Tuache siasa, ajira zipo za kutosha Tanzania kwa wanaojua Kiingereza kwa ufasaha

Tuache siasa, ajira zipo za kutosha Tanzania kwa wanaojua Kiingereza kwa ufasaha

Yaani nikikutana na Mswahili ambaye hata Kiswahili hawezi, simpi kazi ng'o! Halafu huwa wanakuwa na madigrii makubwa makubwa lakini haya mambo tuliyofundishwa shule ya msingi hawawezi!! Bora hata ubabaishe Kiingereza.

Wengine wanakosea maneno ya kila siku, mtu anaandika Kalibu, ongera maneno ambayo haziwezi pita siku mbili hujayaona yani kusoma hawezi na picha haoni. Mtu asiye makini kiasi hiki nani ampe kazi yake?
 
Members, Msipende kusikiliza maneno ya sisi wanasiasa kuwa lugha ya Kiswahili ni bora na elimu ya shule za kata ni bora sana.

Hakuna mwana siasa wa zama hizi ambaye mtoto wake anasoma shule ya kata au anasoma masomo ya msingi kwa lugha ya Kiswahili.

Usahili au Interview za sasa anayejua kujieleza kwa Kiingereza kwa ufasaha zaidi ndiye anayepata ajira kwenye Makampuni na mashirika binafsi.

Sekta binafsi zinahitaji watu wanaojua lugha kwa ufasaha ya Kiingereza.

Nilifika ofisi moja hapa Tanzania, hakuna mfanyakazi wa kitanzania anayoongea kiswahili, Wote wanatumia kiingereza fasaha kuanzia mlinzi nje mpaka wahudumu ndani.

Watoto wa watu wenye uwezo na waliosoma shule za kimataifa za kiingereza ndio Wanao kwenda kuongoza sekta zote nchi hii, Na hao watoto wengi ni wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wakubwa, Wakurugenzi wa taasisi na Mashirika au wale wafanyakazi wa serikali wenye mishahara mikubwa.

Vijana wa sasa wanakosa ajira kwa kushindwa kujieleza kwa Kiingereza fasaha kwenye Usahili wa mahojiano au Oral interview.

Vijana tumieni simu zenu kujiimarisha uwezo wa kuongea Kiingereza Fasaha, Degree bila kuongea Kiingereza kwa ufasaha ajira ni ngumu kupata sekta binafsi na hata taasisi baadhi za Serikali.

Kiingereza cha kufikiria maneno kama oooh, you know sir, Infact Sir. OK no problem..... The... The.... and.... OK you know... know huwezi kupata ajira kwa sasa.

Mtoto wa kihindi Tanzania wa darasa la tano anajieleza vizuri kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.

Mtoto wa chekechea Feza na Class three IST anajieleza kwa ufasaha kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.

Zamani watu walisoma shule za Serikali na waliongea Kiingereza kwa ufasaha lakini sio kwa walimu wa sasa na shule zilizopo sasa.

Shule za Tanzania hasa za serikali na baadhi sekta binafsi walimu wenyewe tu hawajui kiingereza, Je hao wanafunzi watajua Kiingereza?

Jitihada binafsi zinahitajika kwa wahitimu wa sasa kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha.

Kila siku ajira zinatangazwa za Kitaifa na kimataifa, Lakini vijana wetu wanaogopa na hata wakiomba hawawezi kufurukuta na watoto wa nchi jirani za Kenya na Uganda.

Hata sisi wakinga siku hizi familia zetu zinasoma shule za kisasa na vyuo vya kisasa nje ya nchi.

Fuatilieni scholarship vizuri muone watoto wa viongozi wanavyohangaika kuwaombea watoto wao.

Fuatilieni mashirika makubwa ya kimataifa mtawakuta watoto wa viongozi wa kisiasa huko WHO, UNICEF, WORLD BANK, UNESCO, UNHCR, CITI BANK na Bank zote za Kimataifa wapo watoto wao wanaoongea Kiingereza kwa ufasaha.

Ofisi nyingi na Bank kubwa kubwa Dar Salaam hakuna mfanyakazi wa kitanzania anaongea kiswahili ni Kiingereza tu kilichonyooka labda waamue kukuongelesha kwa Kiswahili.

