TUCTA: Miaka miwili ya Rais Samia ameonyesha kuthamini wafanyakazi

TUCTA: Miaka miwili ya Rais Samia ameonyesha kuthamini wafanyakazi

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limesema katika miaka miwili ya uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan amewafanyia mengi wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara watumishi wa kima cha chini kwa asilimia 23.3.

Katibu Mkuu wa Tucta, Hery Mkunda alisema hayo mjini Morogoro jana kwenye ufunguzi wa kikao cha Baraza Kuu la Tucta uliofanywa na Rais wa shirikisho hilo, Tumaini Nyamhokya.

Mkunda alisema wafanyakazi wamekuwa na matumaini makubwa kwa serikali ya Rais Samia kwa kuwa pia amepandisha madaraja ya watumishi wa sekta mbalimbali za umma.

“Katika kipindi hiki cha miaka miwili alichopo madarakani, mambo mengi ya wafanyakazi ameyagusa na wanatarajia kupata mambo mazuri zaidi katika kipindi ambacho anaendelea kuwa madarakani,” alisema na kuongeza:

“Kweli ukiangalia uwezo wa serikali kwa mambo ambayo iliyaahidi kipindi kilichopita, mengi yamefanyika kwa kiwango kikubwa sana na tunatarajia katika kipindi hiki mambo mengine mengi zaidi yatafanyika.”
291215221_1067329197237455_5769959250515085023_n.jpg
 
Watu wanavyohangaika na Hali ya uchumi.

Ukiambiwa anakuja MTU na kuongea ujinga. Watumishi wanaumia bodaboda kwenda kazin unasema serikali imefanya makubwa?? Hakuna anayeweza kufikia serikali ya jakaya.

Mshahara humohumo nauli ya boda, chakula tozo.

Asipomuiondoa mchemba tutakufa.

Kwa ufupi watumishi hawana furaha yoyote. Na Ndio maana kila uchwao ni magomvi na viongozi waangalizi.

Waangalizi wamebaki kama Tabaka tetea upuuzi. Uchumi hauwez kusogea wafanyakazi wakiwa wananung'unika mishahara haitoshelezi Kwa japo wiki Mbili
 
Viongozi wa vyama vyote vya wafanyakazi Tanzania, ni mapandikizi ya ccm.

Hawajawahi kuwa na msaada wowote ule kwa wafanyakazi wenzao. Zaidi tu ni kuimba mapambio, na kulipana posho za vikao.
 
Magufuli aaiwaahidi watumishi. Na walau marehemu alitoa Ile 50 ambayo haikuathirika na tax. Pale alitumia akili Sana fifty Ile unafeel kabisa. Juzi Ile 23.3 % yalikuwa matusi ya waziwazi Kwa watumishi. Akitokea MTU akiitaja Ile nyongeza namuona kama mwehu tu
 
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limesema katika miaka miwili ya uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan amewafanyia mengi wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara watumishi wa kima cha chini kwa asilimia 23.3.

Katibu Mkuu wa Tucta, Hery Mkunda alisema hayo mjini Morogoro jana kwenye ufunguzi wa kikao cha Baraza Kuu la Tucta uliofanywa na Rais wa shirikisho hilo, Tumaini Nyamhokya.

Mkunda alisema wafanyakazi wamekuwa na matumaini makubwa kwa serikali ya Rais Samia kwa kuwa pia amepandisha madaraja ya watumishi wa sekta mbalimbali za umma.

“Katika kipindi hiki cha miaka miwili alichopo madarakani, mambo mengi ya wafanyakazi ameyagusa na wanatarajia kupata mambo mazuri zaidi katika kipindi ambacho anaendelea kuwa madarakani,” alisema na kuongeza:

“Kweli ukiangalia uwezo wa serikali kwa mambo ambayo iliyaahidi kipindi kilichopita, mengi yamefanyika kwa kiwango kikubwa sana na tunatarajia katika kipindi hiki mambo mengine mengi zaidi yatafanyika.”
291215221_1067329197237455_5769959250515085023_n.jpg
Sis tunajua ccm imefirisika
 
Magufuli aaiwaahidi watumishi. Na walau marehemu alitoa Ile 50 ambayo haikuathirika na tax. Pale alitumia akili Sana fifty Ile unafeel kabisa. Juzi Ile 23.3 % yalikuwa matusi ya waziwazi Kwa watumishi. Akitokea MTU akiitaja Ile nyongeza namuona kama mwehu tu
Wala mchele haukuwa 4000 kama ilivyo sasa
 
Mkunda alisema wafanyakazi wamekuwa na matumaini makubwa kwa serikali ya Rais Samia kwa kuwa pia amepandisha madaraja ya watumishi wa sekta mbalimbali za umma.
Madaraja hayapandishwi na Rais bali mtumishi anatakiwa kupandishwa daraja kila baada ya miaka 4. Huyu Rais wa TUCTA ina maana hajui sheria za utumishi wa umma au anafanya hivyo kwa makusudi? Sijawahi kusikia kauli ya ovyo kama hii kutoka kwa mtu tunayetarajia akemee kitendo cha Rais kupandisha watu madaraja. Ina maana Rais akikaa miaka 8 bila kupandisha watu cheo ni sawa tu? Acheni kusikiliza ujinga wa huyu mpumbavu jamani.
 
Viongozi wa vyama vyote vya wafanyakazi Tanzania, ni mapandikizi ya ccm.

Hawajawahi kuwa na msaada wowote ule kwa wafanyakazi wenzao. Zaidi tu ni kuimba mapambio, na kulipana posho za vikao.
Kweli kabisa mkuu. Mle TUCTA imejaa mipandikizi na mikada ya CCM.
 
Viongozi wa vyama vyote vya wafanyakazi Tanzania, ni mapandikizi ya ccm.

Hawajawahi kuwa na msaada wowote ule kwa wafanyakazi wenzao. Zaidi tu ni kuimba mapambio, na kulipana posho za vikao.
Umena vyema kabisa, upumbavu wa hao makada wa CCM tumeyachoka mshahara wa utumwa, hii ni low wages, wajinga kama viongozi wa TUCTA hatutaki hata kusikia ujinga wao
 
Hii UNION ni ya kijinga.
Yatakiwa apatikane shujaa aende Mahakamani kupiga ulazima kwa kujiunga na UNION
 
Viongozi wa vyama vyote vya wafanyakazi Tanzania, ni mapandikizi ya ccm.

Hawajawahi kuwa na msaada wowote ule kwa wafanyakazi wenzao. Zaidi tu ni kuimba mapambio, na kulipana posho za vikao.
 
Back
Top Bottom