Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 7,899
- 10,415
- Thread starter
-
- #61
Kwanini boss
Tanzania tatizo ni elimu yetuUjinga ni mwingi.
Science literacy ni zero.
Kwani mliwekeza nini?Labda Unazungumzia vitalu vipya ila vile vya zamani hatuna chetu pale.
Ndio maana awamu ya tano wala hata haikuhangaika na hayo mambo.
Sasa mafuta yapi wakati Tz haina mafuta?Na wewe umedanganya, Dr.Slaa alisema ni mafuta na siyo gesi na wala hakusema kuna bomba la gesi kwenda ulaya.
Mkuu Meneja Wa Makampuni,Unapo zungumzia gesi ni tofauti sana na mafuta katika swala zima la uhifadhi na usafirishaji.
Gesi ya Mtwara bado ipo zaidi itaanza kuzalishwa mpaka LNG plant itakapokua imejengwa.
Hii inayozalishwa sasa ni kiasi kidogo tu.
Karibuni kwa maswali sasa
Kwa ushauri kuhusu maswala ya gesi na mafuta pia karibuni.
Lakini pia kwa uhitaji wa kuandikiwa propozo za kuanzisha miradi ya vituo vya mafuta na kudizani ramani za vituo vya mafuta vidogo kwa vikubwa karibuni pia.
Mawasiliano: +255747744895
Shukrani mkuu
Kuna mradi wa nyerere hep.Kwani mliwekeza nini?
Inaitwa gesi asilia (Natural Gas).
Mtwara tuna aina moja ya gesi asilia yenye kiwango kikubwa cha kampaundi ya methane. LNG sio aina ya gesi. Kwanza tambua kwamba LNG kirefu chake ni Liquefied Natural Gas (Gesi asilia iliyo badilishwa kuwa kimiminika).
Tambua kwamba ni gesi iliyobadilishwa kuwa kimiminika ili iwe rahisi kuifadhi na kuisafirisha kwa wingi katika umbali mrefu sana sana nje ya nchi. Ukiibadilisha gesi kuwa kimiminika ndipo unaweza kuisafirisha kwa wingi zaidi. Kipimo kimoja cha gesi asilia kinakua mara 600 ikiwa katika hali ya kimiminika.
Bado LNG haijaanza kuzalishwa Mtwara. Ili kuizalisha LNG kinatakiwa kijengwe kiwanda kinacho gharimu Trillion 70 Tsh.
Hivyo kazi kubwa ya kiwanda hicho itakua ni kuibadilisha gesi asilia kuwa LNG.
CNG kirefu chake ni compressed natural gas yaani gesi asilia iliyo kandamizwa au shindiliwa. Nayo bado ni gesi asilia ila yenyewe imeshindiliwa kwa kutumia mashine ili itumike kwenye magari.
LNG na CNG zote ni gesi asilia na zote zina kampaundi ya methane. Isipokua LNG ipo katika katika mfumo wa kimiminika na CNG katika muundo wa kukandamizwa. Lengo kuu ni kuweza kuifadhi na kusafirisha.
Ila naomba tena usichanganye LNG na LPG.
LPG ni liquefied petroleum gas na imeundwa kwa kampaundi za propane na butane.
LPG huwa inazalishwa wakati wa kuchakata mafuta ghafi (crude oil) au wakati wa kuchakata gesi asilia yenye kiwango kikubwa cha butane na propane.
LPG haipo Tanzania, huagizwa kutoka nje ya nchi. LPG ndio gesi tunayotumia kupikia majumbani (Oryx, Mihani, Taifa n.k).
Ili kupata LPG tunazikandamiza butane na propane katika mgandamizo mdogo tu (low pressure). Baada ya hapo butane na, propane zinakua kimiminika.
Ili kupata CNG tunaikandamiza gesi asilia (methane) katika pressure kubwa.
Ili kuipata LNG tunaipoza gesi asilia (methane) katika joto la (-163 °C)
ThanksYou must be working in an O&G industry for sure ! Na kemia ndio discipline yako ! Hongera sana
ThanksBi dada uko vizuri sana!
Thanks
Thanks for good commentYou display high level of professionalism with impeccable argumentation without the slightest deviation from key message! Big big up dada !!
Unanikumbusha mbali hizi issue za organic ChemistryKama ulikimbia organic chemistry na chemistry KWA ujumla kaa mbali
Meneja shikamoo,Boss anuniwi!Ila naomba tena usichanganye LNG na LPG.
LPG ni liquefied petroleum gas na imeundwa kwa kampaundi za propane na butane.
LPG huwa inazalishwa wakati wa kuchakata mafuta ghafi (crude oil) au wakati wa kuchakata gesi asilia yenye kiwango kikubwa cha butane na propane.
LPG haipo Tanzania, huagizwa kutoka nje ya nchi. LPG ndio gesi tunayotumia kupikia majumbani (Oryx, Mihani, Taifa n.k).
Ili kupata LPG tunazikandamiza butane na propane katika mgandamizo mdogo tu (low pressure). Baada ya hapo butane na, propane zinakua kimiminika.
Ili kupata CNG tunaikandamiza gesi asilia (methane) katika pressure kubwa.
Ili kuipata LNG tunaipoza gesi asilia (methane) katika joto la (-163 °C)
aaaaaaaaa mteja ni boss wa meneja lakini. 😀😀😀😀Unajua bila mteja meneja hawezi kuwa meneja.Meneja shikamoo,Boss anuniwi!
Hiyo gesi inayotumika kufua umeme Kinyerezi Dar es Salaam ni gesi asilia pia inayozalishwa katika vitalu vya Songo Songo na Mnazi Bay.Shukrani.
Hiyo gesi inayotumika kuzalisha umeme Dar es Salaam ni gesi ipi na imefikishwaje Dar?