Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!

Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!

Wanabodi,
karma.jpg

Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, linapotokea jambo baya lolote, mtu unaruhusiwa kumhisi mtu yoyote kimawazo, ila huruhusiwi kumtaja wala kumuandika popote, huko ni kipiga ramli chonganishi. Ukimhisi mtu, usimtaje bali mfuatilie tuu nini kitamkuta, karma ndio itamshughulikia. Hivyo natoa wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".

Kwanza Tuendelee Kumuombea Lissu Uponyaji wa Haraka.
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!.

Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!.

Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.

Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!.

Tumuombee Lissu to Get Well Soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!.
Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!.

"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...

Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao ...


Paskali
Unataka kusemaje Pascal Njaa.
 
Wanabodi,
karma.jpg

Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, linapotokea jambo baya lolote, mtu unaruhusiwa kumhisi mtu yoyote kimawazo, ila huruhusiwi kumtaja wala kumuandika popote, huko ni kipiga ramli chonganishi. Ukimhisi mtu, usimtaje bali mfuatilie tuu nini kitamkuta, karma ndio itamshughulikia. Hivyo natoa wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".

Kwanza Tuendelee Kumuombea Lissu Uponyaji wa Haraka.
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!.

Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!.

Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.

Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!.

Tumuombee Lissu to Get Well Soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!.
Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!.

"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...

Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao ...


Paskali
Karma..Karma....Karma, hivi kuna watu wanasahau kuwa tutakufa wote, na hao wapangaji wana ya kujibu mbele za Mungu. Wale waovu, wauaji na wengine wote wana kesi za kujibu
 
Kweli KARMA ni mwamuzi mzuri..

Ukiua, nawe utauwawa tu..

Sishangai sana kwa haya yanayoendelea...

Sishangai sana Tundu Lissu akiwa na hamu kuona kisasi cha Mungu kikilipwa dhidi ya waliotaka kumuua mwaka 2017...

Bahati mbaya kuwa hawakuytumia muda huu wote kutubu. Walishupaza shingo zao. Sasa kisasi cha Bwana, Mungu Wa majeshi kinatekelezwa....
 
Kweli KARMA ni mwamuzi mzuri..

Ukiua, nawe utauwawa tu..

Sishangai sana kwa haya yanayoendelea...

Sishangai sana Tundu Lissu akiwa na hamu kuona kisasi cha Mungu kikilipwa dhidi ya waliotaka kumuua mwaka 2017...

Bahati mbaya kuwa hawakuytumia muda huu wote kutubu. Walishupaza shingo zao. Sasa kisasi cha Bwana, Mungu Wa majeshi kinatekelezwa....
Usihukumu....
P
 
Usihukumu....
P
HAPANA, sijahukumu mtu miye. Nimesema kwa kadiri ya maandiko matakatifu (Neno la Mungu - Biblia) isemavyo..

Hebu soma hapa;

WARUMI 12:19
"...wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imendikwa 'kisasi ni juu yangu Mimi; mimi nitalipa', anena BWANA..."

Unaweza pia kusoma Kumbukumbu la Sheria 32:35; Walawi 19:18; Mathayo5:39 nk nk

Kwa hiyo ndugu yangu Paschal Mayalla, tusifikiri kuwa tunapowatendea watu wengine mabaya kwa sababu na kisingizio chochote hata kama mtu huyo ni mnyonge au dhaifu kisasi gani tukadhani sisi tunaotenda unyama huo tutakuwa salama...

å Waliokosea sana waliompiga marisasi yote yale Tundu Lussu kwa sababu iwayo yoyote...

å Walikosea sana waliomuua kinyama Leopold Lwajabe kwa sababu iwayo yoyote..

å Wanakosea sana watawala wanaotumia nguvu na madaraka yao vibaya kunyanyasa wapinzani wao, wanaowakosoa kwa haki hata isivyo haki, wanaokataa kukubaliana na mawazo au Sera zao...

