Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!

Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!

Not necessarily, sio kweli kwasababu si kila hatua zinazochukuliwa lazima zitangazwe. Kuna mengi makubwa mazuri yanafanyika kimya kimya bila kutangazwa.

P

Hiyo unajua wewe Paschal Mayalla..

Kuchukua hatua kisiri na kimya kimya kwa jambo ambalo linapasa hatua zichukuliwe kwa uwazi, ni kifungo chao...

Na naweza kusema bila shaka kuwa, usemalo hili ni uongo na ni kutetea uovu... Stop this pls...
 
Hiyo unajua wewe Paschal Mayalla..

Kuchukua hatua kisiri na kimya kimya kwa jambo ambalo linapasa hatua zichukuliwe kwa uwazi, ni kifungo chao...

Na naweza kusema bila shaka kuwa, usemalo hili ni uongo na ni kutetea uovu... Stop this pls...
Jee kila kitu kinachofanyika ni lazima itangazwe.
P
 
Jee kila kitu kinachofanyika ni lazima itangazwe.
P
Si lazima..

Lakini yale yazuayo sintofahamu ktk jamii, ni sharti yashughulikiwe hatua kwa hatua na kwa uwazi ili jamii iwe aware kinachoendelea kuepuka speculations kama hizi za kumshuku na kumlaumu kiongozi mkuu..

Tupende ama tusipende kuukiri ukweli, katika eneo la haki za binadamu Hayati Magufuli ali - fail spectacularly. Acha tumlaumu kabisa kabisa...

Mfano, ishu ya mauaji ya utata kukaliwa kimya bila jamii kujulishwa ilikuwaje, wahusika kina nani, wamechuliwa hatua gani, ni mbaya sana...

Tunachokuja kuelezwa na kuambiwa baadae eti ni "wasiojulikana".. This is too bad and unacceptable..

Paschal Mayalla, hakuna ishu ambayo iliweka doa la mashaka makuu ya "usafi" wa serikali ya Rais Magufuli kama assassination attempt ya Tundu Lissu mwaka 2017 huku Rais mwenyewe akionesha kutojali kana kwamba alifurahia tendo lile ovu kabisa kuwahi kutokea ktk nchi yetu...

Hii ilituthibitishia moja kwa moja kuwa, tendo lile lilikuwa na baraka zake huyu hayati. Iliendelea vilevile na hakuna lolote lililofanywa na serikali yake zaidi ya danadana na visingizio tu visivyo na mashiko...

Since then, binafsi nilitokea kumchukia Rais Magufuli kupita kiasi na kumuona kama Rais mnyama na muuaji kabisa..

I always prayed hard for KARMA to take its course...

Ni jambo la kushukuru Mungu kuwa waliodhani kuwa ni "immortal", hawawezi kufa wanaonja uchungu wa mauti kabla ya wale waliowatakia vifo kabla ya wakati...

Kweli nimeamini " KARMA" siyo mchezo..

Dawa yao ni TOBA tu. Wakili kuwa walitukosea na walitutendea mabaya sana, else watakufa vifo vibaya na vya ghafla mmoja baada ya mwingine...

Hata sisi wanyonge tunaye Mungu. Tunamwomba siku zote atupe HAKI yetu. Tunamwomba atulipie visasi kwa maadui na watesi wetu na anatusikia. Amen..
 
Si lazima..

Lakini yale yazuayo sintofahamu ktk jamii, ni sharti yashughulikiwe hatua kwa hatua na kwa uwazi ili jamii iwe aware kinachoendelea kuepuka speculations kama hizi za kumshuku na kumlaumu kiongozi mkuu..

Tupende ama tusipende kuukiri ukweli, katika eneo la haki za binadamu Hayati Magufuli ali - fail spectacularly. Acha tumlaumu kabisa kabisa...

Mfano, ishu ya mauaji ya utata kukaliwa kimya bila jamii kujulishwa ilikuwaje, wahusika kina nani, wamechuliwa hatua gani, ni mbaya sana...

Tunachokuja kuelezwa na kuambiwa baadae eti ni "wasiojulikana".. This is too bad and unacceptable..

Paschal Mayalla, hakuna ishu ambayo iliweka doa la mashaka makuu ya "usafi" wa serikali ya Rais Magufuli kama assassination attempt ya Tundu Lissu mwaka 2017 huku Rais mwenyewe akionesha kutojali kana kwamba alifurahia tendo lile ovu kabisa kuwahi kutokea ktk nchi yetu...

Hii ilituthibitishia moja kwa moja kuwa, tendo lile lilikuwa na baraka zake huyu hayati. Iliendelea vilevile na hakuna lolote lililofanywa na serikali yake zaidi ya danadana na visingizio tu visivyo na mashiko...

