Tuangazie tofauti za kifikra na kimwamko Tanzania dhidi ya wengine

Tuangazie tofauti za kifikra na kimwamko Tanzania dhidi ya wengine

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kuweka mizania sawa kwa minajili ya ulinganifu tuiangalie Tanzania dhidi ya wengine EA.

Nchi zote hapa kuna lugha rasmi za kibeberu yaani kiingereza au kifaransa. Kwingine kasoro Tanzania si ajabu kukuta watu wa kawaida wakiwamo boda boda, vinyozi, maseremala nk wakizimudu vilivyo lugha hizo za kujifunzia ukubwani.

Hali ni tofauti mno hapa kwetu. Tumeyaona kwa madaktari na hata maprofesa.

Yote hayo ni dalili tu ya mvua.

Kwa wenzetu mifumo ya elimu ni rafiki yenye kuwavutia wote katika jamii kujiendeleza. Kwa wenzetu si ajabu kukuta wasomi wabobezi wakifanya shughuli zinazooonekana kwetu kuwa ni za kawaida. Humo wakiwamo boda boda, madereva, wakulima, vinyozi nk.

Kwa wenzetu si ajabu kwa kada yoyote mfano boda boda, mkulima, dereva nk kujiendeleza kielimu kutokea alipo kufikia ngazi.yoyote.

Matokeo yake wenzetu ni jamii ya walioelimika juu hadi chini.

Tujilinganishe vipi nao? Mengine kwetu ni yatokanayo.

Ubora wetu kwenye u Simba na Yanga, kwenye hadithi za ngono na vikorombwezo vyake nk ni yatokanayo tu.

Ubora wetu kwenye kushabikia wanapokamuliwa wengine wasiotuhusu ni mwendelezo huo huo wa yatokanayo.

Kwa mfumo wetu huu wa elimu, kwa hakika bado tupo tupo sana.
 
Maushabiki hata huko kwao yapo. Tena kuna wale walikuwa Mashabiki ya Gorimahiya wanajiita JPM Branch.

Ushabiki hata UK upo, ishu ni kwamba hapa kwetu ushabiki tumefanya kuwa kazi rasmi, na kubet ni ajira wakati huko kwao haya ni starehe na kiburudisho tu.
 
Maushabiki hata huko kwao yapo. Tena kuna wale walikuwa Mashabiki ya Gorimahiya wanajiita JPM Branch.

Ushabiki hata UK upo, ishu ni kwamba hapa kwetu ushabiki tumefanya kuwa kazi rasmi, na kubet ni ajira wakati huko kwao haya ni starehe na kiburudisho tu.

Tofautiisha shabiki aliyeelimika na shabiki Mburura.

Mtu wa mtaani kwa wenzetu anasokota kiingereza au kifaransa kama kazaliwa huko.

Zingatia wenzetu wanazo lugha zao nyingine za msingi kama sisi.

Kulikoni sisi katika mazingira hayo hayo?
 
Nchi ya wadanyanganyika jamhuri ya wafu wanaotembea.
 
Shida kubwa kuliko ni njaa tuu huwezi mtofautisha kati ya aliyeelimika na ambaye hajaelimika wote ni mizania sawa.

Hakuna kipindi ambacho nimekuja kushushia hadhi wasomi wa kitanzania kama kipindi kilichopita .

Wasomi walikimbilia siasa na wakaiharibu siasa ,sijawahi sikia popote duniani kipimo cha kupima kitu x kinatumika kupima kitu z na jamii ya wasomi wanakubaliana na majibu ya kipimo kile
 
Shida kubwa kuliko ni njaa tuu huwezi mtofautisha kati ya aliyeelimika na ambaye hajaelimika wote ni mizania sawa.

Hakuna kipindi ambacho nimekuja kushushia hadhi wasomi wa kitanzania kama kipindi kilichopita .

