Unaweza kuwa sahihi au usiwe sahihi kutegemea na hali, mazingira na uwezo wa watu wengine kufikiri!
Kuna umaskini wa mtu mmoja mmoja na umaskini wa taifa. Maskini ni mhitaji ambaye hana uwezo wa kutatua hitaji lake. Tofauti ya maskini na tajiri ni vitu vinavyoonekana kwa macho kama vile nyumba nzuri, magari, fedha nk.
Kuna aina nyingi za umaskini.
Umaskini wa fikra au kukosa maarifa, ni mbaya kuliko aina nyingine zote.
Hata mimi pia naamini umaskini ni laana hasa ninaposoma kumbukumbu la torati sura ya 28:1...
Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana Mungu wako...., Baraka hizi zitaambatana nawe....
Sasa kama sisi ni wasikivu na watendaji wa maagizo ya aliyetuumba, kwanini tuwe maskini???