Since then, binafsi nilitokea kumchukia Rais Magufuli kupita kiasi na kumuona kama Rais mnyama na muuaji kabisa..

I always prayed hard for KARMA to take its course...

Ni jambo la kushukuru Mungu kuwa waliodhani kuwa ni "immortal", hawawezi kufa wanaonja uchungu wa mauti kabla ya wale waliowatakia vifo kabla ya wakati...

Kweli nimeamini " KARMA" siyo mchezo..

Dawa yao ni TOBA tu. Wakili kuwa walitukosea na walitutendea mabaya sana, else watakufa vifo vibaya na vya ghafla mmoja baada ya mwingine...

Hata sisi wanyonge tunaye Mungu. Tunamwomba siku zote atupe HAKI yetu. Tunamwomba atulipie visasi kwa maadui na watesi wetu na anatusikia. Amen..
AMEN, ila ku assume fulani anahusika katika jambo baya bila ushahidi, you just keep it in your heart, kumtaja kwa jina na huku ameisha tangulia mbele ya haki, kama hahusiki ni kumsingizia marehemu, karma yake ni mbaya, itakuhusu!. Siku zote tunasisitizwa, tusihukumu tusije tukahukumiwa.

P.
 
HAPANA, sijahukumu mtu miye. Nimesema kwa kadiri ya maandiko matakatifu (Neno la Mungu - Biblia) isemavyo..

Hebu soma hapa;

WARUMI 12:19
"...wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imendikwa 'kisasi ni juu yangu Mimi; mimi nitalipa', anena BWANA..."

Unaweza pia kusoma Kumbukumbu la Sheria 32:35; Walawi 19:18; Mathayo5:39 nk nk

Kwa hiyo ndugu yangu Paschal Mayalla, tusifikiri kuwa tunapowatendea watu wengine mabaya kwa sababu na kisingizio chochote hata kama mtu huyo ni mnyonge au dhaifu kisasi gani tukadhani sisi tunaotenda unyama huo tutakuwa salama...

å Waliokosea sana waliompiga marisasi yote yale Tundu Lussu kwa sababu iwayo yoyote...

å Walikosea sana waliomuua kinyama Leopold Lwajabe kwa sababu iwayo yoyote..

å Wanakosea sana watawala wanaotumia nguvu na madaraka yao vibaya kunyanyasa wapinzani wao, wanaowakosoa kwa haki hata isivyo haki, wanaokataa kukubaliana na mawazo au Sera zao...

Watambue kuwa, anayewatetea hawa wote ni Bwana Mungu Muumba wa mbingu na nchi. Mungu anasema hivi: YEYE MWENYEWE NDIYE ALIPAYE KISASI...

Lipo lango la kukimbilia na kuepuka kisasi cha Mungu. Ni TOBA. Ni kukimbilia Golgotha msalabani pa mwokozi Yesu Kristo tukiwa na mafurushi yote ya dhambi zetu na kuzitupa hapo...


Kaka, mimi sijahukumu mtu. Nimesema kwa kuzingatia muktadha wa maandiko matakatifu - Biblia inavyosema...
Heri sisi tulijiepusha kulipa kisasi. MUNGU WWENYEWE AMEWANYOSHA KUANZIA KULE juu kijazi, magu, Majuva......hii trinity ukikutana nayo ni kifo
 
Mungu amewa-punish sisi tulikuwa hatuwawezi
AMEN, ila ku assume fulani anahusika katika jambo baya bila ushahidi, you just keep it in your heart, kumtaja kwa jina na huku ameisha tangulia mbele ya haki, kama hahusiki ni kumsingizia marehemu, karma yake ni mbaya, itakuhusu!. Siku zote tunasisitizwa, tusihukumu tusije tukahukumiwa.

P.
 
Mie wasiwasi wangu yaliyofuata baada ya lile shambulio hapo hata kipofu alifunguliwa macho
AMEN, ila ku assume fulani anahusika katika jambo baya bila ushahidi, you just keep it in your heart, kumtaja kwa jina na huku ameisha tangulia mbele ya haki, kama hahusiki ni kumsingizia marehemu, karma yake ni mbaya, itakuhusu!. Siku zote tunasisitizwa, tusihukumu tusije tukahukumiwa.

P.
 
Leo Tarehe 7 Septembre, imetimia miaka 4 kamili tangu Tundu Lissu ashambuliwe na watu wasiojulikana ambao mpaka leo ni miaka 4, bado hawatajulikana.

Tumuombee Lissu afya njema na kwenye kuikumbuka siku hii, Mungu amuepushe kupata kitu kinachoitwa "stigimatta"

Pole sana Lissu, survival yako tuu ni muujiza, mwacheni Mungu aitwe Mungu, mengine yote mwachie Mungu.

P.
 
