Tuache SIASA: Dege la kwenda Geita limejaa abiria ni wengi, nimekosa siti

Tuache SIASA: Dege la kwenda Geita limejaa abiria ni wengi, nimekosa siti

Aiseee Dege limejaa Kama lote abiria ni wakumwaga tuache masikhara jamani. Wanaosema abiria hawatakuwepo ni waongo sana. Hapa nahisi nitakosa siti jamani.

View attachment 1663486
Ndege imejaa au hakuna ndege inayokwenda huko kwa hizo siku? Kuna mwenye biashara anayekataa wateja? Hivi hatujaona wenye mabasi wakiongeza uendaji wa mkoa fulani kwa siku, mfano msimu wa kawaida kuna kuwa na basi moja, ila msimu wenye abiria wengi wakaweka hata mabasi matatu? Sasa kama kweli ulichoonesha kinaakisi unachozungumzia, kuna shida gani ya kupeleka ndege mara 3 au 4 kwa siku kukidhi mahitaji ya soko?
Kiufupi ni kuwa, hakuna mwendaji huko, na ndio maana hakuna ndege iliyopangwa kwenda huko. 'No flight'!
Na sio 'over booked' au 'full'!
 
Sijui Huyu mjinga mleta post Kama atakuelewa,
Hata Geita hapajui wa Chato,hakuna mjinga yeyote anaweza kupanda ndege ya kwenda kijijini Chato alafu ageuze nyuma kwenda Geita,wakati Mwanza ni jirani sana, baada ya mapumziko ya CHATO,watuoe mrejesho,

Mleta post angejua,hata basi za Dsm Bukoba hazipiti CHATO kutokana na ukosefu abiria,badala yake basi zinapitia Biharamulo,
Hakuna utalii wowote CHATO utakao uzidi wa Katavi Mpanda.
Hujui lolote basi kutoka DSM zitapitaje chato? Route nikupitia kahama ushirombo nyakanazi. Kwan wanaoenda Mbeya wanapitaga njombe mjini? Unachomaanisha wakifika makambako waende njombe then Mbeya
 
We hope ATCL watatengeneza hela za kutosha na kuacha kujiendesha kwa hasara.
 
Unaijua route ya Songea? Miaka yote ipo na haijawahi kufa kuna nini kule cha ajabu? Hii route itaishi miaka 1000 believe me
Mkuu unakosea kuidharau Ruvuma elewa tu ni mkoa tajiri na hakuna umaskini kama mikoa mingine mingi usiwe una kariri vitu.
Ruvuma wanalima tena sana, wana madini, wana misitu ya kupanda na asili, ardhi ya kutosha, mbuga za wanayama, ziwa na mito safi, mipaka kati ya nchi, wasomi sio haba na hali ya hewa nzuri kabisa. Vyote hivi vinaupa mkoa wa Ruvuma nguvu

Songea ipo kwenye big five ya uzalishaji wa chakula nchini hakuna njaa kule asilani labda Tanzania nzima iwe na njaa

Nenda kwenye takwimu za uchumi sio mbaya acha bana kuna mikoa mingi 15 ya kichoko hapa Tanzania

Barabara za kutosha

Nendeni mkapate fursa na sio kuleta maneno ya utopolo kwa hiyo unataka kuifananisha na mikoa gani sipendi kutolea mifano mikoa ya watu lakini elewa tu Songea inafanya vema.

Mwisho wa siku tungekuwa tunaendesha nchi ki majimbo ndio ungejua wapi safi wapi babaya.
 
TISs wafanikiwa kujaza Siti za ndege kwenda chato int. airport ili kuuhadaa umma -
 
Je ukipanda ndege kuja JNIA huwa unasema unakuja Wilaya ya Ilala, Ukonga, Kipawa, Gongolamboto, Sinza au unakuja Dar?! Maana mtu anapouliza unakwenda Chato au Geita , haileti mantiki. Viwanja vya ndege vina catchment areas zake. Arusha Kia karibia kilomita 80, Musoma Mwanza 256, Kuala Lumpa mjini mpaka Airport karibia 200 kilomita. Hakuna issue hapo.
Sahihi ila muhimu ni economical viability???? Umbali si hoja sana nakubali.
Je Chato destination is it economically vibrant to justify three flights per week???????🙄🙄🙄🙄🙄
 
Back
Top Bottom