Lini ulisikia watu wenye account Citi Bank, Standard chartered Bank hawajui Kiingereza, kuanzia wateja wa Bank hizo mpaka waajiriwa wanaongea wengi lugha vizuri ya Kiingereza. Hizo Bank ndani watanzania walioajiriwa wanaongea Kiingereza kwa ufasaha kama wazungu, usiyejua Kiingereza hupati kazi sehemu hizo.

Endeleeni kusema elimu ni uelewa wakati ulichokielewa huwezi kukielezea kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.
Hiki kitu mimi huwa kinanishangaza...

Hata kama umesoma kwa kiswahili shule ya msingi, lakini sekondari miaka 6 umesoma kwa kiingereza masomo yote, ukaenda chuoni miaka 4 ukasoma tena kwa kiingereza masomo yote, jumla miaka kumi unasoma kwa kiingereza tu, bado mtu kujieleza kwa hii lugha uliyopatia digrii yako inakuwa ni tabu, ni umbumbumbu gani huu?

Ila na wewe mleta mada sema tu unapigia debe hayo mashule yenu wanayofundisha kizungu tangu chekechea, which I strongly oppose!
 
Wengine wanakosea maneno ya kila siku, mtu anaandika Kalibu, ongera maneno ambayo haziwezi pita siku mbili hujayaona yani kusoma hawezi na picha haoni. Mtu asiye makini kiasi hiki nani ampe kazi yake?
Hizi shule wanazofundisha kizungu tangu shule ya msingi wanatuharibia watoto, siku hizi hawajui kabisa kiswahili, utasikia " nipe ela, atulipi, kila atuwa duwa, abari za hasubui...".
 
Kama kiingereza ndo ajira basi Kenya kusingekuwa na unemployed...

Na! Unafikiri kuna mzazi asiyependa mwanae asome kisasa!??

Hela ya kula tu shida....
Ukweli mchungu,tunaumia tu na kupambana angalau watoto wetu wasije pitia maisha kama yetu
 
Wewe ndiye hujui hata mambo yaliyo wazi. Lugha jifunze ukiwa mdogo. Lugha siyo ya kujifunza ukiwa mkubwa. Halafu unashangaa kwa nini wanaojifunza wakiwa wakubwa hawaongei hata wakijifunza kwa miaka 100. Mbona jibu liko wazi?
Hiki kitu mimi huwa kinanishangaza...

Hata kama umesoma kwa kiswahili shule ya msingi, lakini sekondari miaka 6 umesoma kwa kiingereza masomo yote, ukaenda chuoni miaka 4 ukasoma tena kwa kiingereza masomo yote, jumla miaka kumi unasoma kwa kiingereza tu, bado mtu kujieleza kwa hii lugha uliyopatia digrii yako inakuwa ni tabu, ni umbumbumbu gani huu?

Ila na wewe mleta mada sema tu unapigia debe hayo mashule yenu wanayofundisha kizungu tangu chekechea, which I strongly oppose!
 
Watanganyika hawa wasiojua tofauti ya R na L wala matumizi ya herufu H are doomed to fail. Lugha yao tu hawawezi ndio iwe yai! Mtu kahitimu chuo kabisa anaandika ela, akuna, apana, ongera, Kalibu nk. Kifupi hatujui Kiswahili wala kimombo.
Dah. Mwanangu mbona unatupiga na kitu kizito ssana kichwani? 😀
😀 😀 😀
 
Ni story za vijiweni

Watoto wa Tbaijuka au Migiro unafikiri wamependelewa, La hasha

Wamepewa elimu bora
Wewe bado Sana hujui maisha yanavyoendeshwa.
Network, simu ya baba, simu ya Mama inampatia kazi mtu.
Kuna dogo kajitolea miaka 3 kwenye bank. Anaenda kwenye interview za bank hiyohiyo huku barua yake ikiwa imesainiwa na branch manager na kale ka neno "I recommend him" Ila anapigwa chini.

Kuna classmate alivolunteer kwa miaka 3. Siku akaitwa kwenye interview kwenye shirika linalofanya kazi kama zilezile anazofanya kila siku. Wakamuuliza mpaka yakaisha wakaanza Kupigisha story za shirika hili na lenu lipi Bora. Mwisho wakamweka wazi kuwa Ile nafasi Ina mtu.