Wanabodi,
karma.jpg

Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, linapotokea jambo baya lolote, mtu unaruhusiwa kumhisi mtu yoyote kimawazo, ila huruhusiwi kumtaja wala kumuandika popote, huko ni kipiga ramli chonganishi. Ukimhisi mtu, usimtaje bali mfuatilie tuu nini kitamkuta, karma ndio itamshughulikia. Hivyo natoa wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".

Kwanza Tuendelee Kumuombea Lissu Uponyaji wa Haraka.
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!.

Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!.

Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.

Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!.

Tumuombee Lissu to Get Well Soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!.
Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!.

"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...

Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao ...


Paskali
Lakini hakuwa Speaker 2020, so huu uzi ulikuwa ni sawa na Ramli Chonganishi tu.
Mimi ni mpingaji mkuu wa ramli chonganishi.
P
 
ivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.
Nimeipenda sana hii aya kwani imejaa ukweli wa neno na Mungu.
 
Tunapo sema kwa Ujasiri kuwa alikuwa muovu na kibaraka wa Ibilisi muwe mnaelewa na Wala hatuna ugomvi binafsi bali ni matendo yake ya kifedhuli dhidi ya Binadamu.
Kama yule mzee hayupo motoni basi hakuna Mungu tuendelee kutenda dhambi.
Mkuu Lituye, mwisho wa uwezo wa binadaamu ni kuyasemea yale tuu ya dunia hii, mtu akiishatangulia mbele ya haki, tumzungumze kwa wema, hoja ni atakuwa wapi kama mbinguni, peponi, kuzimu, toharani, motoni au jehanamu kwenye lile ziwa la moto wa milele, hayo sio yetu ni yake YEYE Mwenyewe ndie ajuaye, jukumu letu ni always kuwaombea marehemu wote na sio kuwalaani!.
Kwa jicho la dunia hii, mtu aweza kuonekana ni mwema kama malaika na mwingine akaonekana mbaya kama shetani, halafu siku ya mwisho unaweza kushangaa na usiamini macho yako pale hao uliodhania wema wakitupwa motoni halafu wale waovu wakipeta peponi.

Mfano you will be surprised kuwakuta Osama, Saddam na Gadafi peponi halafu Bush, Blair na Obama motoni!.
Tuwaombee marehemu wote, wapate rehema kwa Mungu, wapumzike kwa amani...amen.
P
 
Ni wakati gani Wana habari mnatakiwa kuwabarisha jamii kuhusiana na uvunjifu wa katiba kama ilivyo Sasa?
Kuna watu wapo kwenye sekta muhimu na nyeti sana lakini hawajitambui tu, mojawapo ya hao watu ni waandisi wa habari...hapa Tanzania ni mabogus ziro kabisa.
Wanastahili kuuliwa na kilufutwa kabisa, jinga kwelikweli.
Duh yaani unatuombea kifo!.
Huku ni kutupigia ramli chonganishi!.
P
 
Subiri Samia afariki 2024.Hapo ndo tutajua kama Mpango atamalizia mwaka mmoja awamu ya Saba then aendelee tena 2025 -2035
Hii ni ramli chonganishi!.
P
 
Mh. Tundu Lissu awataja waliohusika kumshambulia.

Tundu Lissu amesema Walionipiga risasi ni Kikosi kazi kilichopo chini ya Rais kikisimasimaiwa na Mkuu wa TISS Kipilimba. Kikosi kazi kimeua watanzania wengi sana.

Kimeua watu wengi sana, Kilijumuisha watu wa Usalam wa taifa, Watu wa Jeshi la Wananchi, Jeshi la Polisi. Kinaitwa kikosi kazi cha kupambana na Ugaidi na madawa ya kulevya.

Watu wote waliouawa Maeneo ya Mkuranga, Kibiti Kilwa Rufiji zaidi ya watu 400. Wale waliokuwa wanatupwa mtoni maiti zinaokotwa kwenye beach, wote ni Wahanga wa Kikosi hicho.

Ndio waliomteka Ben Saanane, Azory Gwanda Mdude, Mo Dewji. Yote yalitekelezwa na hicho kikosi kazi hichi chiini ya Kipilimba ammbaye sasa ni Balozi.

Kwa maoni yangu, Tundu Lissu anahitaji ushauri nasaha. Binadamu ukipitia maswahibu na mapito kama aliyopitia, unaathirika ki fizikia, ki emosheni na kisaikolojia, (physical, emotional and psychological), hivyo anahitaji ushauri nasaha jinsi ya kutoka kwenye jinamizi hili na kuendelea na maisha.

Huku kutaja taja majina ya watu, na kutangazia ulimwengu kuwa vyombo vyetu tukuka vya ulinzi na usalama kuwa ndio walio husika, shambulio lake, bila ushahidi wowote, ni kuzidi kuibagaza tuu nchi yetu!.