Wasomi walikimbilia siasa na wakaiharibu siasa ,sijawahi sikia popote duniani kipimo cha kupima kitu x kinatumika kupima kitu z na jamii ya wasomi wanakubaliana na majibu ya kipimo kile

Lililokuwa taifa la kupigiwa Mfano halipo tena

Anasema Prof Shivji:

“Pasipo mijadala au ubunifu huwezi kuendeleza fikra, na hii inakwenda moja kwa moja kuathiri usomaji na ufundishaji.”
 
Kuweka mizania sawa kwa minajili ya ulinganifu tuiangalie Tanzania dhidi ya wengine EA.

Nchi zote hapa kuna lugha rasmi za kibeberu yaani kiingereza au kifaransa. Kwingine kasoro Tanzania si ajabu kukuta watu wa kawaida wakiwamo boda boda....
Akili za ngozi nyeusi zote zinafanana... Hakuna cha afdhari na hakuna cha maana.. waafrica wote vipaombele ni dini, uchawi, ngono na uchawi..
 
Naona kama mtu akizungumzia kueleimika na kuoevuka kifikra ni vitu viwili tofauti, kwangu mtu anaweza kuwa na elimu ya juu kabisa lakini uwezo wake wa kuchambua mambo ukawa chini kabisa.

Hili ndilo linaloikuta hii jamii yetu, kutokana na elimu tunayoipata ya kukariri madesa na kupewa degree imetufanya tuwe taifa la wasiojielewa.

Mfano wa hili utakuta unatumika vizuri sana kwa wanasiasa dhidi yetu, jamii yetu tumekuwa watu tusiojua ku-fight against our common enemy, utakuta tuna fight lakini mwisho wa siku tunabadilika kutokana na mabadiliko yanayotokea kimazingira bila kumshinda yule adui yetu wa siku zote.

Tumekuwa watu tunaobadilika kama upepo, wakati mwingine tunajikuta tuko upande wa adui bila sisi kujua, hii inasababishwa na ushabiki uliotawala vichwa vyetu, na elimu feki tulizopata huko vyuoni na kwingineko zisizokidhi viwango.
 
Akili za ngozi nyeusi zote zinafanana... Hakuna cha afdhari na hakuna cha maana.. waafrica wote vipaombele ni dini, uchawi, ngono na uchawi..

Wapi wanaweza kukubaliana na katiba kama ya kwetu? Wapi wanaweza kukubaliana na makando kando ya mamlaka kama tuyaonayi kwetu? Yako mengi.

Kwa hakika hata Congo hawawezi kukubali.

Africa tunafanana lakini sisi tumezidi.
 
Wapi wanaweza kukubaliana na katiba kama ya kwetu? Wapi wanaweza kukubaliana na makando kando ya mamlaka kama tuyaonayi kwetu? Yako mengi.

Kwa hakika hata Congo hawawezi kukubali.

Africa tunafanana lakini sisi tumezidi.
Kenya wanakatiba nzuri kuliko nchi nying za africa... Angalia kama taifa wamefika wapi.. ?? Ufisadi ejaa na hakuna cha maana...

Kongo ni nchi iliyojaa mali karibu ardhi yote na misitu ambayo wanaweza zalisha mbao karibu dunia nzima.. onana sasa iko wapi hakuna cha maana ni vita tupu ( nchi inashindwa kutawalika )
 
Kwahiyo kwako kujua Kifaransa au Kiingereza ndo kuelimika? Mie nilidhani hizo ni lugha tu elimu ni maarifa, utaalamu na ujuzi, Daktari hapimwi kwa lugha anayoongea bali uwezo wake wakutibia. Tuache huu utumwa wa kuabudu lugha za watu tuwekeze kwenye ufahamu wa watu wetu kwa lugha wanayoilewa vyema.
 
Naona kama mtu akizungumzia kueleimika na kuoevuka kifikra ni vitu viwili tofauti, kwangu mtu anaweza kuwa na elimu ya juu kabisa lakini uwezo wake wa kuchambua mambo ukawa chini kabisa...