June mwaka Jana nikienda interview kwenye nafasi ambayo nimeitumikia miaka zaidi ya 4. Mpaka interviewer mmoja ananiambia "Sina Cha kuuliza sababu wewe unajua kila kitu". Na bado nilipigwa chini. Hii nchi iangalie tu.
 
Watanganyika hawa wasiojua tofauti ya R na L wala matumizi ya herufu H are doomed to fail. Lugha yao tu hawawezi ndio iwe yai! Mtu kahitimu chuo kabisa anaandika ela, akuna, apana, ongera, Kalibu nk. Kifupi hatujui Kiswahili wala kimombo.
Haha..!
tumekosa sisi, tumekosa sisi, tumekosa sana..!

tupo hapa tunaiomba 'serekari' yetu 'itulehemu' hivyo hivyo..!
 
Wewe bado Sana hujui maisha yanavyoendeshwa.
Network, simu ya baba, simu ya Mama inampatia kazi mtu.
Kuna dogo kajitolea miaka 3 kwenye bank. Anaenda kwenye interview za bank hiyohiyo huku barua yake ikiwa imesainiwa na branch manager na kale ka neno "I recommend him" Ila anapigwa chini.

Kuna classmate alivolunteer kwa miaka 3. Siku akaitwa kwenye interview kwenye shirika linalofanya kazi kama zilezile anazofanya kila siku. Wakamuuliza mpaka yakaisha wakaanza Kupigisha story za shirika hili na lenu lipi Bora. Mwisho wakamweka wazi kuwa Ile nafasi Ina mtu.

June mwaka Jana nikienda interview kwenye nafasi ambayo nimeitumikia miaka zaidi ya 4. Mpaka interviewer mmoja ananiambia "Sina Cha kuuliza sababu wewe unajua kila kitu". Na bado nilipigwa chini. Hii nchi iangalie tu.
🤣🤣🤣🤣Nchi nzito sana na hii
 
Wewe ndiye hujui hata mambo yaliyo wazi. Lugha jifunze ukiwa mdogo. Lugha siyo ya kujifunza ukiwa mkubwa. Halafu unashangaa kwa nini wanaojifunza wakiwa wakubwa hawaongei hata wakijifunza kwa miaka 100. Mbona jibu liko wazi?
Kiukweli mkuu nilikuwa sijui..

Hiki ulichosema ni kwa mujibu wa nini?, kuna utafiti wowote ulifanyika ukabaini hivyo au haya ni maoni yako binafsi tu?
 
Unataka utafiti hata kukwambia kuwa ukipigwa risasi ya kichwa unakufa. Kwamba Dar es Salaam iko Tanzania 🤣. Subiri tafiti sasa.
Kiukweli mkuu nilikuwa sijui..
Hiki ulichosema ni kwa mujibu wa nini?, kuna utafiti wowote ulifanyika ukabaini hivyo au haya ni maoni yako binafsi tu?
 
Kama hata kina Ridhi moko hawajui kiingereza na wamesoma internation school, unashanga nini mtoto wa namnyamba Lindi huko aliyesoma shule ya kata!!!.
 
Unataka utafiti hata kukwambia kuwa ukipigwa risasi ya kichwa unakufa. Kwamba Dar es Salaam iko Tanzania 🤣. Subiri tafiti sasa.
Kwa hiyo suala la kushindwa kujifunza lugha ngeni ukiwa mtu mzima liko wazi sawa na suala la mtu kupigwa risasi ya kichwa na kufa kiasi kwamba halihitaji utafiti?! Unazidi kunishangaza!

Unaposema "lugha jifunze ukiwa mdogo", unamaanisha udogo wa umri gani?
 
Kwa hiyo suala la kushindwa kujifunza lugha ngeni ukiwa mtu mzima liko wazi sawa na suala la mtu kupigwa risasi ya kichwa na kufa kiasi kwamba halihitaji utafiti?! Unazidi kunishangaza!

Unaposema "lugha jifunze ukiwa mdogo", unamaanisha udogo wa umri gani?
ok
 
Sipendi ubishi wa kijinga. Mi siyo mjinga. Umeshinda mkuu. Nakupa kombe🙌 🙌
Kwa hiyo suala la kushindwa kujifunza lugha ngeni ukiwa mtu mzima liko wazi sawa na suala la mtu kupigwa risasi ya kichwa na kufa kiasi kwamba halihitaji utafiti?! Unazidi kunishangaza!

