Tuache kudanganyana, Ajira zina afadhali zaidi kuliko kujiajiri, watu wengi waliojiajiri ndio wapo kwenye utumwa

Tuache kudanganyana, Ajira zina afadhali zaidi kuliko kujiajiri, watu wengi waliojiajiri ndio wapo kwenye utumwa

Najua kwa haraka haraka mtafikiria kunijibu kwamba "Mwajiri hawezi fikia mafanikio ya Mo ai Bakhresa" ....vuta pumzi tulia!! Hao kina Mo watoe akilini mwako maana wapo kundi tofauti kabisa ni wafanyabiashara waliofikia mafanikio ya biashara zao kujiendesha hata wakiwa wamelala.

Mtu mwenye ajira hapa bongo serikalini ana nafuu zaidi maana mwisho wa mwezi mwajiriwa ana uhakika ila aliejiajiri ni juhudi zake, akipoteza mda imekula kwake.

Mwajiriwa hata akifiwa, akiumwa, akioa/kuolewa, anapewa kalikizo.. hapo kila jumamosi na jumapili yupo free, bado ana likizo ya mwezi moja kila mwaka, sherehe za serikali na za dini haendi kazini, Ana muda mwingi wa kuweza kupumzika na familia na kufanya shughuli za kijamii.

Wafanyabiashara wengi nawajua tangu nimepata akili za kuijua dunia mpaka leo hii wao siku ya kupumzika ni christmas tu, wenye nafuu huwa wanapumzika jumapili pekee, siku zingine hizo ni bampa to bampa wanaondoka alfajiri wanarudi usiku, yani hata muda wa kuspend na watoto hawana,

Ukiwa kwenye ajira unaweza kujiajiri pia

Nani mtumwa hapo
sijawahi na sitaki hata kuajiriwa na wala sjatoka familia ya kishua but mishe nazopiga kukunja 5m to 10m kawaida sana kwa mwezi

But mpaka nimefikia level hii ni kwamba nimepmbana kwa jasho na damu mzee japokuwa sometime nakula loss mpaka ya 6m but still fighting

kujiajiri kutamu mno sema kunamtaka mtu mwenye roho ya paka
 
Kwa upande wangu kujiajiri ni bora maana nimefanya hivo miaka yote japo changamoto zipo, lakini unakabiliana nazo tu, tena kwa nchi zetu za dunia ya tatu ni afadhali kujiajiri maana hata fursa ni nyingi wakati kwenye dunia ya tatu kuajiriwa malipo ya waliowengi hua ni kidogo sana
 
Jiulize swali kwanini wenye mshahara wa 700k hawana uwezo wa kuwa na akiba ya 100k Kwa mwezi.mshahara hauwezi kukuta 10k ya mshahara mwingine .Kiufupi ukiwa kwenye ajira na unalipwa chini ya million tofauti yako na mama siwema anayechoma vitumbua vya miatano miatano ni ndogo sana ,utamzidi kuvaa ,madeni , kukopa kwenye vikundi na saccos.
Mtu anaelipwa 700k halaf hela haikut mwezi ujao labda wenye sekta za ovyo kuna watu wana marupurupu huo mshahara hawaugusi yaan wapo humo serikalin so msikariri
 
kotekote kuzuri tu kama umekaa pazuri.

Sasa kama umeajiliwa na kazi unaijua na mshahara wako kwa mwezi ni 15m net au zaidi unashida gani zaidi ya kuenjoy.

Kama umejiajili na una kipato cha 15mil na zaidi kimesimama shida nini.. hapo ni kipato tu.
 
