TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

Jana kuanzia saa3 hadi usiku mnene hawakuwa na internet kabisa.asubuhi imerudi lakin bado ni 3G.

TTCL badilikeni bwana mnaboa,sio mpaka magufuli aje atumbue.

Jiwe nae kama anatumia TTCL naamini anaona huu uozo.

Sent using Jamii Forums mobile app
dah! nilifikiri peke yangu ndio nimekutana na kadhia hiyo...... hata mida ya mchana huduma yao ilikuwa inapotea.

namshukuru Mungu jana usiku sikujiunga na kifurushi chenye mgawanyo wa muda kama bandika bandua (huenda ningelikata laini kwa hasira).

Baharia Wa Buza tunaomba utufikishie malalamiko yetu huko makao makuu, wewe pekee ndiye unayesikilizwa🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
nilinunua 4G USB DONGLE ya TTCL sikufanikiwa kuitumia hata mara moja pamoja na kujaribu kuitumia katika vifaa tofauti tofauti haijawahi kunipa ushirikiano!nilipo waendea wahusika wakadai kifaa changu hakiko sawa licha ya kuwaeleza kuwa nimejaribu kutumia kwenye vifaa vingine bila mafanikio bado haikusaidia kitu.
 
Sio siri ngoja niende kwenya mada moja kwa moja.

Huu mtandao una matatizo mengi sana kama yafuatayo:

1. Huduma ya T PESA
Aisee huu mtandao kama utatuma hela siku ya Ijumaa usiku ghafla litokee tatizo wallah utakuja kuhudumiwa siku ya Jumatatu.

Hili tatuzo limenipata juzi hapa Ijumaa tarehe 7 yaani nilitamani kulia wallah.

2. Vifurushi
Hawa majamaa ukitaka uende nao sawa kwenye masuala ya MBs nakushauri tafuta kitambulisho cha chuo.

Aisee yaani GB 5 kwa Tsh 5000 mwezi mzima.

3. Vocha
Asikwambie mtu, TTCL hawana vocha aisee. Jana nimeenda pale Makao Makuu niliulizia vocha ya 500 hakuna wanasema zipo za 1,000.

Aisee ukienda kuulizia madukani yaani muuzaji anaweza akashangaa maana hiyo vocha ya TTCL ndiyo kwanza anaisikia kwako.

Kilichonipata jana
Nilijiapiza nikaonane na Afisa Masoko pale Makao Makuu pale Posta ili nimshauri kitu kimoja tu. Yaani nikafika mapokezi nikaonane na bwana Kindamba lakini nikazuiliwa.

Yule mama wa mapokezi aliongea sana mpaka wakati naondoka nimeinamishwa kichwa chini kwa masikitiko. Maana shida yangu nilitaka kuonana na Afisa Masoko au CEO wao.


Nilitaka niwambie kama vocha mtaani ni ngumu basi katika option ya kununua bando mteja achague alipe upitia T PESA au salio la kawaida.
Mnatafuta nini huko mashenzini?
 
dah! nilifikiri peke yangu ndio nimekutana na kadhia hiyo...... hata mida ya mchana huduma yao ilikuwa inapotea.
namshukuru Mungu jana usiku sikujiunga na kifurushi chenye mgawanyo wa muda kama bandika bandua (huenda ningelikata laini kwa hasira).

Baharia Wa Buza tunaomba utufikishie malalamiko yetu huko makao makuu, wewe pekee ndiye unayesikilizwa🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
ucwaxe
 
TPESA
Huduma ya TPESA changamoto ziko ila zinashughulikiwa, changamoto za kimtandao zipo kwa operators wote ila la kupata tatizo Ijumaa kushughulikiwa ndani ya siku za kazi ni kweli, TPESA wanahitaji kubadilika

Vifurushi
TTCL wanahuduma nzuri sana kulinganisha na other operators, linganisheni vizuri and fairly

Vocha
Kunachangamoto ya upatikanaji wa vocha za kukwangua lakini unaweza pata vocha kupitia selcom, tingApp, tigo, voda airtel, CRDB, NMB etc, sometime unajiongeza

Kilichokupata jana
sometime Lugha za matusi sio heshima, Mungu kila mtu kampa sura yake kutukana mama zetu sio jambo zuri. je baharia wa buza nikikuambia mama yako anasura NGUMU utajisikiaje????Kumbuka udada zako, unashangazi zako, una mama wadogo.
Hapo uliposema unajiongeza, kama ttcl ndio falsafa yao ktk utoaji huduma naweza kusema ndio mtandao wa hovyo kabisa na hautatoboa kibiashara.

.
 
Jana usiku nimejaribu kustream na ttcl 4G hakuna chochote. Niliwasha data na ikasoma 4G ila kwenye data traffic ikabaki 0 kb/s mwanzo mwisho.


Nini shida TTCL? Au nyumbani kumegeuka kuchungu?

Sent using Soviet T-72 Main Battle Tank
 
Alhamisi nimefika makao makuu nikataka wanisajilie Special namba,,wakanambia anaehusika na kutengeneza special namba kaenda likizo hadi 20/04/ ndo atakuwa ofisini,,nikawaambia nataka huduma ya TPESA niwe wakala wakanambia nitoe leseni,tin,id nikawapa ajabu wakanambia mkataba wa kujaza umewaishia nikawauliza ina maama kwenye computer zenu hakuna copy wakanambia hakuna mpaka sijui baada ya Pasaka maana pia hswana RIM PAPER

hapo ni makao makuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alhamisi nimefika makao makuu nikataka wanisajilie Special namba,,wakanambia anaehusika na kutengeneza special namba kaenda likizo hadi 20/04/ ndo atakuwa ofisini,,nikawaambia nataka huduma ya TPESA niwe wakala wakanambia nitoe leseni,tin,id nikawapa ajabu wakanambia mkataba wa kujaza umewaishia nikawauliza ina maama kwenye computer zenu hakuna copy wakanambia hakuna mpaka sijui baada ya Pasaka maana pia hswana RIM PAPER

hapo ni makao makuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Posta au
 
Mtandao unaowajali wateja.
Mtandao wa Nyumbani.
Upo tayari kupata hasara kwa sabb ya wateja wake
 
Back
Top Bottom