Tuache siasa, ajira zipo za kutosha Tanzania kwa wanaojua Kiingereza kwa ufasaha

Sipendi ubishi wa kijinga. Mi siyo mjinga. Umeshinda mkuu. Nakupa kombe🙌 🙌
Mimi nimeuliza swali, unasema ni ubishi wa kijinga! Kwako wewe mtu akikuuliza swali anakuwa ni mbishi wa kijinga!?

Ok! mimi sijui kama wewe ni mjinga au siyo mjinga ila ninachojua umeshindwa kujibu swali langu.

Ukisema umri mdogo, kuna mtu anamaanisha miaka mitatu hadi kumi, mtu mwingine hadi miaka 17 ni "kuwa mdogo", Kuna sehemu hadi umri wa miaka ishirini na tano(25) bado unachukuliwa ni mdogo!

Daniel Everret alizaliwa mwaka 1951, mnamo mwaka 1977 alifika katika kijiji kidogo cha Piraha kilichoko kwenye misitu ya Amazon.. Wapiraha ni jamii iliyokuwa inaongea lugha ngumu kabisa kuwahi kutokea. Lakini Daniel Everret akiwa na mkewe Keren Graham walifanikiwa kujifunza Kipiraha kwa ufasaha wakiwa katika umri wa kiutu uzima(miaka 26+) na kufanikiwa kuandika biblia ya kwanza kwa lugha ya Kipiraha.

Lakini pia, ukienda kusoma Urusi au China, ni ĺazima ujifunze lugha yao kwanza ndio uanze masomo halisi, kwa lugha yao, wengi tu wanakwenda kusoma katika hizo nchi kwa level ya Postgraduate, kwa maana wengi ni watu wazima tayari, na wanazielewa hizo lugha.

Kwa hiyo ndugu yangu usiyependa ubishi wa kijinga kwa sababu unadai kwamba wewe siyo mjinga, maelezo kwamba ili uelewe lugha inabidi ujifunze "ukiwa mdogo", ambayo kiuhalisia ni maoni yako binafsi, hayana msingi wowote, hivyo basi, NINAYAPUUZA!
Hisia zake, watu wazima wanasoma kingereza kwa Ras Simba
 
Ilikuwa zamani.nimehudhuria interview na wakenya,Uganda mpaka Malawi. Round ya kwanA tu.Alibaki mburundi na wabongo.Siku hizi wabongo wapo viuzuri mno
Ilikuwa zamani wabongo sio haba kwa sasa wapo vizuri sana
 
Kuwa konki kwenye kile unachofanya kazi zitakufata zenyewe, f*CK english. Kila siku tunafanya kazi na wazungu hawajui English hata ya kuombea maji lakini anapiga kazi mpaka unakubali.
 
🙌
 
Nikiwa nawaeleza watu hili suala huwa hawanielewi, lakin ndo Ukweli suala la kufundishia kiswahili hadi chuo kikuu tulichelewa Sana haliwezi, kutimia , Nimezunguka SA, Kenya, Uganda, Zambia kiukweli Kama hujui kingereza utapata tabu Sana kuhudumiwa , wakenya wapo vizur Sana kiswahili wanajua na pia kingereza wanajua, hata ukienda nchi yoyote kufundisha kiswahili Kama hujui kingereza wafa ndugu.
 
Heeeh!
Kumbe kuongea kiingereza ndio kuelimika??
Kwa hiyo mwanangu wa darasa la pili kumbe anaweza kupata kazi nzuri tz kisa anajua kiingereza???
Utaalam wa hiyo kzi auhusiki kabisa????
Kuna shida mahali aisee!!!!!
 
Jidanganye tu. Wachina, Wajapan na Wakorea wako hapa kwa vile wako katika makampuni yao wenyewe. Kama una kampuni yako ya ujenzi km Wachina unaweza pia kuajiri mainjinia wako wanaoongea Kisukuma tu na b

Jidanganye tu. Wachina, Wajapan na Wakorea wako hapa kwa vile wako katika makampuni yao wenyewe. Kama una kampuni yako ya ujenzi km Wachina unaweza pia kuajiri mainjinia wako wanaoongea Kisukuma tu na barabara zikajengwa.
Kuna wakorea au wachina hawana ufahamu wa kutosha wa ngeli Ila wanajua civil engineering na ujenzi unafanyika as per BOQ.

JPM kuna somo kaliweka Tz;
ujenzi wa Magomeni kota
Ujenzi wa Dodoma (mji mpya wa serikali)
Ujenzi wa Ikulu ya Dodoma kazi zinafanyika kwa kutumia TBA, SUMA JKT au Watumishi housing;
Ngeli ni lugha ya mawasiliano kama Kiswahili au mandarin.
Principles za ujenzi au uhasibu au utabibu au chochote kila, principles zikifuatwa na kama kuna right technology ipo, ngeli ni sawa na lugha Kiswahili au Vietnamise
kumpa mtu kujua nini afanye based on professional principles.






Jidanganye tu. Wachina, Wajapan na Wakorea wako hapa kwa vile wako katika makampuni yao wenyewe. Kama una kampuni yako ya ujenzi km Wachina unaweza pia kuajiri mainjinia wako wanaoongea Kisukuma tu na barabara zikajengwa.
 
Kiingereza bila hela ni sawa na kupiga kelele. By: Marehemu, Langa Kileo
 
Acha kichaa cha kulinganisha machingwa na ndizi. Ni vitu viwili tofauti. Una mtaji wewe wa kuwa na kampuni yako mwenyewe ili uajiri mainjinia Wamakonde wenzio ili muwe mnaongea Kimakonde wakati mnajenga? Wachina/Wakorea/Wajapan wana kampuni zao wenyewe. Tena ukiwa unaingea lugha yao ni rahisi kupata kazi kwao kuliko mtu anayeongea Kiingereza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…