Mtu anaelipwa 700k halaf hela haikut mwezi ujao labda wenye sekta za ovyo kuna watu wana marupurupu huo mshahara hawaugusi yaan wapo humo serikalin so msikariri
(Halaf ,Haikut,serikalin,so )rekebisha hayo maneno Kisha tuendelee na mjadala husika itakuwa ngumu sana Kwa mtu kama wewe kuweka akiba kutokana na mshahara wakati hayo maneno yanakushinda kuandika.
 
sijawahi na sitaki hata kuajiriwa na wala sjatoka familia ya kishua but mishe nazopiga kukunja 5m to 10m kawaida sana kwa mwezi

But mpaka nimefikia level hii ni kwamba nimepmbana kwa jasho na damu mzee japokuwa sometime nakula loss mpaka ya 6m but still fighting

kujiajiri kutamu mno sema kunamtaka mtu mwenye roho ya paka
Wewe utakua dalali wale wanaosumbua watu wanaotaka kuuza nyumba zao na viwanja vyao.
 
Najua kwa haraka haraka mtafikiria kunijibu kwamba "Mwajiri hawezi fikia mafanikio ya Mo ai Bakhresa" ....vuta pumzi tulia!! Hao kina Mo watoe akilini mwako maana wapo kundi tofauti kabisa ni wafanyabiashara waliofikia mafanikio ya biashara zao kujiendesha hata wakiwa wamelala.

Mtu mwenye ajira hapa bongo serikalini ana nafuu zaidi maana mwisho wa mwezi mwajiriwa ana uhakika ila aliejiajiri ni juhudi zake, akipoteza mda imekula kwake.

Mwajiriwa hata akifiwa, akiumwa, akioa/kuolewa, anapewa kalikizo.. hapo kila jumamosi na jumapili yupo free, bado ana likizo ya mwezi moja kila mwaka, sherehe za serikali na za dini haendi kazini, Ana muda mwingi wa kuweza kupumzika na familia na kufanya shughuli za kijamii.

Wafanyabiashara wengi nawajua tangu nimepata akili za kuijua dunia mpaka leo hii wao siku ya kupumzika ni christmas tu, wenye nafuu huwa wanapumzika jumapili pekee, siku zingine hizo ni bampa to bampa wanaondoka alfajiri wanarudi usiku, yani hata muda wa kuspend na watoto hawana,

Ukiwa kwenye ajira unaweza kujiajiri pia

Nani mtumwa hapo
Huu ushauri ungeenda kuutoa kwa Waajiriwa wenzako
 
Kujiajiri hupelekea kila siku unaumiza kichwa na kupata pressure za ajabu ajabu juu ya biashara yako. Ndo maana wengi wao huzeeka mapema.

Hali kadhalika mawazo na hofu juu ya mwenendo na maendeleo ya biashara yako.

Kujiajiri kumesababisha watu wengi sana kuwa wachawi kwa ajili ya kuboresha vipato vyao.

Kujiajiri ni safari ya kupanda na kushuka, na pia haieleweki na hata Maendeleo ya watu wake hayaeleweki pia.
Na kikukweli wengi waliojiri ndio watumwa wa biashara zao.
Ushauri wa kijinga sana huu,
 
Twende Mbele turudi nyuma, saiz kila mtu anapambana aajiriwe kwanza, hayo mambo ya kujiajiri yanakuja baada ya kuajiriwa.
Sio kila mtu.
Ajira inategemea mshahara kwakweli. Kuna mtu anataka kukupa kazi unapiga hesabu unaona hii ajira haifai bora niendelee na mishe zangu sio kuchukua gross sijui 800k.
Ila kuna ajira zina mshahara na marupurupu yani huwazi mara mbili
 
Uzuri wa kujiajiri kipato kina leverage ila lazima ukumbane na ups and downs lazima ukubaliane nazo.

Kuna hatua ya kujiajiri unafikia angalau unapumbua na hapa lazima uwe nawe umeajiri watu wako wa kukufanyia kazi.

Kuajiriwa ni kuwa na mipaka ya kipato na kama ni kidogo utajamba cheche maana kama matumizi na gharama za maisha zinapanda daily ,lazima uwe smart kujiongeza pembeni
 
Back
Top Bottom