Unaposema "lugha jifunze ukiwa mdogo", unamaanisha udogo wa umri gani?
 
Members, Msipende kusikiliza maneno ya sisi wanasiasa kuwa lugha ya Kiswahili ni bora na elimu ya shule za kata ni bora sana.

Hakuna mwana siasa wa zama hizi ambaye mtoto wake anasoma shule ya kata au anasoma masomo ya msingi kwa lugha ya Kiswahili.

Usahili au Interview za sasa anayejua kujieleza kwa Kiingereza kwa ufasaha zaidi ndiye anayepata ajira kwenye Makampuni na mashirika binafsi.

Sekta binafsi zinahitaji watu wanaojua lugha kwa ufasaha ya Kiingereza.

Nilifika ofisi moja hapa Tanzania, hakuna mfanyakazi wa kitanzania anayoongea kiswahili, Wote wanatumia kiingereza fasaha kuanzia mlinzi nje mpaka wahudumu ndani.

Watoto wa watu wenye uwezo na waliosoma shule za kimataifa za kiingereza ndio Wanao kwenda kuongoza sekta zote nchi hii, Na hao watoto wengi ni wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wakubwa, Wakurugenzi wa taasisi na Mashirika au wale wafanyakazi wa serikali wenye mishahara mikubwa.

Vijana wa sasa wanakosa ajira kwa kushindwa kujieleza kwa Kiingereza fasaha kwenye Usahili wa mahojiano au Oral interview.

Vijana tumieni simu zenu kujiimarisha uwezo wa kuongea Kiingereza Fasaha, Degree bila kuongea Kiingereza kwa ufasaha ajira ni ngumu kupata sekta binafsi na hata taasisi baadhi za Serikali.

Kiingereza cha kufikiria maneno kama oooh, you know sir, Infact Sir. OK no problem..... The... The.... and.... OK you know... know huwezi kupata ajira kwa sasa.

Mtoto wa kihindi Tanzania wa darasa la tano anajieleza vizuri kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.

Mtoto wa chekechea Feza na Class three IST anajieleza kwa ufasaha kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.

Zamani watu walisoma shule za Serikali na waliongea Kiingereza kwa ufasaha lakini sio kwa walimu wa sasa na shule zilizopo sasa.

Shule za Tanzania hasa za serikali na baadhi sekta binafsi walimu wenyewe tu hawajui kiingereza, Je hao wanafunzi watajua Kiingereza?

Jitihada binafsi zinahitajika kwa wahitimu wa sasa kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha.

Kila siku ajira zinatangazwa za Kitaifa na kimataifa, Lakini vijana wetu wanaogopa na hata wakiomba hawawezi kufurukuta na watoto wa nchi jirani za Kenya na Uganda.

Hata sisi wakinga siku hizi familia zetu zinasoma shule za kisasa na vyuo vya kisasa nje ya nchi.

Fuatilieni scholarship vizuri muone watoto wa viongozi wanavyohangaika kuwaombea watoto wao.

Fuatilieni mashirika makubwa ya kimataifa mtawakuta watoto wa viongozi wa kisiasa huko WHO, UNICEF, WORLD BANK, UNESCO, UNHCR, CITI BANK na Bank zote za Kimataifa wapo watoto wao wanaoongea Kiingereza kwa ufasaha.

Ofisi nyingi na Bank kubwa kubwa Dar Salaam hakuna mfanyakazi wa kitanzania anaongea kiswahili ni Kiingereza tu kilichonyooka labda waamue kukuongelesha kwa Kiswahili.

Lini ulisikia watu wenye account Citi Bank, Standard chartered Bank hawajui Kiingereza, kuanzia wateja wa Bank hizo mpaka waajiriwa wanaongea wengi lugha vizuri ya Kiingereza. Hizo Bank ndani watanzania walioajiriwa wanaongea Kiingereza kwa ufasaha kama wazungu, usiyejua Kiingereza hupati kazi sehemu hizo.

Endeleeni kusema elimu ni uelewa wakati ulichokielewa huwezi kukielezea kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.
Nasema hivi; to be born british is to win the lottery of life!!!!
Kwa wale wa saint kayumba: kuzaliwa mwingereza ni kushinda bahati nasibu ya maisha!!!
 
Back
Top Bottom