Ni kweli kuwa ipo tofauti ya kusoma shule na kuelimika.

Hata hivyo idadi ya waliosoma bila kuelimika haiwezi kulinganishwa na wasiosoma ambao pia hawajaelimika.

Kuelimika ni suala muhimu katika kujikomboa kifikra.

Ni heri msomi asiyeelimika kuliko Mburura asiyeelimika. Na hapo ndipo tulipo sisi.
 
Kwahiyo kwako kujua Kifaransa au Kiingereza ndo kuelimika? Mie nilidhani hizo ni lugha tu elimu ni maarifa, utaalamu na ujuzi, Daktari hapimwi kwa lugha anayoongea bali uwezo wake wakutibia. Tuache huu utumwa wa kuabudu lugha za watu tuwekeze kwenye ufahamu wa watu wetu kwa lugha wanayoilewa vyema.

Umeshindwa kuona lugha imeingia je kwenye ulinganifu huu?

Umeshindwa kuona tofauti ya lugha hizi kama dalili ya mvua tu? Sisi sote si twajifunzia lugha hizi ukubwani?

Kwanini sisi huwezi kutana na mkulima dongo beshi huko akizisokota sawa sawa?

Kuna hata cha kujifariji. Mfumo wetu wa elimu umetufikisha huku wala hatuna cha kujivunia.
 
Kenya wanakatiba nzuri kuliko nchi nying za africa... Angalia kama taifa wamefika wapi.. ?? Ufisadi ejaa na hakuna cha maana...

Kongo ni nchi iliyojaa mali karibu ardhi yote na misitu ambayo wanaweza zalisha mbao karibu dunia nzima.. onana sasa iko wapi hakuna cha maana ni vita tupu ( nchi inashindwa kutawalika )

Kwa na katiba nzuri ni mwanzo wa kujikomboa. Katiba nzuri haiji kama mvua.

Vita congo si jambo baya.

Kwamba sisi hatujaamka wala kutambua umuhimu wa kupigania haki zetu tunazostahili ikiwamo katiba yenye kufaa tunaweza kujipongeza na lipi?

DRC makanisa yanahamasisha watu kusimama imara kupigania haki zao hadharani. Sisi je?

Kulinganisha na Congo na Kenya sisi tungali gizani zaidi.
 
Kwa na katiba nzuri ni mwanzo wa kujikomboa. Katiba nzuri haiji kama mvua...
Of coarse nipo na wewe kwny swala la katiba mpya nchini na kufanya evolution ya nchi yetu...

Ila nje na shidahzo.. bado africa matatizo yetu yanafanana.. mfano kama wewe unaamin mtu kujua kiingereza na lugha za nje ndio maendeleo au ndio uspmi.. wakati kiuwalisia sio hcyo kbsa... Anza kubadilika kwamza wewe ki fikra
 
Uzi wako unatufundisha nini ?

Mengi yanatokea kwetu hasi yasiyotokea kwa wenzetu. Ni nia zetu kama binadamu kuishi vyema kama wengine.

Mabadiliko huja kwa kutambua tulipoangukia Ili kusimama.

NInakazia:

"Kwa mfumo wetu huu wa elimu, kwa hakika bado tupo tupo sana."
 
Lililokuwa taifa la kupigiwa Mfano halipo tena

Anasema Prof Shivji:

“Pasipo mijadala au ubunifu huwezi kuendeleza fikra, na hii inakwenda moja kwa moja kuathiri usomaji na ufundishaji.”

Kwa hatua au hali tuliyoifikia kinapaswa kuwekeza nguvu kubwa kwa wale waliosoma na kuelimika kutumia hayo maarifa kwa ambao wako tayari kuyapokea

Maana hata tu utayari wa kuelimika hatuna kabisa , sijui itumike njia ipi Ili utayari tuwe nao sote
 
Back
Top Bottom