maana nikiwa huko, tulishawahi kukodi tower space, power, ground space na E1 zao. Ni ujinga mtupu. Yaani hadi kuandika invoice ili uwalipe nako mpaka mpigizane kelele za maana...!!! Sasa kulipwa wao ndo wanafanya hivyo, FIKIRIA WAO KUWALIPA WENGINE INAKUWAJE..!!!
 

Alooo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Sasa ndio naelewa kwa nini wanadeni la kudai na hawajua wa kumdai.

Anyway nimesikia wameanza kuwafungia watu kipindi cha pasaka hapo.
 
Masikitiko makubwa Sana wengi wa wafanyakazi wa TTCL hawapaswi kukalia vitu walivyokalia wanapaswa wawe nje ya ajira uzembe hauna mfano unawaletea pesa bado wanajivuta wataweza kuendesha shirika kwa faida na ushindani? Survey ya dakika 2 tena kwa google map inachukua miezi 6 hapo kuna shirika la faida kweli ? Shirika linapaswa kuwekewa chini ya mikono sahihi wavaa suti na warsha zisizoisha utendaji sifuri ondoa wote
 
TTCL pamoja na gharama zote za kutandaza Fibre Mpaka maporini mnashindwa unganisha watu mjini?

Kweli nyie ni watu wa hovyo.
Ajabu kweli walipaswa wawe namba moja kwenye huduma ya fiber internet tena kwa gharama za chini zaidi ili kuvutia idadi kubwa ya watumiaji wa internet na kufanya biashara nzuri zaidi nchi nzima lakini eti ukifika ofisini kwao wanakwambia vifaa vichache bila hata aibu utapata huduma baada ya miezi 2/3 Yan ningekuwa na huo uwezo fukuza wote hao
 
Mkuu umetoa povu bure! Hebu muulize Shareholder wa TTCL amewekeza shilingi ngapi kwenye hiyo miradi au TTCL ina struggle kutoa huduma kutoka kwenye own Source ambayo haitoshi?
Pili iulize Serikali kwa nini TTCL ikitaka kununua materials inatakiwa ku comply na sheria za PPRA ambazo ni very bureaucratic kiasi kwamba service delivery kwa mteja inachelewa?
Hao wafanyakazi unaowalaumu ndio waliofanya Shirika likawepp mpaka leo licha ya kupitia misukosuko mingi ikiwemo kubinafsishwa.
Iulize Serikali TTCL inapata unafuu wowote kwenye Kodi kama Shirika la serikali au na lenyewe linalipa sawa na wengine?
Anza na hayo kwanza halafu ukipata majibu rudi kwenye hili povu lako
 
Acha kutetea ujinga yani unasifia uzembe wa wafanyakazi eti ndio wamelifikisha shirika hapo lilipo kitu cha kufanyika dk 3 kinawachukua miezi mpka 6 mfano survey, google map mteja anatuma eneo alipo ili kujua kama huduma zinafika eneo lake halaf unasema natoka povu huu uzembe ndo unauwa mashirika ya umma. Kwanini ipate unafuu wa kodi kama inafanya biashara mbona taasisi binafsi zinamudu na kodi zinalipa? Swala la manunuzi ni uzembe ule ule tunaongelea hapa kama mzabuni yupo tayari inashindikana kitu gani kuagiza vifaa vingi zaidi ili kuondokana na upungufu au ndio kufanya kazi kwa mazoea halafu unakuja na utetezi usio na msingi hapa? Tunataka huduma hatutaki visingizio hapa.
 

Hizi ni za ndani ndani sana.

Anyway tumekuelewa ila jitahidini basi kushirikiana na wananchi vizuri maana kuna mtu anasema baadhi ya vifaa anavyo lakini mnakataa then anakaa miezi 8 hajafungiwa huduma.

Jitahidini kuwashawishi kitengo cha project juu ya hii fursa ya Fiber mlangoni kwako. Mitandao mingine wanaitamani sana.
 

Naona wote mmeamua kupanic na hujataka kuelewa hata kitu kidogo alichokisema.

Bro ukimaliza kupanic njoo kwenye queue ya waitlist wengine tuna miezi 8 tumeona tujifunike na mwamvuli wa Supakasi japo unaumiza ila maisha yanaenda.
[emoji125]
 
Huduma ya fibre ni mwaka sasa nimelipia ila connection haipo wala majibu hakuna ttcl mwanza
Hawa jamaa wanasikitisha Sana huduma mbovu haijapata kutokea halaf mkurugenzi na tai yake yupo tu anapigwa kiyoyozi bila wasiwasi​
 
Mbona zoezi la fibre linaenda taratibu sana nimeomba maombi ya internet kwa kujaza form lakini haijulikani ni lini wanakuja akufunga nipo Bagamoyo
 
Mbona zoezi la fibre linaenda taratibu sana nimeomba maombi ya internet kwa kujaza form lakini haijulikani ni lini wanakuja akufunga nipo Bagamoyo
Mi nimeandika email, kupiga simu, kutext mpaka nimeamua kuacha tu.. Nadhani hawapo tayari kupokea wateja wapya. Taasisi za serikali tabu sana
 
Mi nimeandika email, kupiga simu, kutext mpaka nimeamua kuacha tu.. Nadhani hawapo tayari kupokea wateja wapya. Taasisi za serikali tabu sana
Hili shirika nafikiri ni kama linalazimishwa kutoa huduma hawako tayari wanahudumia wanavyojisikia wao hivi mkurugenzi yupo tu ofisini hashtuki hata malalamiko ni mengi kila uchwao halaf kibaya zaidi yanayofanana wameshindwa kabsa kuyafanyia kazi wameachia bora liende na mishahara wanalipwa.​
 
Kiukweli wanapata mishahara ya bure tu hakuna wanalolifanya. Inasikitisha sana na wenye mamlaka wamekaa tu kimya unashindwa hata kuelewa kuwa hivi hii nchi ina laana au ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…