Watambue kuwa, anayewatetea hawa wote ni Bwana Mungu Muumba wa mbingu na nchi. Mungu anasema hivi: YEYE MWENYEWE NDIYE ALIPAYE KISASI...

Lipo lango la kukimbilia na kuepuka kisasi cha Mungu. Ni TOBA. Ni kukimbilia Golgotha msalabani pa mwokozi Yesu Kristo tukiwa na mafurushi yote ya dhambi zetu na kuzitupa hapo...


Kaka, mimi sijahukumu mtu. Nimesema kwa kuzingatia muktadha wa maandiko matakatifu - Biblia inavyosema...
 
HAPANA, sijahukumu mtu miye. Nimesema kwa kadiri ya maandiko matakatifu (Neno la Mungu - Biblia) isemavyo..

Hebu soma hapa;

WARUMI 12:19
"...wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imendikwa 'kisasi ni juu yangu Mimi; mimi nitalipa', anena BWANA..."

Unaweza pia kusoma Kumbukumbu la Sheria 32:35; Walawi 19:18; Mathayo5:39 nk nk

Kwa hiyo ndugu yangu Paschal Mayalla, tusifikiri kuwa tunapowatendea watu wengine mabaya kwa sababu na kisingizio chochote hata kama mtu huyo ni mnyonge au dhaifu kisasi gani tukadhani sisi tunaotenda unyama huo tutakuwa salama...

å Waliokosea sana waliompiga marisasi yote yale Tundu Lussu kwa sababu iwayo yoyote...

å Wanakosea sana watawala wanaotumia nguvu na madaraka yao vibaya kunyanyasa wapinzani wao, wanaowakosoa kwa haki hata isivyo haki, wanaokataa kukubaliana na mawazo au Sera zao...

Watambue kuwa, anayewatetea hawa wote ni Bwana Mungu Muumba wa mbingu na nchi. Mungu anasema hivi: YEYE MWENYEWE NDIYE ALIPAYE KISASI...

Lipo lango la kukimbilia na kuepuka kisasi cha Mungu. Ni TOBA. Ni kukimbilia Golgotha msalabani pa mwokozi Yesu Kristo tukiwa na mafurushi yote ya dhambi zetu na kuzitupa hapo...


Kaka, mimi sijahukumu mtu. Nimesema kwa kuzingatia muktadha wa maandiko matakatifu - Biblia inavyosema...
Waliomshambulia Lissu ni watu wasiojulikana.
P
 
Kisasi cha Mungu kupitia aibu ya mauti kitawaweka wazi na kisha kujulikana mmoja baada ya mwingine...

Baadhi walishatangulizwa shimoni. Shina lao ndiyo hilo taratibu linaelekea mavumbini...
Kudhanini jambo baya kulihusisha na mtu bila ushahidi wowote pia ni dhambi!.

Kumsingizia marehemu jambo lolote ni dhambi kubwa zaidi!.

P
 
Kudhanini jambo baya kulihusisha na mtu bila ushahidi wowote pia ni dhambi!.

Kumsingizia marehemu jambo lolote ni dhambi kubwa zaidi!.

P

Hasingiziwi mtu lolote..

Alikuwa ni kiongozi mwenye dhamana kubwa na nchi hii yote...

Maovu yote yalitendeka mbele ya macho yake. Hakuchukua hatua. Alinyamaza kimya...

Huwezi ukamtenga nayo yote huyu. Yalifanyika kwa amri yake, likely...
 
Hasingiziwi mtu lolote..

Alikuwa ni kiongozi mwenye dhamana kubwa na nchi hii yote...

Maovu yote yalitendeka mbele ya macho yake. Hakuchukua hatua. Alinyamaza kimya...

Huwezi ukamtenga nayo yote huyu. Yalifanyika kwa amri yake, likely...
Not necessarily, sio kweli kwasababu si kila hatua zinazochukuliwa lazima zitangazwe. Kuna mengi makubwa mazuri yanafanyika kimya kimya bila kutangazwa.

P
 
Back
Top Bottom