Ametaja Kikosi kazi kinachojumuisha Polisi, JWTZ na TISS,, hawa ni askari wetu, trained, how could they do such a messy dirty job?. Kwa trained snipers, only one single shot would have finished the job!. Hili hata Mama Samia amewahi kuizungumzia, askari wetu trained wakimiss target by two shots, wanaandika maelezo kujieleza!.

Mimi kwa upande wangu naendelea kusisitiza Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!

Pia Lissu niliisha mshauri na namshauri tena, ajifunze kunyamaza.


Kitendo cha Rais Samia kukubali kukutana na Lissu ni uthibitisho tosha wa kauli na matendo she is healing this nation.

kwenye bandiko hilo nilisema
Kitendo cha rais Samia kukubali kukutana na Tundu Lissu, ni uthibitisho wa ile nia ya dhati ya kulioponya taifa kwa kufuata ile filosofia ya Rais Samia ni rais Watanzania wote, ni rais wa wana CCM, ni rais wa wapinzani ni rais wa Watanzania wote hata wasio na vyama, lengo la kila Mtanzania ni kuijenga Tanzania yetu, hivyo CCM na wapinzani, tunajenga nyumba moja, hatuna sababu yoyote ya kugombea fito.

Kwa vile ni mazungumzo ya faragha, Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu chini ya Mkurugenzi mpya, Zuhura Yunus (hongera), ikaeleza kuhusu mkutano huo wa Rais Samia na Tundu Lissu bila kueleza kilicho zungumzwa.

Rais wa JMT, ndiye raia number moja wa JMT na ndie Mkuu kuliko mtu mwingine yeyote kimamlaka na kimadaraka ndani ya JMT. Sasa inapotokea mtu yeyote umeomba kumuona rais na kuongea nae jambo lako lolote na rais akakukubalia kumuona na kuongea nae, ile tuu kuongea na rais ni heshima kubwa, ina maana umeaminiwa.

Hivyo Tundu Lissu kukubaliwa kukutana na rais Samia, ni Lissu ameaminiwa. "Ukiaminiwa, jiaminishe". Baada ya mazungumzo, of course, lazima kuna hoja na maombi aliwasilisha kwa rais Samia.

Kwa vile Lissu ni mtu mdogo compared to Samia, na amekutana na mtu mkubwa, rais wa JMT, baada ya kikao, ukiona mkubwa amenyamaza, na wewe mdogo nyamaza!.

Moja ya mapungufu makubwa ya upinzani wa Tanzania, ni kupayuka payuka sana, kuropoka ropoka na kupiga sana kelele kuhusu karibu kila kitu!.

Kuna mambo ya kupigia kelele na kelele zikasaidia, lakini kuna mambo ya kufanywa kimya kimya, sio kila kitu ni kupayuka, kuropoka na kupiga kelele.

Kama Lissu ameaminiwa na kuzungumzia na rais Samia in confidence, kitendo cha kusema alichozungumza ni breach of confidence. Mambo mengine ni kujifunza kunyamaza, ukiaminiwa jiaminishe.

Paskali
Ile voice note ya Lissu ni muendelezo wa ramli chonganishi!
P
 
Wanabodi,

karma.jpg

Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, linapotokea jambo baya lolote, mtu unaruhusiwa kumhisi mtu yoyote kimawazo, ila huruhusiwi kumtaja wala kumuandika popote, huko ni kipiga ramli chonganishi. Ukimhisi mtu, usimtaje bali mfuatilie tuu nini kitamkuta, karma ndio itamshughulikia. Hivyo natoa wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!"

Kwanza Tuendelee Kumuombea Lissu Uponyaji wa Haraka
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!

Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!

Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.

Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!

Tumuombee Lissu to get well soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!

Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!
Paskali
Nimeangalia mahojiano haya ya Tundu Lissu LIVE: Mahojiano na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu katika Clouds 360 kuhusu waliomshambulia ametaja jina la mtu ambaye hayupo na hawezi kujitetea!.

Kwavile kwa sasa huyo mtu hatunaye na hakuna ajuaye sababu ni kwanini alitwaliwa, it might be ni karma or any other reasons lakini sasa hayupo!, be it ni karma or not, sio busara kuendelea kumtuhumu mtu aliyetangulia mbele ya haki, ambaye hawezi kujitetea!.

Ushauri kwa Lissu, asiendelee kutaja hilo jina la huyo mtu, ikitokea hahusiki, Lissu atajichumia karma ya kuchafua majina ya watu bure, halafu karma ikimrudia watu waanze kumtafuta uchawi!.

Badala ya kutaja watu na kuwachafua, Lissu aende kwenye vyombo winavyohusika, akaripoti na kukabidhi evidence yake huko ili uchunguzi wa kijinai uanze.
P
 
Back
Top Bottom